Kwanini Hans van der Pluijm anatajwa kumrithi Mwinyi Zahera Yanga
Baada ya kichapo cha juzi dhidi ya Pyramids Fc ya Misri, inaelezwa kuwa uongozi wa Yanga upo kwenye mchakato wa kuachana na Kocha wao Mkuu, Mwinyi Zahera. Maamuzi hayo yanakuja si baada tu ya mechi ya jana bali pia katika mechi za Ligi Kuu Bara ambapo Yanga imeonekana kutofanya vizuri.
Hans aliinoa Yanga kwa mafanikio miaka ya hivi karibuni na kuipa ubingwa wa Ligi Kuu mara kadhaa ambapo sasa anatajwa kutua tena Jangwani.
Hans mara ya mwisho alikuwa Kocha wa Azam FC ambayo ilimtimua mapema baada ya kuingia naye mkataba kutokana na kufanya vibaya kwenye mechi za ligi.

Comments
Post a Comment