Kuishi Na Mume

Kuishi Na Mume

Kazi ya mke ni kumtunza na kumlea mume. Si kazi rahisi. Wanawake hao ambao hawatambui sifa hii ya wajibu wao, wataona vigumu katika kutimiza kazi hii.
Ni kazi ya mwanamke ambaye anatambua kwamba kazi hii inahitaji kiwango fulani cha busara, mtindo na ustadi. Kwa mwanamke kuwa mke aliyefuzu, lazima auteke moyo wa mume wake na kuwa chanzo cha furaha kwake.
Lazima amtie moyo katika kutenda matendo mema na kumshawishi asifanye matendo maovu. Lazima pia mke achukue hatua za kutosha kutunza afya yake na ustawi wake. Matokeo ya bidii yake yanaelekezwa katika kumfanya mume awe mwema na anaye heshimika ambaye atastahili kuwa mlezi wa familia yake, na baba mzuri ambapo watoto watapata mwongozo na heshima. Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa yote amemjaalia mwanamke uwezo usio wa kawaida. Mafanikio na furaha, na pia mateso ya familia yapo mikononi mwake.
Mwanamke anaweza kuifanya nyumba kuwa pepo ya hali ya juu au jahanamu inayowaka moto. Anaweza akamfikisha mume wake kwenye kilele cha mafanikio au balaa isiyofaa. Mwanamke mwenye sifa alizopewa na Mwenyezi Mungu, ambaye anatambua wajibu wake kama mke, anaweza kumnyanyua mume wake kuwa mtu wa kuheshimika hata kama alikuwa mtu wa chini sana kuliko wote.
Mwanachuoni mmoja aliandika: Wanawake wanao uwezo wa ajabu ambao kutokana nao wanaweza kupata chochote wanachotaka.”
Katika Uislamu, mke kumtunza mume kuna daraja la maana sana. Imelinganishwa na jukumu la Jihadi (vita takatifu katika njia ya Mwenyezi Mungu). Imam Ali (a.s) alisema: “Jihadi ya mwanamke ni kumtunza mume wake vizuri.”
Fikiria kwamba Jihadi ni mapambano na vita vitakatifu katika njia ya Mwenyezi Mungu, pamoja na mapambano ya kuendeleza heshima ya Uislamu, kulinda nchi za kiislamu na kutekeleza haki katika jamii, ni mojawapo ya matendo ya kiwango cha juu sana ya ibada.
Faida ya kutekeleza majukumu ya mke mzuri, vile vile huakisiwa wakati wa kufikiriwa kwa Jihadi.
Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Mwanamke yeyote anayekufa ambapo mume wake yuko radhi naye, huingia Peponi.”
Mtume pia alisema “Kama mwanamke hatatimiza wajibu wake kama mke, hajafanya wajibu wake kwa Mwenyezi Mungu.”

Wema

Kila mtu ana hamu ya urafiki na wema. Wote wanataka kupendwa na wengine. Moyo wa mwanadamu hunemeeka kwa hilo.
Mtu ambaye hapendwi na mtu yeyote anajifikiria yeye mwenyewe kama yupo peke yake na ametelekezwa. Bibi mpendwa! Mumeo hajawa tofauti. Yeye pia anahitaji mapenzi na huba. Kabla ya kuoa mapenzi na huba ya wazazi wake yalitimiza haja hii, lakini sasa, anayo matumaini kwamba wewe ndiye utakae timiza haja hii.
Mwanaume anategemea kwa mkewe kupata urafiki na mapenzi, ambyo ni haja ya wanadamu wote. Hujitahidi sana ili apate riziki na kukufurahisha wewe.
Hushirikiana na wewe matatizo yote ya maisha, na kama mwenza wako wa kweli, anajali kukufurahisha wewe kuliko hata wazazi wako wafanyavyo. Kwa hiyo, onesha shukurani zako kwake na umpende yeye, atakupenda wewe. Mapenzi ni uhusiano wa huku na huku ambao huunganisha nyoyo.
“Mvulana wa miaka ishirini ambaye alikuja Tehran kusoma kwenye chuo Kikuu, alimpenda mjane mwenye umri wa miaka thelathini na tisa ambaye alikuwa mama mwenye nyumba wake.” Hii ni kwa sababu mwanamke huyu aliijaza nafasi tupu iliyoachwa wazi na mama yake moyoni mwake kupitia wema wake.
Kama mapenzi yanatoka sehemu zote mbili, msingi wa ndoa unakuwa na nguvu na hatari za kutengana zinaepukwa. Usifikiri kwa majivuno kwamba mumeo alikupenda wewe alipokuona mara ya kwanza, kwa sababu mapenzi ya aina hiyo hayadumu. Mapenzi yanayodumu ni yale yanayopitia kwenye wema na huba ya kudumu katika namna ya urafiki wa karibu sana.
Kama unampenda mumeo na unao urafiki mzuri naye, atafurahi na atakuwa radhi kujitahidi na kujitolea kwa ajili ya ustawi wako.
Mwanaume anayefurahia mapenzi ya mkewe, husumbuliwa na maradhi mara chache au matatizo ya mshtuko. Kama mwamaume hapewi uhusiano mwema na wa kirafiki na mkewe anaweza kukata tamaa na kuanza kuikwepa nyumba yake. Anaweza kujikuta anatumia muda wake mwingi sana katika kutafuta marafiki na watu wa kumjali. Anaweza akajisemea mwenyewe: “Kwa nini nifanye kazi na kuwasaidia watu ambao hawanitaki. Inawezekana labda nikajifurahisha mwenyewe na kujaribu kupata marafiki wa kweli.”
Mwanamke anaweza akampenda mumewe kwa uaminifu, lakini mara nyingi haoneshi au kuyadhihirishi mapenzi yake.
Haitoshi kuanzisha uhusiano wa kirafiki na kuchukulia kwamba hali hiyo ni sawa. Matamshi ya mara kwa mara kama vile, ‘ninakupenda,’ ‘umepotea machoni kwangu sana,’ Ninafurahi kukuona,’ husaidia sana kuendeleza uhusiano mzuri. Mume anapokuwa safarini, mwanamke lazima amwandikie barua kuonesha kwamba haoni raha bila kumuona.
Kama ipo simu ofisini kwa mwanamume, mke anatakiwa kumpigia simu mara kwa mara, lakini isizidi kiasi. Mke amsifu mumewe kwa marafiki na ndugu zake wakati hayupo, na kumtetea endapo mtu anamsema kwa ubaya.
Mwenyezi Mungu Mweza wa yote anazungumzia kuhusu mapatano haya ya mapenzi na huba ya mume na mke ndani ya Qur’an:
وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُمْ مِنْ أَنْفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُمْ مَوَدَّةً وَرَحْمَةً ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ {21}
“Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wenza kwa ajili yenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. hakika katika haya bila shaka; zipo Ishara kwa watu wanao fikiri ”.(Quran 30:21)
Imam Ridha (a.s) alisema: “Wanawake wengine ni baraka kwa waume zao ambao huonesha mapenzi na huba yao.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Watu walio bora sana miongoni mwa wanawake ni wale wenye mapenzi na huba.” Imam Sadiq (a.s) alisema: “Ukimpenda mtu mwoneshe kwamba unampenda.”

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU