Kuishi Na Mume

Kuishi Na Mume

Kazi ya mke ni kumtunza na kumlea mume. Si kazi rahisi. Wanawake hao ambao hawatambui sifa hii ya wajibu wao, wataona vigumu katika kutimiza kazi hii.
Ni kazi ya mwanamke ambaye anatambua kwamba kazi hii inahitaji kiwango fulani cha busara, mtindo na ustadi. Kwa mwanamke kuwa mke aliyefuzu, lazima auteke moyo wa mume wake na kuwa chanzo cha furaha kwake.
Lazima amtie moyo katika kutenda matendo mema na kumshawishi asifanye matendo maovu. Lazima pia mke achukue hatua za kutosha kutunza afya yake na ustawi wake. Matokeo ya bidii yake yanaelekezwa katika kumfanya mume awe mwema na anaye heshimika ambaye atastahili kuwa mlezi wa familia yake, na baba mzuri ambapo watoto watapata mwongozo na heshima. Mwenyezi Mungu, Mjuzi wa yote amemjaalia mwanamke uwezo usio wa kawaida. Mafanikio na furaha, na pia mateso ya familia yapo mikononi mwake.
Mwanamke anaweza kuifanya nyumba kuwa pepo ya hali ya juu au jahanamu inayowaka moto. Anaweza akamfikisha mume wake kwenye kilele cha mafanikio au balaa isiyofaa. Mwanamke mwenye sifa alizopewa na Mwenyezi Mungu, ambaye anatambua wajibu wake kama mke, anaweza kumnyanyua mume wake kuwa mtu wa kuheshimika hata kama alikuwa mtu wa chini sana kuliko wote.
Mwanachuoni mmoja aliandika: Wanawake wanao uwezo wa ajabu ambao kutokana nao wanaweza kupata chochote wanachotaka.”
Katika Uislamu, mke kumtunza mume kuna daraja la maana sana. Imelinganishwa na jukumu la Jihadi (vita takatifu katika njia ya Mwenyezi Mungu). Imam Ali (a.s) alisema: “Jihadi ya mwanamke ni kumtunza mume wake vizuri.”
Fikiria kwamba Jihadi ni mapambano na vita vitakatifu katika njia ya Mwenyezi Mungu, pamoja na mapambano ya kuendeleza heshima ya Uislamu, kulinda nchi za kiislamu na kutekeleza haki katika jamii, ni mojawapo ya matendo ya kiwango cha juu sana ya ibada.
Faida ya kutekeleza majukumu ya mke mzuri, vile vile huakisiwa wakati wa kufikiriwa kwa Jihadi.
Mtume (s.a.w.w) wa Uislamu alisema: “Mwanamke yeyote anayekufa ambapo mume wake yuko radhi naye, huingia Peponi.”
Mtume pia alisema “Kama mwanamke hatatimiza wajibu wake kama mke, hajafanya wajibu wake kwa Mwenyezi Mungu.”

Wema

Kila mtu ana hamu ya urafiki na wema. Wote wanataka kupendwa na wengine. Moyo wa mwanadamu hunemeeka kwa hilo.
Mtu ambaye hapendwi na mtu yeyote anajifikiria yeye mwenyewe kama yupo peke yake na ametelekezwa. Bibi mpendwa! Mumeo hajawa tofauti. Yeye pia anahitaji mapenzi na huba. Kabla ya kuoa mapenzi na huba ya wazazi wake yalitimiza haja hii, lakini sasa, anayo matumaini kwamba wewe ndiye utakae timiza haja hii.
Mwanaume anategemea kwa mkewe kupata urafiki na mapenzi, ambyo ni haja ya wanadamu wote. Hujitahidi sana ili apate riziki na kukufurahisha wewe.
Hushirikiana na wewe matatizo yote ya maisha, na kama mwenza wako wa kweli, anajali kukufurahisha wewe kuliko hata wazazi wako wafanyavyo. Kwa hiyo, onesha shukurani zako kwake na umpende yeye, atakupenda wewe. Mapenzi ni uhusiano wa huku na huku ambao huunganisha nyoyo.
“Mvulana wa miaka ishirini ambaye alikuja Tehran kusoma kwenye chuo Kikuu, alimpenda mjane mwenye umri wa miaka thelathini na tisa ambaye alikuwa mama mwenye nyumba wake.” Hii ni kwa sababu mwanamke huyu aliijaza nafasi tupu iliyoachwa wazi na mama yake moyoni mwake kupitia wema wake.
Kama mapenzi yanatoka sehemu zote mbili, msingi wa ndoa unakuwa na nguvu na hatari za kutengana zinaepukwa. Usifikiri kwa majivuno kwamba mumeo alikupenda wewe alipokuona mara ya kwanza, kwa sababu mapenzi ya aina hiyo hayadumu. Mapenzi yanayodumu ni yale yanayopitia kwenye wema na huba ya kudumu katika namna ya urafiki wa karibu sana.
Kama unampenda mumeo na unao urafiki mzuri naye, atafurahi na atakuwa radhi kujitahidi na kujitolea kwa ajili ya ustawi wako.
Mwanaume anayefurahia mapenzi ya mkewe, husumbuliwa na maradhi mara chache au matatizo ya mshtuko. Kama mwamaume hapewi uhusiano mwema na wa kirafiki na mkewe anaweza kukata tamaa na kuanza kuikwepa nyumba yake. Anaweza kujikuta anatumia muda wake mwingi sana katika kutafuta marafiki na watu wa kumjali. Anaweza akajisemea mwenyewe: “Kwa nini nifanye kazi na kuwasaidia watu ambao hawanitaki. Inawezekana labda nikajifurahisha mwenyewe na kujaribu kupata marafiki wa kweli.”
Mwanamke anaweza akampenda mumewe kwa uaminifu, lakini mara nyingi haoneshi au kuyadhihirishi mapenzi yake.
Haitoshi kuanzisha uhusiano wa kirafiki na kuchukulia kwamba hali hiyo ni sawa. Matamshi ya mara kwa mara kama vile, ‘ninakupenda,’ ‘umepotea machoni kwangu sana,’ Ninafurahi kukuona,’ husaidia sana kuendeleza uhusiano mzuri. Mume anapokuwa safarini, mwanamke lazima amwandikie barua kuonesha kwamba haoni raha bila kumuona.
Kama ipo simu ofisini kwa mwanamume, mke anatakiwa kumpigia simu mara kwa mara, lakini isizidi kiasi. Mke amsifu mumewe kwa marafiki na ndugu zake wakati hayupo, na kumtetea endapo mtu anamsema kwa ubaya.
Mwenyezi Mungu Mweza wa yote anazungumzia kuhusu mapatano haya ya mapenzi na huba ya mume na mke ndani ya Qur’an:
وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُمْ مِنْ أَنْفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُمْ مَوَدَّةً وَرَحْمَةً ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ {21}
“Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wenza kwa ajili yenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. hakika katika haya bila shaka; zipo Ishara kwa watu wanao fikiri ”.(Quran 30:21)
Imam Ridha (a.s) alisema: “Wanawake wengine ni baraka kwa waume zao ambao huonesha mapenzi na huba yao.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w) alisema: “Watu walio bora sana miongoni mwa wanawake ni wale wenye mapenzi na huba.” Imam Sadiq (a.s) alisema: “Ukimpenda mtu mwoneshe kwamba unampenda.”

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1