Kikwazo Kikubwa Katika Kusuluhisha Tofauti

Kikwazo kikubwa sana katika kusuluhisha ugomvi wa kifamilia ni ubinafsi na kiburi. Kwa bahati mbaya, watu wengi huathiriwa na tabia hizi. Watu kama hawa hupungukiwa na sehemu fulani ya akili ambapo hukubali tabia zao tu na kukataa za wengine na hawataki kukubali makosa yao. Hususan ni hatari sana ambapo ghasia ya tabia inafanikishwa na mtu mwingine yaani, kuwakosoa wengine kwa makosa yao. Wakati mwingine mume na mke wote husumbuliwa na tatizo hili kwa maana hiyo, watagombana kila siku. Kila mmoja atamlaumu mwenzake na wakati huo huo kila mmoja wao atakataa kuhusika kabisa na makosa yote.
Wakati mwingine kama upande moja tu utaumia kutokana na dosari hii ya kukoseana, kila mmoja atamwona mwenzake analo kosa na kwa kufanya hivyo watakuwa wanajikomboa kabisa kutokana na kulaumiana.
Pale ambapo mume na mke wote wanakumbwa na usumbufu wa vurugu hii, ni vigumu sana kuwasuluhisha, kwa sababu hawatakuwa tayari kuzingatia ushauri wa mtu yeyote. Wakati ambapo kila mmojawao anasikiliza redio au anaangalia vipindi vya runinga vinavyohusu mambo ya familia, wataona dosari fulani ya tabia ambayo inaendekezwa na mwenza wake na kwa hiyo ataanzisha lawama zake hapo hapo. Lakini dosari yoyote ikizungumziwa inayogusa udhaifu wao watajifanya hawasikii na wataelekeza fikira zao kwenye mambo mengine. Wanaweza kununua kitabu kinachohusu maadili ya familia na kumpa mwenza wake, bila wao kuwa na hisia zozote za kuwa na hamu ya kusoma yaliyomo humo.
Ubinafsi unaweza kuwa mkali sana hivyo kwamba muathirika hataweza hata kutambua tatizo hilo. Katika hali kama hiyo, uhusiano baina ya wanandoa unaharibika na hata usiwezekane kuendelea. Matokeo yake ni, ama maisha yataendelea katika hali ya ugomvi, huzuni, kutokuwa na furaha au hata kutalikiana.
Kwa hiyo, inashauriwa kwamba wanandoa wote waache tabia ya ubinafsi na kiburi. Wanandoa ambao wanatatizwa na hali hii, wanatakiwa wapate muda wakae pamoja, na wawe kama majaji wawili waaminifu wazungumzie matatizo yao. Kila mmoja amsikilize mwenzake kwa umakini na bila upendeleo wowote. Kila mmoja wao anatakiwa kufahamu dosari zake bila kusahau hata iliyo ndogo sana pamoja na nia ya kuzirekebisha. Halafu wote wawili wanatakiwa waamue kujisahihisha wao wenyewe; lakini ni hapo tu ambapo wanahisi umuhimu wa uelewano wa kina na ambapo wote wanatamaani kufufua mapenzi yao na utulivu ambao ulikuwapo baina yao.
Hata hivyo, inapokuwa hakuna uwezekano wa kupatikana suluhu, wanandoa wanatakiwa kuwasilisha matatizo yao kwa mtu mwenye uzoefu, mwaminifu, mtambuzi wa kutegemewa na mwema. Kama mtu kama huyo ni rafiki au ndugu, hiyo itakuwa nafuu yao kwa sababu wanaweza kumwambia kila kitu na kungoja hukumu yao. Lazima wamsikilize na kuupokea ushauri wake na kutia nia ya kuutekeleza kwa vitendo.
Kama ilivyo, kuamini ushauri wa jaji si rahisi, lakini mtu ambaye anajali familia yake na uimara wake, amani kudumu kwake anatakiwa kuvumilia na baadaye afurahie matokeo yake yenye manufaa.
Wazazi wa wanandoa wa aina hiyo, kama wanatambua matatizo ya kifamilia ya watoto wao, wanatakiwa kuwashauri wamuone Kadhi mwenye uzoefu, mwaminifu na nia njema. Wazazi hawatakiwi kuonesha upendeleo kwa mume au mke., Kwa njia hii, kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, matatizo yao yanaweza kutatuliwa.
Mwenyezi Mungu anasema kwenye Qurani Tukufu:

وَإِنْ خِفْتُمْ شِقَاقَ بَيْنِهِمَا فَابْعَثُوا حَكَمًا مِنْ أَهْلِهِ وَحَكَمًا مِنْ أَهْلِهَا إِنْ يُرِيدَا إِصْلَاحًا يُوَفِّقِ اللَّهُ بَيْنَهُمَا ۗ إِنَّ اللَّهَ كَانَ


عَلِيمًا خَبِيرًا

{35}

“Na mkichelea kutakuwepo mfarakano baina ya mume na mke basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke, wakitaka mapatano mwenyezi Mungu atawawezesha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye Khabari.”(Quran 4:35)

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU