Kama Allah angetaka, angepeleka dini moja tu; kwa nini aliachilia ziwe dini tatu tofauti?

Neno Uislamu hutumika katika ufahamu wa namna nyingi. Hata hivyo, jina mahususi la dini aliyotumwa kuileta Mtume Muhammad (s.a.w) pia ni Uislamu. Kwa hivyo, jina la dini alitumwa Mtume wetu na aliyotumwa Ibrahim ni tofauti. Dini hizi zina majina tofauti lakini mambo yake ni ya namna moja. Hata hivyo, kuna tofauti katika yaliyomo.
Mitume wote, tangu Adam mpaka Muhammad (s.a.w), waliwafikishia watu dini ya kweli. Kanuni za imani, ambazo ni misingi ya dini, mara zote zilibakia zilezile a namna moja. Hata hivyo, masuala ya kiibada na mambo ya kidunia, tunayoyaita shari’ah, na baadhi ya hukumu zilibadilika kwa kuzingatia mahitaji muhimu ya kilakipindi na watu kuanzia kwa Adam mpaka kwa Muhammad (s.a.w). Allah Mtukuka alittuma shari’ah tofauti kwa kila ummah kwa kuzingtattia mitindo ya kimaisha na matakwa ya watu wa kila enzi. Yafuatayo yameeleza katika aya ya 48 ya sura al-Maida:
“…Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake...”
Mathalani, Wayahudi waliabudu katika masinagogi tu na Wakristo makanisani tu; hata hivyo, sisi, Waislamu, tunaweza kufanya ibada popote. Shahamu ya ng’ombe na kondoo iliharamishwa katika shari’ah ya Musa lakini ni halali katika dini yetu.
Suala hili limeelezwa kama ifuatavyo katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur:
“Sheria takatifu zunabadilika kwa mujibu wa enzi mbalimbali. Kwa hakika, katika enzi moja huenda kukawa na Mitume zaidi ya mmoja, na hayo yalitokea. Kwa kuwa baada ya Muhuri wa Mitume, Shari'a yake tukufu inatosha kwa watu wote katika kila enzi, hakuna haja tena ya kuwa na Sheria tofauti. Hata hivyo, kwa mambo mengine baada ya hapo, haja ya madhehebu imebakia kwa kiasi.” (Sözler (Maneno), uk. 485)
“Mengi katika hayo yana manufaa kwa wakati fulani na kuleta madhara katika wakati mwingine, na dawa nyingi zilimfaa binadamu wakati wa utotoni na zikaacha kumponya katika wakati wa ujana. Hii ndio sababu Qur’an ilifuta baadhi ya matamko yake ya baadaye. Yaani, ilipitishwa hukumu kuwa wakati wake umekwisha na kwamba umewadia wakati wa hukumu zingine.” (İşarât-ül İ’caz (Alama za Kimiujiza), uk. 50)
Hukumu kuu ni zie zile kwa mitume wote; hazibadliki na wala hazifutwi. Mathalani, kanuni za imani ni zilezile kwa dini zote za kimbinguni, na ibada ipokatikazote hizo. Hata hivyo, kuna tofauti chache katika hukumu za upili (undani) za ibada. Kulikuwa na mabadiliko katikahukumu kama muundo na nyakati za swala na mwelekeo wa qiblah.
Kwa kuwa jina la dini ya wafuasi wa vitabu hivyo halikutajwa katika vitabu vya kiungu isipokuwa Quran na kwa kuwa majina ya Uyahudi na Ukristo yalitungwa baadaye na kwa kuwa wafuasi wa mitume hao waliitwa hivyo baadaye, tunadhani kuwa maana ya ibara “dini mbele ya Allah ni Uislamu (kujisalimisha Kwake)” katika Quran inafahamika vyema. Dini ambayo Mtume Muhammad (s.a.w) aliwafikishia watu ina amri za kipekee isipokuwa ukweli unaotiliwa mkazo katika Quran kuwa kitabu hiki pia kinathibitisha walicholeta mitume waliotangulia inaonesha kuwa walichofikisha kwa ujumla kilikuwa katika Uislamu isipokuwa, kutokana na hekima ya kiungu, muundokamilifu wa mafunzo hayo ulipatikana pindi alipotumwa Muhammad (s.a.w) kama mtume. Kisha, njia pekee ya kupata radhi za Allah ni kuamini yote aliyotuletea.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU