Kama Allah angetaka, angepeleka dini moja tu; kwa nini aliachilia ziwe dini tatu tofauti?
Neno Uislamu hutumika katika ufahamu wa namna nyingi. Hata hivyo, jina mahususi la dini aliyotumwa kuileta Mtume Muhammad (s.a.w) pia ni Uislamu. Kwa hivyo, jina la dini alitumwa Mtume wetu na aliyotumwa Ibrahim ni tofauti. Dini hizi zina majina tofauti lakini mambo yake ni ya namna moja. Hata hivyo, kuna tofauti katika yaliyomo.
Mitume wote, tangu Adam mpaka Muhammad (s.a.w), waliwafikishia watu dini ya kweli. Kanuni za imani, ambazo ni misingi ya dini, mara zote zilibakia zilezile a namna moja. Hata hivyo, masuala ya kiibada na mambo ya kidunia, tunayoyaita shari’ah, na baadhi ya hukumu zilibadilika kwa kuzingatia mahitaji muhimu ya kilakipindi na watu kuanzia kwa Adam mpaka kwa Muhammad (s.a.w). Allah Mtukuka alittuma shari’ah tofauti kwa kila ummah kwa kuzingtattia mitindo ya kimaisha na matakwa ya watu wa kila enzi. Yafuatayo yameeleza katika aya ya 48 ya sura al-Maida:
“…Kila mmoja katika nyinyi tumemwekea sharia yake na njia yake...”
Mathalani, Wayahudi waliabudu katika masinagogi tu na Wakristo makanisani tu; hata hivyo, sisi, Waislamu, tunaweza kufanya ibada popote. Shahamu ya ng’ombe na kondoo iliharamishwa katika shari’ah ya Musa lakini ni halali katika dini yetu.
Suala hili limeelezwa kama ifuatavyo katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur:
“Sheria takatifu zunabadilika kwa mujibu wa enzi mbalimbali. Kwa hakika, katika enzi moja huenda kukawa na Mitume zaidi ya mmoja, na hayo yalitokea. Kwa kuwa baada ya Muhuri wa Mitume, Shari'a yake tukufu inatosha kwa watu wote katika kila enzi, hakuna haja tena ya kuwa na Sheria tofauti. Hata hivyo, kwa mambo mengine baada ya hapo, haja ya madhehebu imebakia kwa kiasi.” (Sözler (Maneno), uk. 485)
“Mengi katika hayo yana manufaa kwa wakati fulani na kuleta madhara katika wakati mwingine, na dawa nyingi zilimfaa binadamu wakati wa utotoni na zikaacha kumponya katika wakati wa ujana. Hii ndio sababu Qur’an ilifuta baadhi ya matamko yake ya baadaye. Yaani, ilipitishwa hukumu kuwa wakati wake umekwisha na kwamba umewadia wakati wa hukumu zingine.” (İşarât-ül İ’caz (Alama za Kimiujiza), uk. 50)
Hukumu kuu ni zie zile kwa mitume wote; hazibadliki na wala hazifutwi. Mathalani, kanuni za imani ni zilezile kwa dini zote za kimbinguni, na ibada ipokatikazote hizo. Hata hivyo, kuna tofauti chache katika hukumu za upili (undani) za ibada. Kulikuwa na mabadiliko katikahukumu kama muundo na nyakati za swala na mwelekeo wa qiblah.
Kwa kuwa jina la dini ya wafuasi wa vitabu hivyo halikutajwa katika vitabu vya kiungu isipokuwa Quran na kwa kuwa majina ya Uyahudi na Ukristo yalitungwa baadaye na kwa kuwa wafuasi wa mitume hao waliitwa hivyo baadaye, tunadhani kuwa maana ya ibara “dini mbele ya Allah ni Uislamu (kujisalimisha Kwake)” katika Quran inafahamika vyema. Dini ambayo Mtume Muhammad (s.a.w) aliwafikishia watu ina amri za kipekee isipokuwa ukweli unaotiliwa mkazo katika Quran kuwa kitabu hiki pia kinathibitisha walicholeta mitume waliotangulia inaonesha kuwa walichofikisha kwa ujumla kilikuwa katika Uislamu isipokuwa, kutokana na hekima ya kiungu, muundokamilifu wa mafunzo hayo ulipatikana pindi alipotumwa Muhammad (s.a.w) kama mtume. Kisha, njia pekee ya kupata radhi za Allah ni kuamini yote aliyotuletea.
Maswali juuyau islamu

Comments
Post a Comment