Je wanawake wamepuuzwa katika sheria ya Kiislamu?

Dear Brother / Sister,
Katika Uislamu, wanawake wamepata nafasi na thamani wanayostahiki na wamepata amani na furaha kamili waliyoitamani mara nyingi katika historia yote. Sheria ya Kiislamu imekomesha vitendo vya kukithirisha na kupuuzia na imeweka urari na utangamano baina ya jinsia mbili.
Kwa mujibu wa Uislamu, wanawake na wanaume wako sawa kwa upande wa kuwa w Mtume Muhammad anavyolieleza hilo, “Wanadamu wote wanaume au mwanamke wako sawa kama meno ya kitana.” (Bilmen, Ömer, Nasuhi, Hukuk-u İslâmiye ve İstilahat-ı Fıkhiye Kamusu, II. 73-74).
aja aliowaumba Allah. (al-Hujurat, 13; an-Nisa 1) Kama
Wanawake na wanaume ni nusu mbili za tufaha. Aya hii inalieleza hilo vizuri zaidi:
“Wao ni vazi kwenu, na nyinyi ni vazi kwao.” (Al-Baqarah, 2:187) Kama mavazi yanavyositiri sehemu za siri, kukukingeni dhidi ya joto na baridi, basi pia msitiriane na mrekebishane kasoro zenu.
Basi mjadala ‘kama wanaume au wanawake ndio walio bora’ haufai. Tena, kwa mujibu wa maelezo katika Qur’an, wanaume wana baadhi ya sifa na fadhila, wasizokuwa nazo wanawake; halikadhalika, wanawake wana baadhi ya sifa na fadhila wasizokuwa nazo wanaume. Kwa hiyo, jinsia zote mbili zinahitajiana katika sura mbalimbali; na kwa hivyo, jinsia zote mbili zina fadhila zinazotofautiana kimaumbile. Kulinganisha nukta zinazolingana kutatufanya tufikie kwenye majibu yasiyo sahihi. (An-Nisa, 4:34)
Kwa mujibu wa Quran, mwanadamu ana sifa moja tu pasi na kujalisha jinsia. Wanawake na wanaume wanawajibishwa kwenye sifa zinazolingana za kimaadili. Kinachozingatiwa mbele ya Allah ni maadili ya kidini na taqwa. Allah anatueleza ukweli huu katika Quran kama ifuatavyo:
Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu kwa Mwenyezi Mungu ni huyo aliye mchamngu zaidi katika nyinyi.” (al-Hujurat, 13)
Kama inavyoonekana, kwa mujibu wa Quran, kwa Allah undugu hautegemei jinsia, rangi au mbari ya mtu bali juu ya “maadili bora ya Kiislamu” yaliyoelezwa na Allah. Kiukweli, Allah anaeleza kuwa muumini mwanamume au mwanamke anayefuata maadili atalipwa mema duniani na ahera:
“Mwenye kutenda mema, mwanamume au mwanamke, naye akawa ni Muumini, tutamhuisha maisha mema; na tutawapa ujira wao kwa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda.” (an-Nahl, 97)
Baada ya utangulizi huo mfupi, hebu tuangalie kwa ukaribu baadhi ya mila zilizofutwa na Uislamu kwa manufaa ya wanawake na haki ambazo Uislamu unawapa wanawake.
Baadhi ya Mila Zilizobatilishwa na Uislamu kwa manufaa ya Wanawake: Uislamu umekataa dhana kuwa wanawake wamelaaniwa, ambazo ni imani ya Wakristo na Wayahudi. Uislamu umekataza kwa nguvu desturi ya kuwazika watoto wa kike wakiwa hai, ambazo zilikuwa mila za enzi za kabla ya Uislamu Uarabuni. Mtume Muhammad (S.A.W) alitangaza kuwa hakukuwa na ndege mbaya katika chochote na kuvunja imani ya kuwaona wanawake kuwa ni nuksi. Aliwaamuru wanaume wawe na huruma sana, mapenzi na kuwajali wanawake. Aliitweza chuki dhidi ya watoto wa kike na akawasifu kwa kusema, “kuweni waadilifu wakati wa kuwapa zawadi watoto wenu; kama ningekuwa mwenye kupendelea, basi ningewapendelea watoto wa kike.” Katika kumjibu mmoja kati ya Masahaba zake aliyeuliza kuhusu nani alistahiki zaidi kuheshimiwa, alisema “Mama yako” mara tatu, katika mara ya nne alisema “Baba yako.”
2. Haki Zinazotambulika za Wanawake: Haki na wajibu ni maneno mawili pacha. Ikiwa kuna haki, lazima kuwe na wajibu pia. Sheria ya Kiislamu, ilitambua haki na uhuru wa wanawake kutoka mwanzoni kabisa na imetweza jambo la kuwadharau, umeweka majukumu juu yao. Kabla ya kuzitaja, tutakumbuka kanuni alizozitaja katika Hotuba ya Mwisho mbele ya watu 130.000:
“Enyi Watu! Ni kweli mnazo haki kwa wanawake wenu lakini nao pia wana haki juu yenu. Kumbukeni kuwa mmewachukua wawe wake zenu chini ya dhamana ya Allah na idhini yake tu. Kama watashikamana na haki zenu basi na wao wana haki ya kulishwa na kuvalishwa kwa ukarimu. Watendeeni wema na ukarimu kwani wao ni wenzenu na wasaidizi wenye kujitolea nafsi. Na pia ni haki yenu kuwa wasifanye urafiki na yeyote msiyemkubali, pia wasifanye machafu.
Katika hadithi nyingine, anasema tena, “Mcheni Allah kuhusu kutimiza haki za wanawake. Kuweni na hadhari ya kukiuka haki na uhuru wao. Kwani mmedhaminiwa hayo.” (Ajluni, Kashfu’l-Khafa, Beirut, 1351, I.36)
Baada ya majumui haya, hebu tuangalie kwa kifupi haki zinazotambuliwa za wanawake katika sheria ya Kiislamu:
Haki ya Masurufu (Nafaqa) kwa wanawake: Mume amewajibishwa kumpa masurufu mkewe na watoto aliomzalia. Yaani, wanawake wanaweza kudai masurufu kutoka kwa waume wao. Katika sheria ya Kiislamu, mume anatakiwa akidhi matumizi ya mkewe ya chakula, mavazi, makazi, na mtumishi. Wanawake wasishurutishwe kugawana uchangiaji matumizi: ni wajibu juu ya mume kuleta matumizi ya mke na watoto...
Haki ya wanawake ya kutenda: Katika sheria ya Kiislamu, wanawake wana haki ya kutenda. Wana uhuru juu ya mali zao wenyewe. Wanaweza kujipatia au kujichukulia wenyewe haki yoyote ya kiraia.
Zaidi ya hayo, uleaji watoto hupewa wanawake, kwa watoto wa kiume mpaka umri wa miaka saba, na kwa watoto wa kike mpaka waolewe.
Haki ya Mirathi: Kinyume na mifumo yote ya sheria za mila-desturia (isipokuwa Sheria za Kirumi) katika kipindi ulipoingia Uislamu, sheria ya Kiislamu ilitambua haki za wanawake katika mirathi. Desturi hii imezingatia usawa isipokuwa kwa kuwapa mafungu mawili makaka na fungu moja kwa madada miongoni mwa ndugu wa baba mmoja na mama mmoja. Mantiki ya desturi hiyo ya (fungu) moja kwa mawili imeelezwa kwa kiasi cha kutosha katika Qur’an na katika hadithi. Suala la wanawake kupunjwa katika mirathi si jambo la hakika.
Haki ya Kujifunza na Elimu kwa Wanawake: Kujifunza na elimu imekuwa na dhima kubwa katika jamii ya Kiislamu. Mwanamke ni mwalimu wa uhakika. Ni mwanamke ndiye kwa sehemu kubwa huwalea na kuwafundisha watoto. Haiingii akilini kuwa wanawake wanyimwe elimu. Mtume Muhammad (S.A.W) kila mara aliwahimiza na kuwaamrisha wanawake wajifunze kuandika na kusoma. Kulitokea idadi kubwa ya wanawake wasimulizi wa hadithi, wanafasihi wa kike, na la muhimu zaidi wanasheria wa kike katika historia ya Kiislamu.
Haki ya kufanya kazi: Wanawake wanaweza kuwa na taaluma yoyote, ambayo si kinyume na dini na maadili.
Haki nyingine ambazo Wanawake wanaweza kudai kutoka kwa Waume wao: Mwanamke anaweza kutaka mahari (mahr) yake anayostahiki kutoka kwa mumewe. Mbali na hayo, mume anatakiwa akae vyema na mkewe. Mwanamke anaweza kuzuru familia yake baada ya kumjulisha mumewe wakati wowote anapotaka kufanya hivyo. Mume ataniane na mkewe na kumruhusu kupata starehe za halali. Mume asimfanyie ukatili mkewe kwa sababu yoyote ile. Mume asifichue siri za mkewe.
Hebu tuoneshe kuwa ingawa wanawake wana haki hizo, mkuu wa familia ni mume. Hata hivyo, hiyo ni kanuni iliyochukuliwa kutoka katika mfumo wa sheria za Wayunani na Warumi. Kuafikiana na kanuni hizi hakumaanishi, kama wanavyodai baadhi ya wanasheria, kuwa zipo tofauti baina ya wanawake na wanaume. Aya inayoeleza ukweli huu kuwa mume ni mkuu wa familia pia inayakanusha madai hayo. Qur’an Tukufu inatangaza:
Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Mwenyezi Mungu baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayo yatoa.” (an-Nisa, 4:34)
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU