Je inawezekana kwetu kumuona Allah na kufahamu asili yake halisi?

Dear Brother / Sister,
Haiwezekani kwa mwanadamu kumuona Allah katika dunia hii na kufahamu asili yake halisi.
Ni kwa sababu akili na hisia za mwanadamu zina ukomo. Havitoshi kufahamu asili halisi ya Allah. Hata hivyo, mwanadamu anaweza kufahamu uwepo wake na umoja wake kwa kuangalia viumbe na kufahamu nguvu yake isiyokuwa na ukomo, na sifa zake nyingine pamoja na majina yake.
Kwa hivyo, Allah ametukataza kufikiria kuhusu dhati yake na asili yake halisi; ametuamuru kufahamu kuwepo kwake na umoja wake na kufahamu sifa zake na majina yake.
Hayo yameelezwa katika hadithi:
“Angalia mbingu na ardhi na jiangalie wewe mwenyewe ili uweze kufahamu kuwepo na umoja wa Allah; na fikiri kuhusu uzuri katika maumbile ambao hushangaza akili na kwamba haviwezi vikawepo wenyewe. Kwa sababu, hizo ni dalili zenye kuonesha kuwepo na umoja wa Allah.
Hata hivyo, usifikiri kuhusu dhati na asili halisi ya Allah. Usianze kufikiri ‘Je, Allah ni kama hivi au kama vile?’ Vipi Allah huona na kusikia? Nguvu yako haitatosha katika hilo. Hata ukijaribu vipi, huwezi kujua na kufahamu vizuri. Utachanganyikiwa. Vipimo vyako vya elimu na uzoefu havitatosheleza.
Ikiwa tutafikiri japo kidogo, tunaweza kufahamu kupitia akili zetu kwamba ni muhali kufahamu asili halisi ya Allah. Kifaranga ndani ya yai hatarajiwi kufahamu dunia iliyo nje ya yai. Akili ya mwanadamu haitofautiani na kifaranga ndani ya yai kuhusu suala la kujua ulimwengu wa kushangaza na Nyanja za ulimwengu ambazo Allah ameziumba. Hivyo, haiwezekani kwa akili ambayo imewekewa uwezo wa kufahamu wenye ukomo kufahamu asili halisi ya aliyeumba ulimwengu pale mtu anapofikiri kuhusiana na hilo kupitia akili yake.
Mehmed Kırkıncı anafafanua kuhusiana na jambo hilo kama ifuatavyo:
 “Jaalia kwamba kuna mtu ameishi ndani ya pango na kwamba hakuwahi kuona mwanga wowote na kwamba alitolewa nje ya pango mapema asubuhi kabla ya jua kuchomoza. Pale mtu huyo ambaye amepata kizunguzungu kwa mwanga ambao umekuja kutoka kila sehemu alipo ambiwa kwamba mwanga umetoka katika jua, angelishangazwa na jua hilo na angelijaribu kujua kuhusiana na jua hilo.
Ni wazi kwamba, vyovyote alivyolifikiria jua katika mawazo yake, asingeweza kulifahamu jua na angelifikiria vitu tofauti kila mara atakayojaribu kulijengea picha jua hilo. Angelilifananisha jua hilo na vitu alivyoviona;  kila mfanano ungelikuwa si sahihi.
Ikiwa kuamini juu ya jua ingelikuwa msingi wa Imani kwa mtu huyo, vyovyote angelifikiria jua angefanya shirki. Kitu pekee angeliweza kufanya ingelikuwa ni kufahamu kwamba mwanga umetoka katika jua lakini asingeliweza kujua asili halisi ya jua hilo. Kwa hakika, Imani inayotarajiwa kutoka kwake ni hiyo tu.
Kama ilivyokuwa mtu huyo katika mfano hawezi kulifahamu jua, mwanadamu hawezi kufahamu asili halisi ya mfalme aitwaye roho ambaye anatawala katika nchi ya mwili wake. Japo kuwa tunajua kwamba miili yetu hufanya kazi pamoja na roho, na kwamba mwili utashindwa kufanya kazi pale roho itakapouacha mwili huo, kwamba mfalme anautazama ulimwengu huu kupitia dirisha la jicho, anafahamu ulimwengu wa sauti kupitia sikio, na anaonja kila kitu kupitia mizani ya ulimi, sisi hatufahamu asili  halisi ya roho. Vyovyote tusemavyo kuhusiana na asili yake halisi, itakuwa ni kinyume na ukweli; vyovyote tuifikiriavyo dhati ya roho, tutafanya makosa kuhusiana na hilo.
Mwanadamu, ambaye ni dhaifu kuelewa au kufahamu dhati ya jua ambayo hakuwahi kuiona kabla na ambaye ni mjinga mno kufahamu  asili halisi ya roho yake, hawezi kumfahamu, kwa namna yoyote, muumbaji mtukufu na mmiliki wa kweli wa limwengu zote. Ambaye yupo huru kutokana na wakati pamoja na mahali; itakuwa ni kosa kubwa na uendawazimu kujaribu kuifahamu dhati yake na ni fikra isiyo ya kawaida ambayo itamfanya mwanadamu adondoke katika shirki.” .” (Hikmet Pırıltıları: Glitters of Wisdom)

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

Kisa Cha Nabii Ibraahiym عليه السلام - Sehemu Ya 1