Je inampasa Mwisilamu aongozwe na Quran au hadithi? Je Sunnah na Hadith zimegandana? Kwa kiwango gani hadithi ni za kuaminika?
Ulipotokea msambaratiko katika historia ya Uisilamu na wakati watu walipoihama Qur’an, wanazuoni wa Kiisilamu wamepekuwa na kukuta suluhisho katika Sunnah kwa sababu mwenye kuifafanua Quran bila ya shaka yoyote ni Mtume.
Wanazuoni wote wamezikubali Sunnah za Mtume (s.a.w.) kuwa ndio chanzo cha msingi cha kuifafanua Quran. Je kuna ukweli wowote ulioegemewa?
Ndio, wajibu wa utume hauishii kwa kufikisha Quran; kuifafanua, kuonesha namna itakavyotekelezwa pia ni wajibu wa Mtume. Mathalani aya zifuatazo zinachambua baadhi ya wajibu wa kiungu wa Mtume:
“Na hatukumtuma Mtume ila kwa ulimi wa kaumu yake ili apate kuwabainishia.” (Ibrahim,14-4)
“Ambao kwamba wanamfuata huyo Mtume, Nabii, asiye soma wala kuandika, wanayemkuta kaandikwa kwao katika Taurati na Injili, anaye waamrisha wema na anawakanya maovu, na anawahalalishiavizuri, na ana waharamishia viovu, na anawaondolea mizigo yao na minyororo iliyo kuwa juu yao. Basi wale waliomuamini yeye, na wakamhishimu, na wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyo teremshwa pamoja naye – hao ndio wenye kufanikiwa.” (al-Araf, 7-157)
“Haiwi kwa Muumini mwanamume wala Muumini mwanamke kuwa na khiari katika jambo, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapo kata shauri katika jambo lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake basi hakika amepotea upotofu ulio wazi.” (al-Ahzab ,33-36)
“La! Naapa kwa Mola wako Mlezi! Hawataamini mpaka wakufanye wewe ndiye muamuzi katika yale wanayo khitalifiana, kisha wasione uzito katika nyoyo zao juu ya hukumu utayo toa, na wanyenyekee kabisa.” (an-Nisa, 4-65)
“Mwenye kumt’ii Mtume basi ndio amemt’ii Mwenyezi Mungu. Na anaye kengeuka, basi Sisi hatukukutuma wewe uwe ni mlinzi wao.” (an-Nisa, 4-80)
“Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.” (al-Hashr, 59-7)
“Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu.” (Aal-e-Imran, 3-31)
Ndio, aya hizo hapo juu na mfano wa hizo zinaeleza kuwa wajibu wa Mtume wetu hauna mipaka wa kuifikisha Quran kwa watu.
Je tunaweza kulibainisha hilo?
1. Moja ya wajibu wa Mtume wetu ni kufafanua aya zilizofupishwa: Mathalani, Quran inasema, “Simamisheni sala”, lakini tusimamishe sala kwa namna gani? Inasema “Rukuuni (inamieni chini) na sajdah (sujuduni)”, lakini haitwambii kwa undani namna gani tufanye hivyo. Hakuna ufafanuni wa namna gani tufanye qiyam (tusimame wima). Mtume wetu anaifafanua ayah ii kwa muundo na maudhui, na kuonesha namna ya kutekeleza kwa kusema “Simamisheni sala kama nifanyavyo mimi”. Mtume wetu anafafanua maamrisho ya kimuhtasari ya Quran kama vile sala, funga na hajj.
2. Kufafanua aya ambazo ni ngumu kufahamika pia ni moja ya wajibu wa Mtume wetu.
Mathalani, yafuatayo yanaelezwa katika aya, “Basi waandalieni nguvu kama muwezavyo, na kwa farasi waliofungwa tayari-tayari, ili kuwatishia maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu, na wengineo ambao hamwajui, lakini Mwenyezi Mungu anawajua.” (al-Anfal,8-60). Katika aya hiyo, ibara “basi waandalieni nguvu kama muwezavyo na kwa farasi waliofungwa tayari-tayari” imetumiwa. Maswahaba wakamuuliza Mtume: “Nini nguvu?” Mtume wetu akasema, “Tambueni kwamba nguvu ni kurusha, nguvu ni kurusha, nguvu ni kurusha” mara tatu. Akatuamuru kudaka kwa kubadilisha vifaa vya kurushia kwa kila umri kwa kasi, bila ya kupoteza muda.
3. Mtume pia ameweka mipaka na kuhifadhi yasiyo na mipaka na aya jumla za Quran. Mathalani, yafuatayo yanaelezwa katika Quran, “Kakini Mwenyezi Mungu ameihalalisha biashara na ameiharamisha riba” (al-Baqara, 2-275). Kwa mujibu wa aya hii biashara ya kila kitu ni halali (imeruhusiwa). Hata hivyo, Mtume wetu ameliwekea mpaka na kukataza biashra ya nguruwe na vilevi. Hivyo, alifafanua mipaka ya biashara halali. Mfano mwengine ni aya hii: “Wale ambao wameamini, na hawakuchanganya imani yao na dhulma – hao ndio watakao pata amani na wao ndio walio ongoka.” (al-An'am, 6-82) Wakati aya hiyo ilipoteremshwa, maswahaba walimuuliza Mtume wetu: “Sote tunazidhulumu nafsi zetu. Ewe Mjumbe wa Allah, je yupo yeyote kati yetu asiyefanya kosa?” Mtume wetu (s.a.w.) akakumbusha aya “Kwa hakika shirki ndio dhambi kubwa-kabisa” na akafafanua hilo jambo ovu hapa ni shirki. Kwa hivyo, Mtume wetu anafafanua aya za Quran ambazo ni ngumu kufahamika.
3. Matukio katika Quran yalithibitishwa na kuidhinishwa na Mtume kwa kuyakariri. Hivyo, aliwafanya watu wayafahamu vizuri zaidi, ambako ndiko kulikotajwa hapa kuhusiana na suala hilo.
4. Mtume wetu pia ana mamlaka ya kisheria, yaani, anapitisha sheria ambazo hazimo ndani ya Quran. Mathalani, vyakula ambavyo ni haramu (vilivyokatazwa) vimetajwa katika aya mbili. Hata hivyo, nyama ya punda haijatajwa katika aya yoyote kati ya hizo. Mtume wetu akakataza kula nyama ya punda wa mitaani wakati wa safari ya vita vya Khaybar.
Kwa nini hazikuelezwa ndani ya Quran lakini zimeachwa kwa Mtume wetu?
Kama Quran ingetoa undani wote, kingekuwa ni kitabu chenye juzuu nyingi. Ingekuwa ni vigumu kwetu kunufaika nacho. Kwa hivyo, Quran imemwachia Mtume wetu ufafanuzi wa baadhi ya masuala. Zipo sababu nyengine za kwa nini ufafanuzi umeachwa kwa Mtume wetu. Baadhi ya masuala yalikuwa yamebatilishwa kufuatana na wakati.
Baadhi ya hadithi zimetufikia kuwa ni hadithi dhaifu. Kutekeleza kwa mujibu wa hadithi hizo dhaifu kunasababisha hitilafu. Khitilafu ni rehema kwa umma. Kama Allah ametja masuala yote kwa uhakika katika Quran, uwezekano wa hitilafu ungepungua. Unyumbukaji wa dini yetu dhidi ya mazingira ya wakati yanayobadilika na jamii ungepungua. Kwa hakika, mandhari ya juu ya dini yetu, nadhani, ni kuwa inafungua njia kwa tafsiri mpya kulingana na muda na pahala, jambo ambalo ni kitu kizuri.
Sio hayo tu. Mtume wetu ameacha mwanya kwa wanazuoni. Ndio uzuri wa dini yetu. Wanazuoni wanabainisha baadhi ya sheria za kimsingi na mitindo ya kutoa maamuzi kutekeleza kwa mujibu wa Quran na Sunnah. Wanazuoni wamefasiri masuala mapya kwa mitindo hiyo. Hivyo, tunaweza kuweka sheria zetu wenyewe kwa mazingira mapya bila ya kuhitaji sheria nyengine zozote mfumo wa kitamaduni na bila ya kuhaulisha sheria. Kwa hakika, mahitaji mapya yote yaliyotokea hadi kipindi cha mwisho cha Dola la Othmaniya yamefanywa sheria kwa kutegemea Quran na Sunnah na yamekusanywa kwenye kitabu pamoja na mfumo tunaouthamini wenyewe. Vipi watu wetu wataisoma Quran kupitia hadithi? Mathalan, sote tunasoma Sura Ya Sin kwa wingi. Kama tunataka kutambua “vipi Mtume wetu aliifasiri sura hiyo?”, tutajuaje? Kuna njia mahususi au mtindo fulani wa hilo?
Awali ya yote, Quran hufasiriwa kupitia Quran kwa sababu aya moja hufafanua aya nyengine. Suala fulani linafafanuliwa kwa namna moja katika aya fulani; katika aya nyengine, namna nyengine ya suala hilo hufafanuliwa, n.k. Hata hivyo, zipo tafsiri nyingi za Mtume wetu kuhusu Quran. Moja ya sehemu kubwa ya Bukhari ni Tafsir (tafsiri). Aidha, zipo hadithi zinazohusiana na tafsiri ambazo hazimo katika kitabu cha Bukhari wala Tirmidhi lakini zimetajwa katika vyanzo vyengine.
Kutumia sayansi ya hisabati, mimi baadhi ya wakati husema: mstari unapita kati ya nukta mbili. Vivyo hivyo, Quran ni nukta asili kuhusu maana ambayo tunaihitimisha kutokana na Quran. Kama haturejei kwenye hadithi kama ndio chanzo cha pili, kunaweza kuwa na maelfu ya mitazamo itakayoasisiwa kutoka kwenye nukta moja. Hata hivyo, ni nini dini? Ni dini ya kumpwekesha na mshikamano. Watu hawawezi kuhitimisha tafsiri tofauti kwa utashi wao kutoka kwenye aya hiyo lakini kwa kuitafsiri kwa mujibu wa ukweli. Tutapekuwa kile Mtume alichosema kuhusiana na suala hilo. Kama hakuna kitu kuhusu jambo hilo katika maneno ya Mtume, basi tutatafuta walivyosema Maswahaba wa Mtume, Tabi’in (wafwasi wa Maswahaba) na Atbaut Tabi’in (Wafwasi wa tabi’in; tutayatia akilini waliyoyasema. Wanazo fursa zaidi kuliko sisi katika kuifahamu Quran kwa mujibu wa uasili wake.
Kwa kiasi gani hadithi ni za kuaminika?
Hakuna sababu ya kwa nini tusizitegemee hadithi. Kama tulivyotaja hapo kabla, Quran inawaelekeza watu kwenye maneno ya Mtume, “Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho.” Yaani, mara zote Quran inaonesha kwa Mtume kuwa ndio chanzo cha pili.
Pili, Mtume anajiashiria mwenyewe; anavutia mazingatio kwa Sunnah zake na kueleza kuwa Uisilamu utaendelea kwa Sunnah zake. Mathalani, Bwana Mtume alimtuma Muadh nchini Yemen. Mtume alimuuliza, “Utashughulika vipi ukiwa huko?” Bwana Muadh akasema, “Nitashughulika kwa mujibu wa Quran”. Mtume wetu akauliza, “Itakuwaje ikiwa hukupata kitu kutoka katika Quran?” Akasema, “Kwa mujibu wa Sunnah zako na ikiwa sikupata kitu katika Sunnah zako, basi kwa jitihada yangu (kutoa sheria kutoka katika vyanzo asili)”. Mtume wetu akafurahishwa na majawabu yake. Hadithi hiyo ni ushahidi kwa ajili ya wanazuoni wa Uisilamu. Ni hoja kuwa Sunnah ni ushahidi na kwamba ijtihad ni muhimu. Hivyo, pale Mtume alipokuwa hai, Swahaba wamezijua hadithi kuwa ndio chanzo cha pili.
Bwana Umar anasimulia: “Nimefunga mkataba wa zamu kwa zamu na kaka yangu. Siku moja, alienda shambani na akalishughulikia; nikenda kwa Mjumbe wa Allah na kumsikiliza. Jioni, nikamjulisha kaka yangu kuhusu nilichokiona na kukisikia nilipokuwa pamoja na Mjumbe wa Allah. Kesho yake, nikenda shambani na kulishughulikia; kaka yangu akaenda kwa Mjumbe wa Allah na kumsikiliza. Jioni, aliniarifu kuhusu alichokiona na kukisikia alipokuwa na Mjumbe wa Allah. Hivyo, tuna fursa ya kumfuata Mjumbe wa Allah kwa karibu zaidi.”
Swahaba akasema: “Nilikuwa naandika kila nilichosikia kutoka kwa Mtume. Baadhi ya watu wakaniambia, ‘Mjumbe wa Allah ni binadamu pia. Wakati mwengine, anazungumza anapokuwa kakasirika na baadhi ya wakati, anapokuwa mtulivu. Sio sahihi kuandika kila anachokisema.’ Hapo, nikaacha kuandika. Hata hivyo, nikaanza kusahau nilichokisikia kutoka kwa Mtume. Kwa hivyo, nikenda kwa Mtume na kumwambia kuhusu suala hili. ‘Ewe Mjumbe wa Allah! Nimesikia habari nzuri kutoka kwako na nikaziandika lakini baadhi ya watu kutoka Ansar wamesema jambo. Kwa hivyo, nikaacha kuandika. Hata hivyo, nahisi sio rahisi kama siandiki. Nifanyeje? Mjumbe wa Allah akaashiria mdomo wake na kusema, ‘Hakuna chochote isipokuwa ni ukweli tu unaotoka katika kinywa hiki. Andika.’
Baadhi ya watu wamemjia Mjumbe wa Allah na kumlalamikia kuhusu hifadhi yao. Akawaambia, “Ombeni msaada wa mikono yenu ya kulia” akiwashauri kuandika.
Wacha niseme kitu kingine. Anas (Allah amridhie) amesimulia hadithi nyingi na yeye ni mmoja kati ya watu saba waliosimulia hadithi nyingi. Katika hadithi fulani nimeisoma katika Mustadrak, Bwana Anas anasema, “Nimeandika hadithi kutoka kwa Mjumbe wa Allah wakati wa mchana na kumsomea wakati wa usiku hivyo akawa anazisahihisha.” Yaani, Mtume wetu alisahihisha kile alichokiandika. Baada ya hayo, katika sayansi ya hadithi, wanafunzi huchukua hadithi walizojifunza kuzipeleka kwa walimu wao na kuwawasilishia. Wanafunzi huzisoma hadithi walizoziandika na kuzihifadhi mbele ya walimu wao; walimu huwasahihisha na kisha kuwapa wanafunzi stashahada.
Je tunaweza kusema kuwa hadithi zote ni tafsiri ya Quran?
Ndio tunaweza kusema hivyo. Mtume wetu (s.a.w.) aliitumia Quran katika maisha yake. Kwa hivyo, mfumo bora wa maisha ambao Quran unawataka watu umedhihirishwa kwa Mtume wetu (s.a.w.) Tukiuzingatia kwa mtazamo wa ibada, Mtume wetu ametuonesha namna ya kumwabudu Allah kunavotakiwa kuwe kamilifu. Mtume wetu ametekeleza aina zote za ibada kwa namna sahihi. Ibada ya Mtume wetu ni namna kamilifu ya kuabudu ambako Quran inatutaka tufanye kwa hali zote. Ni kitu hicho hicho kinafaa kwa mahusiano ya binadamu pia. Mtume wetu ametuonesha mifano bora zaidi katika uhusiano wake na watu na majirani zake. Pia ametuonesha mifano bora zaidi ya uhusiano wa mume na mke. Ametuonesha namna ya kukaa na watoto.
Hivyo, Mtume wetu (s.a.w.) amewakilisha vitendo na kuonesha mifano bora ya Quran katika hatua zote, vitengo na nyakati za maisha yake. Waisilamu wanaweza kuzichukua kama zilivyo kutoka kwa Mtume kwa kiasi kikubwa wawezacho. Katika hadithi, Bibi Aisha anaelezea maadili ya Mtume kuwa ni, “Maadili yake ni maadili ya Quran.” Kwa hivyo, Mtume wetu amefafanua maadili ya Quran kwa upande wa maadili. Labda, hakufafanua kila kitu kwa kusema kwa mdomo lakini alifanya kwa vitendo. Kila neno, tendo na ishara ya Mtume ni tafsiri ya roho ya Quran.
Kwa upande mwengine, alifafanua habari za mataifa yaliyopita. Katika hadithi, tunaweza kuona baadhi ya matukio kuhusu Bwana Ibrahim (Abraham) ambayo hayamo katika Quran. Hivyo, tunakuta masomo yote ambayo Quran inataka kuyataja, kuyaleta kwa watu kwa upande wa sheria, maadili na mfumo wa maisha katika maisha ya Bwana Mtume baadhi ya wakati kwa maneno yake, na wakati mwengine kwa amali zake na wakati mwengine kwa uchanganuo wake.
Yafuatayo yanaelezwa katika Quran,”kuleni na kunyweni: lakini msifanye israfu”. Katika aya nyengine, ufujaji umekatazwa. Ufujaji ni ndugu wa israfu. Hebu tuangalie utendaji wa Mtume ili tufahamu aya mbili hizo vizuri: Mtume wetu ameweka wazi mpaka wa israfu; mfano hai wa hilo ni wudu (udhu). Alipotia udhu, alitumia maji kwa uangalifu hivyo hakufanya israfu. Akatuamuru kuosha viungo vyetu kwa maji mara tatu-tatu tukiwa tunatawadha. Kutumia maji mengi zaidi ni makrooh (karaha). Akaweka mpaka huo. Mmoja ya Maswahaba alistaajabishwa na kuuliza: “Ewe Mjumbe wa Allah! Ni kwa ajili ya kuhifadhi maji?” Akajibu, “Hapana, hata kama ukiwa karibu na mto, utaosha viungo vyako mara tatu.”
Nimeona masimulizi kutoka kwa Abu ad-Darda katika hadithi: “Wakati mmoja, Mtume wetu aliwasili mtoni akiwa njiani kuelekea pahala fulani. Wakamletea bakuli la maji kutoka mtoni. Akatawadha kwa kutumia maji hayo na maji mengine yakabakia. Ni kawaida kwetu kuyamwaga pembezoni. Hata hivyo, Mtume wetu akasema, “Nenda kayamimine mtoni. Yanaweza kuwa ni kinywaji cha kiumbe fulani baadaye.”
Tukila zaidi ya tunavyohitaji, tukizungumza zaidi ya ulazima, tukitumia muda wetu ovyo, tunavipoteza. Ni upotevu ambao hatuwezi kuurejesha tena. Kuwasha kiberiti pia ni upotezaji. Ni makrooh. Ukweli kwamba Mtume ametwambia tusiyapoteze maji tukiwa tunatia udhu mara tano kwa siku, alitupa somo la kuheshimu uasili. Anatufundisha kwamba ufujaji ni swala hatari katika nyanja nyengine za maisha kupitia mfano wa udhu.
Sasa, hebu tuangalie ufafanuzi wa aya, “msifanye israfu”. Hivyo, tukiisoma aya hiyo, tunahitajika kurejea kwenye hadithi ili kuona namna aya hiyo inavyofafanuliwa. Utamaduni mpana wa hadithi yetu ni, kila tutakavyoielewa vyema basi tutaifahamu Quran. Je naweza kusema jambo kama hili kuwa ndio hitimisho? Tunaposoma aya katika Quran, tunapaswa tujaribu kuifahamu maana na tafsiri ya Quran. Hata hivyo, haitoshi kwetu, bali tunapaswa tuongeze utamaduni wa hadithi yetu. Tunapaswa tujifunze hadithi nyingi na kuyatengeneza maisha yetu kupitia hadithi hizo. Tunaposoma Quran kama hivyo, itakuwa kama tunajifunza maana ya Quran kutoka kwa Mtume.
Bila ya shaka. Wanazuoni wetu waliolifahamu hilo kwa namna hiyo, kwa mfano, Tabari, ameandika hadithi zote alizozikumbuka kuhusu aya. Baadhi ya watu wakamkosoa Tabari kwa sababu ameripoti hadithi nyingi. Tafsiri yake nyingi ya juzuu arubaini imejaa hadithi. Hata hivyo, tunapozirejea hadithi, tunazifahamu aya vizuri zaidi. Mwanga unaotolewa na hadithi ni tofauti na maana tunayoifasiri kwa kutafakari. Kwa maoni yangu, ni vyema zaidi kujaribu kuifahamu Quran kupitia hadithi.
Je Sunnah na hadithi ni kitu kimoja?
Je Sunnah, maisha ya Mtume wetu inamuunganisha Mwisilamu; je waifuate?
Tutalishughulikia suala hilo kwa mujibu wa hadithi na mitazamo ya wanazuoni.
1. Quran: Zipo baadhi ya aya zinaonesha kuwa Bwana Mtume anapokea ufunuo mwengine usiokuwa Quran (1) pia.
Baadhi ya hizo ni kama ifuatavyo:
1- Inafahamika kutokana na aya zifuatazo kuwa Mtume wetu alipewa hekima pamoja na Kitabu kitukufu: ‘Hakika Mwenyezi Mungu amewafanyia wema mkubwa Waumini vile alivyo waletea Mtume aliye miongoni mwao wenyewe, anaye wasomea Aya zake, na anawatakasa, na anawafunza Kitabu na hikima’, (2) ‘Na Mwenyezi Mungu amekuteremshia Kitabu na hikima’, (3).
Maneno hayo mawili yana mfanano na utofauti. Kwa mujibu wake, kwa kuwa kilichokusudiwa na Kitabu kitukufu ni Quran, hekima inalazimika kiwe ni kitu kingine. Uwezekano kwamba ni Sunnah unakubalika. (4) Ni nukta ya kutofautiana. Nukta ya kufanana ni kwamba vyote viwili vinatokana na ufunuo. (5)
2- Ahadi iliyoelezwa katika aya ifuatayo wamepewa Waisilamu lakini haikuelezwa katika aya hiyo ilikuwa ni nini: “Na Mwenyezi Mungu alipo kuahidini kuwa moja katika makundi mawili ni lenu” (6). Inathibitisha kuwa inaarifiwa kupitia namna nyengine ya ufunuo.
3- Aya ifuatayo inathibitisha waziwazi kuwa upo ufunuo mbali na Quran: “Na Nabii alipomwambia mmoja wa wake zake jambo la siri. Basi alipo litangaza yule mke, na Mwenyezi Mungu akamdhihirishia Mtume, alimjuvya sehemu na akaacha sehemu nyengine. Alipo mwambia hayo, huyo mke akasema: Nani aliye kwambia haya? Mtume akasema: Kaniambia Mjuzi Mwenye khabari zote!” (7) Licha ya kuwa hakuna ufafanuzi kuhusu kufichua siri katika Quran, Mtume anayajua hayo. Ni wazi kuwa upo ufunuo ambao haukujumuishwa katika Quran kwa kuwa hawezi kujua kivyakevyake na kwa kuwa inaelezwa kuwa Allah alimpa khabari.
2. Hadithi:
1- Kwa mujibu wa masimulizi ya Miqdad b. Ma’dikarib, Mjumbe wa Allah (s.a.w.) amesema yafuatayo: “…Nimepewa Kitabu na mfano wake”. (8)
2- Hadithi Qudsi: (9) ibara zifuatazo zilizomo katika hadithi za aina hii: “Mjumbe wa Allah ameeleza yafuatayo katika hadithi aliyoipokea kutoka kwa Mola wake Mlezi”, “Allah ameeleza yafuatayo katika hadithi kuwa Mjumbe wa Allah (s.a.w.) amesimulia” na ukweli kuwa hadithi hizo zimeanzia na maneno “Ewe mja wangu” zinathibitisha kuwa Bwana Mtume amepokea ufunuo mwengine usiokuwa Quran.
3- Tukio mashuhuri linalofahamika kuwa ni Jibiril (Jibrilu) hadithi: (10). Jibril alikuja katika umbile la binadamu, akiuliza maswali na kupokea majibu; Bwana Mtume aliwaambia maswahaba zake kuwa alikuwa ni Jibril na kwamba amekuja kuwafundisha dini.
4- Maneno ya Bwana Mtume (s.a.w.) kama vile ‘kwa uhakika Mola wangu Mlezi amenifunulia, (11) Nimeamrishwa, Nimekatazwa, (12) na ukweli kwamba alisema Jibril amemfundisha mambo fulani (13) yanathibitisha pia kuwepo ufunuo mwengine usiokuwa Quran. (14) Ukweli kwamba Bwana Mtume amesema “kwa kweli sikujua kuhusu hayo lakini Allah ameniambia” alipoyajibu maswali ya Myahudi” (15) yanaunga mkono suala hilo.
3. Mitazamo ya Wanazuoni:
Maswahaba wa Mtume walitambua kuwa Mtume wetu (s.a.w.) amepokea ufunuo mwengine zaidi ya Quran kutokana na matendo yake, ufafanuzi wake na maneno. Waliyasema hayo mara nyingi. Wanazuoni pia walitoa mitazamo yao kuhusu asili ya Sunnah inayoegemea kwenye hadithi na maneno ya maswahaba; wengi wao wameelezea kuwa chanzo cha Sunnah kiliegemea kwenye ufunuo.
Bibi Aisha (Allah amridhie) amesema kuwa kulikuwa na ufunuo kuhusu Bibi Khadija na kwamba amepewa kasri Peponi.
Maneno yaliyopo katika masimulizi: Jibril ameteremsha Sunnah kama alivyoteremsha Quran kunaonesha kwamba upo ufunuo mwengine usiokuwa Quran. (16) kwa kuongezea, ukweli kwamba Mtume amepokea habari kama kuwatendea wema majirani, kutawadha (udhu), kusimamisha sala, kutamka talbiya, kusimamisha sala kwenye Bonde tukufu la Aqiq, nyakati za sala, mlango wa pepo ambao umma wa Muhammad utaingilia, jina la Bwana Hamza (Allah amridhie) yameandikwa katika ubao na viumbe wa mbinguni (17) kunaonesha kwamba upo ufunuo mwengine usiokuwa Quran.
Tawus anasema kuwa yeye mwenyewe anayo maandishi yaliyoletwa na ufunuo kuhusu diyah (pesa ya damu, kikombozi/fidia) na kwamba hukumu kuhusu zakat na diyah zimekuja kwa ufunuo. (18)
Kwa kusema, “pindi hadithi inapotoka kwa Mjumbe wa Allah (s.a.w.) inapokufikia wewe, usitoe hukumu kinyume nayo; kwa sababu Mjumbe wa Allah (s.a.w.) alikuwa ni mfikishaji kutoka kwa Allah, Aliye Juu” (19) Awza ameeleza kuwa sunnah zimeegemea kwenye ufunuo.
Kama tulivyotaja kabla, mtu mwenye kutoa ufafanuzi muhimu kuhusu suala hilo alikuwa ni Imam Shafi. (20) Kwa mujibu wa ufahamu kuwa anaegemea kwa mtu ambaye elimu yake anaitegemea na kuwa yeye mwenyewe pia amekubali, Sunnah ima ni ufunuo, au maelezo ya ufunuo au ni kitu ambacho Allah amemkabidhi. Umeegemea zaidi kwenye utume wake ambao ni mahususi kwake na hekima kuwa Allah anamhamasisha umeegemea huko. Haijalishi ni upi kati ya vibadala hivyo ni chenye kukubalika, Allah ameamrisha watu kumtii Mjumbe wa Allah na kutenda kwa mujibu wa Sunnah. Ufafanuzi wa Quran kwa Sunnah unatokea ima kwa utume kuja kutoka kwa Allah, au kwa msukumo au kwa “amri” aliyopewa.
Ibn Hazm, anaekubaliana na mtazamo huo huo, anaelezea sunnah kuwa ni ufunuo usio-somwa (ghayr matluw) na anasema kuwa ni lazima kutii sunnah, ambazo ni ufunuo wa pili kama ilivyolazimika kuitii Quran. Vyote ni sawasawa katika hilo vyote vimeungana na vyote vinatoka kwa Allah. (21)
Ghazali anaeleza kuwa sunnah zinategemea ufunuo na kwamba ni ufunuo usio-somwa. (22)
Kama sunnah zote zinazingatiwa kuwa ni ufunuo, itakuwa ni wazi papo hapo kwamba Bwana Mtume (s.a.w.) hawezi kuzibadili Sunnah kama alivyokuwa hawezi kuibadili Quran. (23)
Hapa panaibuka suala muhimu pamoja na ufahamu kwamba sunnah zote zinategemea ufunuo kama ilivyo Quran. Kama Bwana Mtume (s.a.w.) aliusubiria ufunuo wa sunnah kama aya za Quran katika kila hali na tukio, mashauriano yake na jitihada zake zingeshughulikiwa vipi? Kwa hakika kuna baadhi ya nyakati alikuwa akisubiri ufunuo lakini kufikiria na kukubali kuwa alitenda kama hivyo katika kila hatua ya maisha yake kutasababisha matatizo.
Kutokana na hali hizo, baadhi ya wanazuoni wamekuwa na mtizamo kwamba si sunnah zote bali baadhi yake zilitegemea ufunuo na baadhi yake zilitegemea mazingira kama vile jitihada na mashauriano
Mathalani, Ibn Qutayba anasema yafuatayo, kukigawa chanzo cha sunnah katika sehemu tatu:
a) sunnah ambazo Jibri amezileta kutoka kwa Allah. (24)
b) sunnah ambazo Allah ameziacha kwa Mjumbe Wake (s.a.w.), ambazo Amemtaka kutoa mtazamo wake. (25)
c) sunnah ambazo Mjumbe wa Allah amezitekeleza kwa ajili ya adab; sunnah ambazo mtu anapata thawabu anapozifanya lakini hapati adhabu anapoziwacha. (26)
Sarakhsi wa Hanafi, aliyeupitisha mtazamo huo huo, anasema kuwa hukumu ambazo Bwana Mtume amezitoa zilizotegemea mawazo yake na jitihada ni kama ufunuo:
Ufunuo unakusanya sehemu mbili:
1- Ufunuo wa waziwazi. Umegawika sehemu tatu.
a) Ufunuo ambao unakuja kupitia ulimi wa malaika, unaodirikiwa na sikio na kwamba unatambulika kwa uhakika kuja kutoka kwa Allah. Sehemu hii ni ufunuo wa Quran.
b) Ufunuo ambao unafafanuliwa kwa Mtume na malaika kupitia ishara, bila ya hata neno moja. (27)
c) Msukumo. Ni udhihirisho wa kiungu katika moyo wa Mjumbe wa Allah (s.a.w.) bila ya kuwa na shaka yoyote. Mwangaza huchomoza moyoni mwake na hukumu kuhusu suala husika inakuwa waziwazi.
2- Ufunuo wa siri: Unaitwa “ma yushbihu’l-wahy” (unaofanana na ufunuo), Sarakhsi anasema kuwa zipo hukumu ambazo Mjumbe wa Allah (s.a.w.) zimemfikia kupitia mawazo yake na jitihada. Ukweli kwamba hakuachwa burebure kufanya makosa na kuwa mara zote alikuwa chini ya udhibiti wa ufunuo akitoa hukumu za namna hiyo kama ufunuo. Jitihada za watu wengine kutoka umma wake hazipo kama jitihada ya Bwana Mtume (s.a.w.) kwa kuwa upo uwezekano wa kufanya makosa na ni jambo lisilowezekana kusahihishwa kupitia ufunuo. (28)
Uchambuzi wa Sarakhsi unamaanisha matendo yote ya Bwana Mtume (s.a.w.) yanategemea na kusahihishwa na ufunuo. Tendo au neno la Bwana Mtume (s.a.w.) ima ni sahihi au si sahihi. Kama litabakia kama lilivyo, inakuwa wazi kwamba ni sahihi kwa sababu Allah hatoliacha tendo au neno lisilo sahihi kuendelea.
Shatbi anasema yafuatayo:
Hadithi ima ni ufunuo safi unaokuja kutoka kwa Allah au ni jitihada ya Bwana Mtume (s.a.w.). Hata hivyo, katika hali hiyo, jitihada yake ni ima inategemea ufunuo mzuri katika Kibatu kitukufu au sunnah au imeshakaguliwa. Hata kama mtazamo kuwa Bwana Mtume anaweza kukosea katika jitihaza yake inakubaliwa, kamwe hatoachwa kwenye makosa; litasawazishwa haraka. Mwishowe, litakuwa ni sahihi. Kwa hivyo, hakuna uwezekano wa makosa katika kitu chochote kinachokuja kutoka kwake. (29)
Kutenda kwa mujibu wa mitazamo hiyo, inaweza kusemwa kuwa wale wote wanaosema sunnah zote ni ufunuo hawakuzi-mambo kwa sababu sunnah zote zinakaguliwa na ufunuo; hizo ima zinaachwa kama zilivyo au kusahihishwa. Yaani, kwa kuwa hatuwezi kukubali uwepo wa utendaji ambao haujakaguliwa na ufunuo, tunaweza kusema kama ni hitimisho kuwa sunnah zote zinategemea ufunuo. Hata hivyo, tunaposema sunnah zote zinategemea ufunuo, tunamaanisha sunnah ambazo zimebainishwa wakati wa umri wa Mjumbe wa Allah na kwamba zimetufikia zikiwa sahihi.
4. Ufunuo uliothibitishwa Kimyakimya (taqrir)
Tunachomaanisha kuwa ni sunnah za taqrir tunapofafanua sunnah ni uthibitisho wa ukimya wa Bwana Mtume (s.a.w.) wa baadhi ya matendo au maneno aliyoyaona au kuyasikia. (30) Yaani, maswahaba walipofanya au kusema kitu kilichoegemea kwenye matendo ya Jahiliyya au maono yao wenyewe, Bwana Mtume baadhi ya wakati aliwasahihisha, na wakati mwengine aliwabadilishia na wakati mwengine hakusema kitu. Maswahaba walikizingatia kimya chake kuwa ni ruhusa kwa sababu isingefaa kwa mtume kuacha kosa kama lilivyo. Kwa hivyo, ukimya wake umemaanisha kuwa tendo hilo au neno halikuwa kosa.
Maswahaba walikuwa chini ya udhibiti wa Bwana Mtume (s.a.w.); vivyo hivyo, kwa Mjumbe wa Allah (s.a.w.) daima alikuwa chini ya udhibiti wa ufunuo kama ulivyo ulazima wa sifa ya ismah (kutokufanya makosa) (31). Kwa hivyo, inapaswa itambulike kwamba kosa lake lisingeachwa bila ya kusahihishwa (32) na kwamba lingetolewa onyo haraka, bila ya kusita (33). Bwana Mtume (s.a.w.) anatofautiana na mtu mwengine yeyote na kutokana na wale walioidhinishwa kujitahidi.
Inaeleweka kuwa alionywa kwa sababu ya baadhi ya matendo yake hata kabla hajawa mtume. (34)
Wakati mmoja, alipotaka kuvua izar yake (vazi la nje/seruni) ili arembee mawe alizuiliwa. Katika tukio jengine, alitaka kuivua izar yake ili amsaidie mjomba wake Abu Talib kwa ajili ya kukarabati Kisima cha Zamzam lakini alizimia. Alisema mtu mmoja aliyekuwa na nguo nyeupe alimwambia ajisitiri yeye mwenyewe alipokuja. (35)
Mwili wake ulihifadhiwa ili kumlinda asioneshe sehemu ambazo sio vyema kuwaonesha wengine; pia alihifadhiwa kutokana na baadhi ya matendo yasiyopendeza katika kipindi hicho. Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe, alitaka kutazama baadhi ya michezo na burudani katika maeneo ambayo sherehe za arusi zikifanyika lakini alilala na hakutazama wala kuzisikia; baadaye, hakutenda tena mambo mabaya mpaka alipochaguliwa kuwa mtume. (36)
Je inaweza kufikiriwa kuwa mtu aliyekuwa chini ya matunzo hata kabla hajawa mtume na hajachaguliwa kuwa ni mfano kwa umma wake na utu bado asingehifadhiwa katika kipindi alipokuwa mfano katika mandhari zote kwa ajili ya umma wake na utu na kuwa makosa yake yasingesahihishwa? (37)
Kwa hakika, tunaona mifano kadhaa ya katika Quran.
Bwana Mtume (s.a.w.) alikuwa na wasiwasi kuhusu matunzo ya ufunuo na Allah, Aliyetukuka, aliuondosha wasiwasi wake kwa kusema hakuna haja ya kuwa na woga kuhusu hilo. (38)
Alionywa kuhusu masuala kama vile kuwaongoa watu, watu kutii amri ya Allah, jukumu lake lilikuwa tu ni kufikisha ujumbe wa Allah ambao uongofu huo unategemea utashi wa Allah na kwamba matokeo hayo yanategemea utashi wa Allah (39); alionywa kuhusu Abu Talib, ambaye alimwombea msamaha na akakatazwa kumwombea dua mjomba wake. (40)
Kwa upande mwengine, alisitishwa kuwalaani maadui zake baada ya Vita vya Uhud (41) kutokana na utashi wake wa kutolewa viungo kutokana na yale aliyofanyiwa Bwana Hamza (Allah amridhie) (42).
Zaidi ya hayo, alionywa kuhusu kuwaachia huru wafungwa wa vita kwa kupewa fidia baada ya Vita vya Badr (43); aliepushwa kutokana na matendo aliyoyataka ili kuzichota nyoyo za wanafiki (munafiq) (44); pia alionywa alipojiharamishia yale ambayo Allah amemhalalishia kutokana na matakwa ya wafungwa wa vita. (45)
Aya hizo hapo juu na sawa na hizo ni ishara za wazi ambazo Bwana Mtume (s.a.w.) amesawazishwa wakati kile alichokifanya hakikuendana na ridhaa ya kiungu. Allah, Mtukufu, mwanzo alimwachia tu na akamtaka ajitahidi au ashauriane na maswahaba zake. Kisha, kama iliwiana na ridhaa ya Allah, basi iliachwa kama ilivyo; kama haikuwiana, alisahihishwa. Kwa hakika, ukweli kwamba mwanzo alisema watoto wa washirikina walikuwa ni kama baba zao na kisha akasema kuwa wangeweza kwenda Peponi, kwamba mwanzo alisema mijusi wamewalaani Wayahudi na kisha akaiwacha rai hiyo kwa onyo la ufunuo. Kwamba mwanzo alisema mtazamo unaohusiana na mateso ya kaburini yalikuwa ni uovu wa Wayahudi na kisha akakubali uwepo wa adhabu kaburini kutokana na onyo lililoletwa na ufunuo na kutubia kwa Allah kutokana na hilo katika dua zake, (46) akionesha kuwa alionywa na kusahihishwa nje ya ufunuo wa Quran pia.
Kama inavyoonekanwa, ni muhali kwa Mjumbe wa Allah kuendelea na amali mbovu, tendo au neno aliloliona au aliloarifiwa kwa sababu ruhusa ya ukimya wa namna hiyo inafuatwa na umma; pia ni muhali kwa Mjumbe wa Allah (s.a.w.) kuendelea kutenda maovu au maneno katika uwepo wa Allah; lolote alilofanya wakati wa maisha yake ni mfano na ni kitu cha kufuatwa na sisi.
Kisha, Allah, ambaye ni Mjuzi-wa-Kila-Kitu, Mwelewa-wa-Kila-Jambo, Msikivu-wa-Kila-Kitu, Mwenye-Kuona-Kila-Kitu na Mwingi wa Hekima, pia aliyasahihisha maneno ya namna zote, amali na matendo ya Mtume au aliyaidhinisha na kuyawacha kama yalivyokuwa. Iwe tunayaita mambo hayo ambayo Allah hakuyabadilisha na kuyaacha kuwa ni ufunuo wa siri kama wanazuoni wa madhehebu ya Hanafi wanavyoyaita (47) au ni ufunuo uliothibitishwa kimya-kimya, tunaweza kusema kuwa sunnah za Bwana Mtume (s.a.w.) zinategemea ufunuo.
Kutenda kwa mujibu wa ukweli huo, tunafikiria kuwa tunapaswa tukubali kuwa mwendelezo wa baadhi ya ada na mila za jumuia ya Mtume zimeishi wakati zimeshakaguliwa na Allah na kwa kuwa zilikuwa ni idhinisho la kimya-kimya, sio sahihi kuyazingatia hayo kuwa ni desturi tu na mila. Isitoshe, tumeeleza kuwa yameegemea kwa Bwana Ibrahim (a.s.) au mitume wengine.
Kisha, hata kama ishara na matendo ya Mtume yalikuwepo kwa muundo sawa na wa kipindi cha Jahiliyya, yangesahihishwa na ufunuo kama yangekuwa ni kosa. Inaweza kusemwa kuwa yale yote ambayo hayakusahihishwa basi yameidhinishwa.
MASIMULIZI YALIYORUHUSU HADITHI KUANDIKWA
Kuna masimulizi mengi yanayoonesha kuwa imeruhusiwa kuziandika hadithi. Moja ya masimulizi yapo kwa Abullah Ibn Amr (Allah amridhie); hadithi alizoziandika zimepelekwa kwa kizazi kilichokuja baada yake kwa namna ya vitabu. Akasema:
“Nilikuwa nikiandika chochote nilichosikia kutoka kwa Mtume ili kukihifadhi. Makuraishi walinikataza kuandika wakisema: ‘Unaandika unachokisikia kutoka kwa Mjumbe wa Allah (s.a.w.); hata hivyo, Mjumbe wa Allah ni binadamu pia. Wakati mwengine, anazungumza akiwa na hasira na wakati mwengine, anapokuwa mtulivu. Hapo, niliacha kuandika. Hata hivyo, nilimwarifu Bwana Mtume kuhusu hali hiyo. Mjumbe wa Allah akauashiria mdomo wake uliobarikiwa na akasema, ‘Andika! Naapa kwa Allah kwamba hakuna chochote zaidi ya ukweli unaotoka kinywani mwangu.” Masimulizi haya yanathibitisha kuwa Abdullah Ibn Amr (Allah amridhie) aliandika hadithi kwa mfumo wa Abu Hurayra na umesajiliwa kwa Bukhari. Abu Hurayra (Allah amridhie) anasema yafuatayo: “Hakuna anayenishinda kwa kuzijua hadithi za Bwana Mtume isipokuwa Abdullah Ibn Amr; kwa sababu alikuwa akiandika lakini mimi sikuandika.
Masimulizi yanayoelezea ruhusa kuhusu hadithi sio tu zile tulizozitaja. Ukweli kwamba Mjumbe wa Allah (s.a.w.) aliwaambia watu waliokuwa wakilalamikia hifdhi yao: “Ombeni msaada wa mikono yenu ya kulia”, ishikeni elimu kwa kuiandika”, kwamba alitoa maandishi ya hotuba zake kwa watu waliozitaka kwa maandishi, ambapo kuna kiasi cha makala 300 (ambazo ni nyaraka zilizoandikwa) ambazo zote ni hadithi na urefu wao unatofautiana kwa mistari michache kwenye kurasa chache kunathibitisha kuwa ilikuwa ni ruhsa kuandika hadithi. Hata kama ni makala tu zilizozingatiwa, itafahamika kuwa Bwana Mtume hakupinga kimfumo na kimsisitizo kuandika vitu vyengine visivyokuwa Quran na kwamba alitoa umuhimu mkubwa kwa matumizi ya uandishi katika maisha ya kiraia.
AS-SAHIFA AS-SAHIHA (KURASA NJEMA) ZA ABU HURAYRA:
Katika baadhi ya masimulizi, inaelezwa kuwa Abu Hurayra (Allah amridhie) ameandika hadithi alizozisikia kutoka kwa Mjumbe wa Allah (s.a.w.). Jina la ukurasa huo ni as-Sahifa as-Sahiha. Al-Hasan Ibn Amr Ibn Umayya ad-Damri anasimulia: “Nimeripoti hadithi karibu na Bwana Abu Hurayra (Allah amridhie). Hata hivyo, akaikanusha kwa kusema: “hakuna hadithi kama hiyo.” Nikamwambia kuwa nimeisikia kutoka kwake. Kisha, akasema, “Kama umeisikia kutoka kwangu, lazima niwe nayo kwa maandishi” na akanichukua kwa kunikamata mkono hadi nyumbani kwake. Huko, akanionesha vitabu tele ambavyo hadithi za Bwna Mtume (s.a.w.) zimeandikwa. Akaikuta hadithi ambayo nimeiripoti na akanambia: “Sikukwambia mie kuwa kama nimesimulia hadithi, itakuwa ninayo kimaandishi?”
KUKUSANYA HADITHI:
Kipindi cha pili muhimu cha historia ya hadithi kimekusanya kazi zilizoitwa “tadwin as-sunnah” (uandikaji nyaraka na usajili wa hadithi kwa maandishi”. Inaifunika karne ya pili ya Hijria.
NINI/NI NINI TADWIN?
Katika kamusi, tadwin inamaanisha kutunga na kukusanya kwenye kitabu kimoja. Kama ulivyo msamiati wa hadithi, inamaanisha kusajili rasmi hadithi kwa njia ya maandishi na kuzikusanya kwenye kitabu kimoja. Neno “rasmi” ni muhimu mno hapa. Kama inavyoonekana katika sehemu zilizopita, usajili wa hadithi umeanza wakati wa zama za Mjumbe wa Allah (s.a.w.) na mtu mmoja mmoja na binafsi. Kwa hakika, MJUMBE WA ALLAH yeye mwenyewe ameacha nyaraka nyingi za maandishi na zote ziliitwa “sunnah”. Hata hivyo, hakuna kati ya hizo zimehusishwa katika tendo la “uandishi” ikielezwa kwa neno tadwin kwa sababu kwenye tadwin, uandishi wa hadithi zote unahusika. Kisha, tunaweza kuchambua tadwin kiusahihi kama ifuatavyo: “mchakato wa uandishi wa hadithi zote uliotekelezwa katika karne ya pili ya Hijria chini ya uangalizi wa dola”.
UMEANZAJE?
Mchakato wa tadwin umeanza na Umar bin Abdulaziz, Khalifa wa kabila la Umayya. Umar bin Abdulaziz (Allah amrehemu), ambaye ni maarufu sana kwa uchamungu wake na bidii yake kwa sunnah za Mjumbe wa Allah (s.a.w.), akaanza kupatwa na wasiwasi kuhusu hadithi kama ilivyokuwa ni/katika kazazi cha maswahaba waliojua sunnah vizuri sana na wanazuoni wakubwa walivyoanza kufariki mmoja baada ya mwengine. Akafikiria kuwafanya wanazuoni waandike hadithi ili kuepusha hatari ya kupotea kwake. Kwa hivyo, yeye kwa kuwa ni Khalifa/Halifa alipeleka mashauri na notisi za ilani kwa magavana.
Maandiko ya moja ya barua ambazo Umar bin Abdulaziz aliyapeleka yamesajiliwa na Bukhari. Ni barua aliyoituma kwa gavana/kadhi wa Madina, Abu Bakr Ibn Hazm: “Tafuta, kusanya na andika masimulizi ya Bwana Mtume (s.a.w.) katika mji wako. Nachelea kuwa sayansi (hadithi) itapotea na wanazuoni watatoweka. Ukiwa unafanya hivyo, sunnah za Mjumbe wa Allah pekee (s.a.w.) ndio zitakazokubalika. Wanazuoni wanapaswa wakae katika maeneo maarufu ya wazi kwa umma kama misikitini, kueneza elimu na kuwafundisha wasiojua. Sayansi haitotoweka labda ifanywe ni siri.” Kwa mujibu wa masimulizi ambayo Ibn Sa’d ameyasajili, Umar Ibn Abdilaziz (Allah amrehemu) anayo ibara ifuatayo ya ziada katika barua aliyoiyandika/aliyoiandika kwa Ibn Hazm:
“…sunnah zilizopo zinazojulikana au masimulizi ya Amra Bintu Abdirrahman yanapaswa yakubalike…”
Ibara ya ziada ifuatayo/ibara ifuatayo ya ziada ipo katika simulizi/masimulizi ya Darimi:
“Andika masimulizi ambayo ni hakika yamekuja kutoka kwa Bwana Mtume (s.a.w.) na kutoka kwa Bwana Umar uliyo nayo (au ambayo yapo katika eneo lako)”.
Kwa mujibu wa aliyoyasajili Abu Nuaym katika Tarikh Isfahan, Umar Ibn Abdilaziz alipeleka barua kwa miji yote ya Kiisilamu.
Hivyo, kwa kuchukua masimulizi mbalimbali yaliyotaja tadwin kwa mazingatio, tunayo rai ya jumla kuhusu suala hili. Ili kulienzi jaribio hilo la Umar Ibn Abdilaziz, tunahitaji kutaja maneno yafuatayo ya Muhammed Ibnu Shihab az-Zuhri, ambaye ni mtu aliyehudumia kwa kiwango kikubwa katika mchakato wa tadwin na ambaye ndiye aliyeupa mchakato huo jina la tadwin:
“Hatuzingatii kuwa ni mwafaka kuandika elimu mpaka watawala watulazimishe kufanya hivyo. Tukianza kufanya hivyo (kama ni matokeo ya kulazimishwa na uingiliaji kati wa watawala), tumeamini kwamba hatutakiwi tumzuie Mwisilamu yeyote kuandika.”.
SABABU ZILIZOSABABISHA KUKUSANYWA KWA HADITHI
Kutakuwa na manufaa kutazama kwa karibu sababu halisi zilizosababisha hadithi kuandikwa na kukusanywa kwenye vitabu:
1- Kwa makubaliano ya pamoja ya wanazuoni, moja ya sababu hizo ni hii ifuatayo kwamba imeelezwa katika barua ya Umar Ibn Abdilaziz: Wasiwasi kwamba hadithi zitapotea kwa sababu ya vifo vya wanazuoni: Ni suala muhimu sana. Ingawa hadithi zimeandikwa na mtu mmoja mmoja, zimeandikwa ili zihifadhiwe; zikishahifadhiwa, vitachomwa moto; au itashauriwa vichomwe moto baada ya kifo cha mmoja wao. Masimulizi ya hapo juu tuliyoyanukuu kutoka kwa Zuhri yanatosha kufahamu wasiwasi na hofu kati ya wanazuoni.
Isitoshe, kipindi hicho kilikuwa ni kipindi ambapo machafuko ya kisiasa na vurugu za wenyewe kwa wenyewe zimetokea. Kifo cha Said Ibn Jubayr, mwanazuoni mashuhuri wa hadithi wa zama hizo, ambaye aliuliwa na Hajjaj az-Zalim, ilikuwa inatosha kumtia hofu Umar Ibn Abdilaziz kuwa hadithi zingeweza kupotea. Nini chengine zaidi, matukio yanofanana/yanayofanana na hilo yamesababisha kifo cha Talq Ibnu Habib; Mwanazuoni mashuhuri, Mujahid ameponea chupuchupu kufa lakini alitupwa gerezani.
2- Ingawa haikuakisi waziwazi katika barua ya Umar Ibn Abdilaziz, sababu nyengine muhimu ambayo ilianzisha tadwin ilikuwa ni ongezeko la michakato ya uchakachuaji wa hadithi kutokana na khitilafu za kisiasa na kimadhehebu. Maneno yafuatayo ya Zuhri (Allah amrehemu) yanathibitisha na kutilia mkazo hilo: “Kama isingekuwa kwa hadithi isiyojulikana kwamba imekuja kutoka mashariki na kwamba tumeikataa, nisingeandika hata hadithi moja wala nisingemruhusu yeyote kuandika hata moja.”
Suyuti anasema yafuatayo ili kueleza mchango wa mchakato wa udanganyifu wa hadithi katika tadwin: “Katika enzi ambapo wanazuoni wametawanyika na udanganyifu na uzushi (bid’a) za Khawarija na Rafidhwa umeongezeka, sunnah zikaandikwa na kukusanywa kwenye vitabu kwa kuviunganisha na maneno ya Swahaba na fatwa za Tabi’in.”
VIPI TADWIN IMETOKEA:
Masimulizi yanaonesha kuwa Umar Ibn Abdilaziz hakukuta kuwa inatosha kutuma notisi ya ilani; alifwatilia na kukagua michakato ya tadwin kwa uangalifu. Mathalani, aliwakodi makarani maalumu kufanya kazi ya tadwin katika kituo maalum; aliwateua makarani wawili kwenda kwa Hishm Ibn Abdilmalik, na Zuhri. Waliandika hadithi za Zuhri kwa mwaka mzima.
Umar Ibn Abdilaziz, Khalifa, yeye mwenyewe alishiriki katika michakato ya tadwin; alikwenda msikitini na kalamu mkononi mwake kwa ajili ya kusali na akajiunga na masomo baada ya sala, kuandika hadithi kutoka kwa Awn Ibn Abdillah na, Yazid Ibnu’r Raqqasi.
Wakati wa tadwin, sio tu masimulizi yaliyorejeshwa katika/ya zama za Mjumbe wa Allah (s.a.w.) bali pia maneno na matendo ya Maswahaba na Tabi’in yamehusishwa na baadhi ya wanazuoni wa hadithi kuwa katika nadharia ya sunnah.
Hadithi zilizoandikwa kutokana na amri ya KhalifaHalifa zilipelekwa kwenye kituo katika muundo wa vitabu; vilitolewa nakala huko na vikapelekwa kwenye miji ya Kiisilamu. Usimulizi wa uandishi wa waraka muhimu ambao umetolewa unakuja kutoka kwa Zuhri: “Umar Ibn Abdilaziz (Allah amrehemu) ametuamuru kukusanya sunnah na tumeziandika katika vitabu. Umar Ibn Abdilaziz (Allah amrehemu) alipeleka kitabu kwa kila mji alioutawala.”
Ni hakika kuwa vitabu vilivyopelekwa vilikuwa ni nakala za vitabu asilia katika kituo.
Baadhi ya masimulizi yanaeleza kuwa hadithi zilikusanywa kituoni hapo zikakaguliwa na wanazuoni: Abu’z-Zinad Abdullah Ibnu’z-Zakwan anasimulia: nimemwona Umar Ibn Abdilaziz akiwaleta pamoja wanazuoni wa fiqh. Wanazuoni wa fiqh wamekusanya kiwango kikubwa cha hadithi. Akazisoma pamoja na wanazuoni na wakati sunnah ambayo haikutekelezwa/haikuwepo imesomwa, amesema: “Hii ni ziada; hakuna haja ya kuitegemea.”
Inaweza kusemwa kuwa nakala zilizopelekwa mijini zilitolewa nakala baada ya kuchunguzwa na kamati hiyo:
Sifa muhimu za msingi za michakato ya tadwin ni kwamba hadithi hazikuandikwa chini ya vigawanyo kama vile sunan, sahih au musnad. Jambo lililokuwa muhimu katika tadwin lilikuwa ni kuziandika, kuziweka katika maandishi sio namna nyengine yoyote au lengo/au lengolingine lolote. Kwa hivyo, masimulizi marfu (yaliyorejeshwa kwa Mtume), mawqut (yaliyowekewa wakati), maqtu (yaliyokatika) yameandikwa pamoja na hasan (yaliyohakikiwa vyema) na daif (dhaifu). Tofauti yao na vigawanyo vingeshughulikiwa katika karne ijayo iliyoitwa zama za tabwib (kugawanywa katika milango).
MCHANGO WA ABU BAKR IBN HAZM:
Hatuna waraka wowote unaoonesha kwamba gavana/kadhi wa Madinah, Abu Bakr Ibn Hazm, ameandika hadithi zozote yeye mwenyewe kutokana na amri licha ya kuwa alikuwa ni mwanazuoni mkubwa wa hadithi. Labda aliona inatosha kuwalazimisha wanazuoni wafanye kazi ya tadwin kama ni gavana/akiwa kama kadhi. Kwa hakika, Zuhri, aliyeikubali kazi ya tadwin na kutoa mchango wa msingi ndani yake, ni mwanazuoni wa Madinah na kwa hakika alianza kufanya kazi kutokana na amri ya Abu Bakr Ibn Hazm.
Ingawa maisha ya Umar Ibn Abdilaziz yalikuwa sio marefu ya kutosha kuona matunda ya michakato ya tadwin, tumeripoti hapo juu kutoka kwa Zuhri kwamba vitabu vilivyokusanywa katika kipindi chake vimefikia kiwango cha kutosha cha kutolewa nakala na kupelekwa miji mikubwamikubwa. Kwa hivyo, wanazuoni wa Kiisilamu wamekubaliana kwa kauli moja kuwa tadwin ya kwanza imeanza wakati wa zama za Umar Ibn Abdilaziz (Allah amrehemu), katika miaka ya mwisho ya karne ya kwanza ya Hijria.
Profesa Dk. İbrahim Canan
Dk. Ahmet Çolak
Dk. Ahmet Çolak
Tanbihi:
1- Ingawa imesemwa kuwa kilichomaanishwa na aya: “Wala hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni ufunuo uliofunuliwa” ni Quran, wapo wanazuoni wanaosema inahusisha sunnah pia. Mathalani, Elmalılı (mwanazuoni wa kituruki wa tafsiri) anatafsiri aya hii kuwa “Hiyo, yaani, Quran au hotuba yake, si chochote/kingine isipokuwa ni ufunuo. Haiwezekani kuelezewe/kuzieleza kwa namna nyengine yoyote. Inawezekana tu kuteremshwa kuwa ni ufunuo.” Hivyo, anaashiria kuwa sunnah ni ufunuo pia. (Yazır, Hak Dini VII, 457); Cf Qurtubî, Tafsir, XVII,84-85; Aydınlı, Abdullah, Sünnetin Kaynağı Hakkında, Din Öğretimi dergisi, Issue37, Ank, 1992, uk.48; Kırbaşoğlu, Sünnet, 236 pamoja na wengine.
2- al-Baqara, 48; Aal-e-Imran, 164.
3- an-Nisa, 113; al-Jumua, 2.
4- Kwa wale wanaosema kilichokusudiwa na neno hekima ni sunnah, tazama Hasan al-Basri, Qatada, Yahya b. Kathir, (Suyuti, Miftahu’l-Janna, s.23); Imam ash-Shaii, ar Risala, 32,78,93.
5- Ukweli kwamba Quran na sunnah vyote ni ufunuo unazusha swali kuwa tofauti kati yao ni ipi? Tunafahamu kutokana na aya hiyo kuwa hakuna tofauti kati yao kwa upande wa asili. Hata hivyo, mmoja kati yao ni wahy matluw (ufunuo unaosomwa), na mwengine ni wahy ghayr matluw (ufunuo usio-somwa). Suyuti anafafanua suala hili kama ifuatavyo: Neno la Allah lina pande mbili. Allah anamwambia Jibril, “Mwambie Mtume, Allah anakuamrisha kufanya hili na lile. Jibril anafahamu utashi wa kiungu na kufikisha kwa Mtume. Inaweza kufananishwa na mfalme anampeleka mtu wa kuaminika kama ni mjumbe kwa maudhui zake na uwasilishaji wa ujumbe kwa ujumbe kupitia maneno yake mwenyewe. Nyengine ni: Allah anamwambia Jibril, “Nenda kwa Mtume na msomee kitabu hiki.” Jibril anamsomea Mtume kitabu hiko kama kilivyo, neno kwa neno. Ufunuo wa Quran unaweza kufananishwa na huo muundo wa pili na sunnah kufananishwa na muundo wa kwanza. Kwa hivyo, inasemwa kuwa inaruhusika kuripoti sunnah pamoja na maana. Suyuti, al-Itqan, I,45; tazama Subhi es-Salih, Hadis İlimleri, s.261-262; Karaman, Hadis Usulü, uk.9-10.
6- al-Anfal, 7.
7- at-Tahrim, 3.
8- Ni muhimu kwa suala letu kwamba imeelezwa mwanzoni mwa hadithi kuwa kutaibuka watu watakaosema tutakubali kile kilichomo ndani ya Quran lakini tutakataa kisichokuwemo na kuwa sunnah zimetolewa. Tazama Abu Dawud, Sunnah, 6.
9- Hadithi zote zinazoitwa qudsi (takatifu) au za kiungu zimeeleza kwa kusifiwa Allah. Ipo mitazamo fulani ambayo maneno yote mawili na maana zake ni za Allah au maana ni za Allah na maneno ni ya Mtume kama hadithi nyengine. Tazama Al-Hadith, wa’l-Muhaddithun, s.18; Qawaidu’t-Tahdith, uk.64 pamoja na wengine.
10- Tazama, Bukhari, Eeman, 37; Muslim, Eeman, 1; Abu Dawud, Sunnah, 16; Tirmidhi, Eeman,4.
11- Muslim, Jannah, 63-64; Tazama, Aydınlı, Sünnetin Kaynağı, p.50-51; Toksarı, Sünnet, uk.98-99; Abu Dawud, Adab, 48.
12- Muslim, Eeman, 32-36; See, al-Munawi, Fayzu’l-Qadir, VI, 289-290.
13- Kwa mfano/Kwa mifano, tazama, Muslim, Janaiz, 1; Tirmidhi, Eeman, 18; Jihad, 32.
14- Ingawa baadhi ya watafiti wanadai kuwa kwa kuwa hadithi ambazo neno ufunuo limetajwa zinasimuliwa kwa upande wa maana, haziwezi kukubalika kuwa ni ushahidi kwamba hadithi kwa ujumla ni ufunuo (Erul, Bünyamin, İslamiyat, C.1, s.1, uk.55 pamoja na wengine), katika makala nyengine mtu huyo huyo anasema kuwa haiwezekani kusema kuwa Allah hawasiliani na Bwana Mtume isipokuwa kwa Quran. Pia anasema Mjumbe wa Allah ameteuliwa kwa jukumu la tabligh (kufikisha ujumbe), kufundisha na kufafanua. Hata hivyo, pia anasema kuwa itakuwa vyema kuiita ni hekima. (Erul, Bünyamin, İslamiyat, V.III, uk.1., uk.184.
15- Muslim, Hayd, 34.
16- Bukhari, Nikah, 108.
17- Tazama yanayohusika, Suyuti, Miftah, 29; Musnad, II, 85,160; Bukhari, Adab, 28; Muslim, 1,140; Abu Dawud, Manasik, 24,27; Tirmidhi, Hajj, 14; Abu Dawud, Salat, 2; Bukhari, Badu’l-Khalk, 6; Abu Dawud, Sunnah, 9; Musnad, I, 191; Ibn Hisham, Sira, III, 101-102.
18- Suyuti, Miftah, 29.
19- Abdulghani Abdulkhaliq, Hujja, 337; Inasemwa kuwa ipo ijma (makubaliano ya wanazuoni) kwamba sunnah zinategemea ufunuo. Tazama, ibid, uk.338; Inaripotiwa kuwa Hasan b. Atiyya amesema sunnah inategemea ufunuo kama Quran. Darimi, Muqaddima, 49.
20- Imam Shafii, anayesema wahy matluw ni Quran na wahy ghayr matluw ni sunnah, anaeleza kuwa sunnah ni ‘hekima’ iliyotajwa katika Quran. (ar-Risala, 3-4,10; al-Umm, V, 127,128.)
21- Ibn Hazim, al-Ihkam, 93; cf. Kırbaşoğlu, Sünnet, uk.260-261.
22- Ghazali, Mustasfa, I, 83; kwamba Kattabi ana maoni hay ohayo/hayo hayo, tazama Khattabi, Maalimu’s-Sunan, V, 10.
23- Çakan, İ.Lütfi, Hadislerde Görülen İhtilaflar ve Çözüm Yolları, Ist, 1982, uk.96.
24- Hadithi inayoeleza mwanamke na mama yake mdogo au shangazi yake hawezi kuolewa na mwanamme huyo huyo kwa wakati mmoja ni kama hiyo/hivyo. Bukhari, Nikah, 27; Muslim, Nikah, 37-38.
25- Anaeleza tukio lifuatalo kuwa ni mfano: kuvaa nguo za hariri ni haramu kwa wanaume lakini Bwana Mtume alimwachia Abdurrahman b. Awf avae nguo za hariri kutokana na ugonjwa wake. Tazama, Bukhari, Jihad, 91; Libas, 29; Muslim, Libas, 24-26.
26- Ibn Qutayba, Abu Muh. Abdullah, Ta’wilu Mukhtalifi’l-Hadith, Beirut, 1972, uk.196 pamoja na wengine.
27- ibara/Ibara kama roho mtakatifu/roho takatifu imepulizwa kifuani mwangu ni ufunuo wa aina hiyo. Ibn Majah, Tijarah, 2; Bayhaqi, Sunan, VII, 76; Suyuti, Miftah, 30.
28- Sarakhsi, Shamsuddin, Usulu’s-Sarakhsi, Beirut, 1973, II, 90-96.
29- Shatibi, Muwafaqat, IV, 19; Kwa ajili ya Mitazamo hiyo hiyo, tazama, Abdulghani, Hujja, uk.334 pamoja na wengine.
30- Tazama, Aydınlı, Istılah, 148; Pia Tazama, Bukhari, I’tisam, 24.
31- Ismah, moja ya sifa za mitume, inamaanisha kuwa mbali na ukafiri, kutokumjua Allah, kusema uongo, kufanya makosa, uovu, kutelekeza, kutokujua undani wa Shariah. Pia inamaanisha kwa kutowezekana/kushindikana kuendelea kufanya makosa. Tazama, Ghazali, Mustasfa, II, 212-214; Sabuni, Maturidiyye Akâidi, trns Bekir Topaloğlu, Ank. 1979, s.212-212; Yazır, Hak Dini, IX, 6357; Abdulghani, Hujja, 108 pamoja na wengine/pamoja na wengine.
32- Sarakhsi, Usul, II, 68.
33- Sabuni, Maturidiyya, 121; Abdulghani, Hujja, uk.222; Kwa mtazamo wa Ibn Taymiyya kwamba mitume hawatoachwa waendele kufanya makosa, tazama Abduljalil Eesa, Ijtihadu’r-Rasul, Misri, nd. uk.33.
34- Kwamba Allah alimhifadhi (s.a.w.) kutokana na uchafu wa Jahiliyya, tazama Ibn Sa’d, Tabaqat, I, 121; Abu Nuaym, Dalail, I, 129; Bayhaqi, Dalaîl, I, 313.
35- Abu Nuaym, Dalail, I, 147; Pia tazama, Bukhari, I, 96; Muslim, I, 268; Bayhaqi, Dalail, I, 313-314.
36- Tazama. Tabari, Tarikh, II, 196; Abu Nuaym, Dklail, I, 143; Bayhaqi, Dalail, I, 315; Mara, wakamchukua (s.a.w.) kwa nguvu kwenda kwenye burudani, lakini akatoweka; Kisha, akasema; mtu mwenye-ngozi-nyeupe, mrefu amenambia/aliniambia; ‘Ewe Muhammad! Usiliguse sanamu hilo. Rudi!’” Cf Musnad, II, 68-69; Köksal, İslam Tarihi, II,117-121.
37- Kwa maelezo zaidi, tazama Sarakhsi, Usul, II, 91; Ghazali, Mustasfa, II,214; Sabuni, Maturidiyya, s.121; Abdülghani, Hujja, 221-222; Abduljalil Eesa, İjtihad, uk.31-33; Çakan, İhtilaflar, uk.96,113; Erdoğan, Sünnet, 192 pamoja na wengine/pamoja na wengine.
38- Qiyamah, 16-17.
39- Tazama yanayohusika al-Ghashiya, 21-22; Hud, 12; al-Kahf, 23; al,-Qasas, 56; Yunus, 99; ash-Shuara, 3.
40- at-Tawba, 113.
41- Tirmidhi, Tafsir, sura 3/12; Aal-e-Imran, 128; Abduljalil Eesa, Ijtihad, uk.95.
42- Viungo vya Bwana Hamza kama sikio lake na pua vimekatwa na ini lake limenyofolewa. Ibn Hisham, Sira, III, 101-103. Kwa ajili ya aya tazama an-Nahl, 126-127.
43- al-Anfal, 67-68. Tazama Abdülghani, Hujja, 185.
44- at-Tawba, 88, 84; Tazama Ibn Kathir, Tafsir, II, 378; Abduljalil Eesa, uk.105.
45- at-Tahrim, 1-2.
46- Tazama Abduljalil Eesa, Ijtihad, s.59-66.
47- Tazama, Sarakhsi, II, 90-91; Tahanawi, Muh. Ali b. Ali, Kashshafu Istilahati’l-Funun, Ist, 1984, II, 1523.
2- al-Baqara, 48; Aal-e-Imran, 164.
3- an-Nisa, 113; al-Jumua, 2.
4- Kwa wale wanaosema kilichokusudiwa na neno hekima ni sunnah, tazama Hasan al-Basri, Qatada, Yahya b. Kathir, (Suyuti, Miftahu’l-Janna, s.23); Imam ash-Shaii, ar Risala, 32,78,93.
5- Ukweli kwamba Quran na sunnah vyote ni ufunuo unazusha swali kuwa tofauti kati yao ni ipi? Tunafahamu kutokana na aya hiyo kuwa hakuna tofauti kati yao kwa upande wa asili. Hata hivyo, mmoja kati yao ni wahy matluw (ufunuo unaosomwa), na mwengine ni wahy ghayr matluw (ufunuo usio-somwa). Suyuti anafafanua suala hili kama ifuatavyo: Neno la Allah lina pande mbili. Allah anamwambia Jibril, “Mwambie Mtume, Allah anakuamrisha kufanya hili na lile. Jibril anafahamu utashi wa kiungu na kufikisha kwa Mtume. Inaweza kufananishwa na mfalme anampeleka mtu wa kuaminika kama ni mjumbe kwa maudhui zake na uwasilishaji wa ujumbe kwa ujumbe kupitia maneno yake mwenyewe. Nyengine ni: Allah anamwambia Jibril, “Nenda kwa Mtume na msomee kitabu hiki.” Jibril anamsomea Mtume kitabu hiko kama kilivyo, neno kwa neno. Ufunuo wa Quran unaweza kufananishwa na huo muundo wa pili na sunnah kufananishwa na muundo wa kwanza. Kwa hivyo, inasemwa kuwa inaruhusika kuripoti sunnah pamoja na maana. Suyuti, al-Itqan, I,45; tazama Subhi es-Salih, Hadis İlimleri, s.261-262; Karaman, Hadis Usulü, uk.9-10.
6- al-Anfal, 7.
7- at-Tahrim, 3.
8- Ni muhimu kwa suala letu kwamba imeelezwa mwanzoni mwa hadithi kuwa kutaibuka watu watakaosema tutakubali kile kilichomo ndani ya Quran lakini tutakataa kisichokuwemo na kuwa sunnah zimetolewa. Tazama Abu Dawud, Sunnah, 6.
9- Hadithi zote zinazoitwa qudsi (takatifu) au za kiungu zimeeleza kwa kusifiwa Allah. Ipo mitazamo fulani ambayo maneno yote mawili na maana zake ni za Allah au maana ni za Allah na maneno ni ya Mtume kama hadithi nyengine. Tazama Al-Hadith, wa’l-Muhaddithun, s.18; Qawaidu’t-Tahdith, uk.64 pamoja na wengine.
10- Tazama, Bukhari, Eeman, 37; Muslim, Eeman, 1; Abu Dawud, Sunnah, 16; Tirmidhi, Eeman,4.
11- Muslim, Jannah, 63-64; Tazama, Aydınlı, Sünnetin Kaynağı, p.50-51; Toksarı, Sünnet, uk.98-99; Abu Dawud, Adab, 48.
12- Muslim, Eeman, 32-36; See, al-Munawi, Fayzu’l-Qadir, VI, 289-290.
13- Kwa mfano/Kwa mifano, tazama, Muslim, Janaiz, 1; Tirmidhi, Eeman, 18; Jihad, 32.
14- Ingawa baadhi ya watafiti wanadai kuwa kwa kuwa hadithi ambazo neno ufunuo limetajwa zinasimuliwa kwa upande wa maana, haziwezi kukubalika kuwa ni ushahidi kwamba hadithi kwa ujumla ni ufunuo (Erul, Bünyamin, İslamiyat, C.1, s.1, uk.55 pamoja na wengine), katika makala nyengine mtu huyo huyo anasema kuwa haiwezekani kusema kuwa Allah hawasiliani na Bwana Mtume isipokuwa kwa Quran. Pia anasema Mjumbe wa Allah ameteuliwa kwa jukumu la tabligh (kufikisha ujumbe), kufundisha na kufafanua. Hata hivyo, pia anasema kuwa itakuwa vyema kuiita ni hekima. (Erul, Bünyamin, İslamiyat, V.III, uk.1., uk.184.
15- Muslim, Hayd, 34.
16- Bukhari, Nikah, 108.
17- Tazama yanayohusika, Suyuti, Miftah, 29; Musnad, II, 85,160; Bukhari, Adab, 28; Muslim, 1,140; Abu Dawud, Manasik, 24,27; Tirmidhi, Hajj, 14; Abu Dawud, Salat, 2; Bukhari, Badu’l-Khalk, 6; Abu Dawud, Sunnah, 9; Musnad, I, 191; Ibn Hisham, Sira, III, 101-102.
18- Suyuti, Miftah, 29.
19- Abdulghani Abdulkhaliq, Hujja, 337; Inasemwa kuwa ipo ijma (makubaliano ya wanazuoni) kwamba sunnah zinategemea ufunuo. Tazama, ibid, uk.338; Inaripotiwa kuwa Hasan b. Atiyya amesema sunnah inategemea ufunuo kama Quran. Darimi, Muqaddima, 49.
20- Imam Shafii, anayesema wahy matluw ni Quran na wahy ghayr matluw ni sunnah, anaeleza kuwa sunnah ni ‘hekima’ iliyotajwa katika Quran. (ar-Risala, 3-4,10; al-Umm, V, 127,128.)
21- Ibn Hazim, al-Ihkam, 93; cf. Kırbaşoğlu, Sünnet, uk.260-261.
22- Ghazali, Mustasfa, I, 83; kwamba Kattabi ana maoni hay ohayo/hayo hayo, tazama Khattabi, Maalimu’s-Sunan, V, 10.
23- Çakan, İ.Lütfi, Hadislerde Görülen İhtilaflar ve Çözüm Yolları, Ist, 1982, uk.96.
24- Hadithi inayoeleza mwanamke na mama yake mdogo au shangazi yake hawezi kuolewa na mwanamme huyo huyo kwa wakati mmoja ni kama hiyo/hivyo. Bukhari, Nikah, 27; Muslim, Nikah, 37-38.
25- Anaeleza tukio lifuatalo kuwa ni mfano: kuvaa nguo za hariri ni haramu kwa wanaume lakini Bwana Mtume alimwachia Abdurrahman b. Awf avae nguo za hariri kutokana na ugonjwa wake. Tazama, Bukhari, Jihad, 91; Libas, 29; Muslim, Libas, 24-26.
26- Ibn Qutayba, Abu Muh. Abdullah, Ta’wilu Mukhtalifi’l-Hadith, Beirut, 1972, uk.196 pamoja na wengine.
27- ibara/Ibara kama roho mtakatifu/roho takatifu imepulizwa kifuani mwangu ni ufunuo wa aina hiyo. Ibn Majah, Tijarah, 2; Bayhaqi, Sunan, VII, 76; Suyuti, Miftah, 30.
28- Sarakhsi, Shamsuddin, Usulu’s-Sarakhsi, Beirut, 1973, II, 90-96.
29- Shatibi, Muwafaqat, IV, 19; Kwa ajili ya Mitazamo hiyo hiyo, tazama, Abdulghani, Hujja, uk.334 pamoja na wengine.
30- Tazama, Aydınlı, Istılah, 148; Pia Tazama, Bukhari, I’tisam, 24.
31- Ismah, moja ya sifa za mitume, inamaanisha kuwa mbali na ukafiri, kutokumjua Allah, kusema uongo, kufanya makosa, uovu, kutelekeza, kutokujua undani wa Shariah. Pia inamaanisha kwa kutowezekana/kushindikana kuendelea kufanya makosa. Tazama, Ghazali, Mustasfa, II, 212-214; Sabuni, Maturidiyye Akâidi, trns Bekir Topaloğlu, Ank. 1979, s.212-212; Yazır, Hak Dini, IX, 6357; Abdulghani, Hujja, 108 pamoja na wengine/pamoja na wengine.
32- Sarakhsi, Usul, II, 68.
33- Sabuni, Maturidiyya, 121; Abdulghani, Hujja, uk.222; Kwa mtazamo wa Ibn Taymiyya kwamba mitume hawatoachwa waendele kufanya makosa, tazama Abduljalil Eesa, Ijtihadu’r-Rasul, Misri, nd. uk.33.
34- Kwamba Allah alimhifadhi (s.a.w.) kutokana na uchafu wa Jahiliyya, tazama Ibn Sa’d, Tabaqat, I, 121; Abu Nuaym, Dalail, I, 129; Bayhaqi, Dalaîl, I, 313.
35- Abu Nuaym, Dalail, I, 147; Pia tazama, Bukhari, I, 96; Muslim, I, 268; Bayhaqi, Dalail, I, 313-314.
36- Tazama. Tabari, Tarikh, II, 196; Abu Nuaym, Dklail, I, 143; Bayhaqi, Dalail, I, 315; Mara, wakamchukua (s.a.w.) kwa nguvu kwenda kwenye burudani, lakini akatoweka; Kisha, akasema; mtu mwenye-ngozi-nyeupe, mrefu amenambia/aliniambia; ‘Ewe Muhammad! Usiliguse sanamu hilo. Rudi!’” Cf Musnad, II, 68-69; Köksal, İslam Tarihi, II,117-121.
37- Kwa maelezo zaidi, tazama Sarakhsi, Usul, II, 91; Ghazali, Mustasfa, II,214; Sabuni, Maturidiyya, s.121; Abdülghani, Hujja, 221-222; Abduljalil Eesa, İjtihad, uk.31-33; Çakan, İhtilaflar, uk.96,113; Erdoğan, Sünnet, 192 pamoja na wengine/pamoja na wengine.
38- Qiyamah, 16-17.
39- Tazama yanayohusika al-Ghashiya, 21-22; Hud, 12; al-Kahf, 23; al,-Qasas, 56; Yunus, 99; ash-Shuara, 3.
40- at-Tawba, 113.
41- Tirmidhi, Tafsir, sura 3/12; Aal-e-Imran, 128; Abduljalil Eesa, Ijtihad, uk.95.
42- Viungo vya Bwana Hamza kama sikio lake na pua vimekatwa na ini lake limenyofolewa. Ibn Hisham, Sira, III, 101-103. Kwa ajili ya aya tazama an-Nahl, 126-127.
43- al-Anfal, 67-68. Tazama Abdülghani, Hujja, 185.
44- at-Tawba, 88, 84; Tazama Ibn Kathir, Tafsir, II, 378; Abduljalil Eesa, uk.105.
45- at-Tahrim, 1-2.
46- Tazama Abduljalil Eesa, Ijtihad, s.59-66.
47- Tazama, Sarakhsi, II, 90-91; Tahanawi, Muh. Ali b. Ali, Kashshafu Istilahati’l-Funun, Ist, 1984, II, 1523.

Comments
Post a Comment