Inadaiwa kuwa hakuna aya inayohusu tasattur (stara) katika Quran. Je unajibu vipi madai hayo?
Dear Brother / Sister,
Katika Enzi za Jahiliyya, watu wengi hawakuwa na maadili mema na staha. Maadili, Usafi wa tabia na utukufu yalikuwa ni mambo yaliyozungumzwa lakini hayakufanywa. Wanawake walikuwa wakivaa bila ya staha kama ilivyo leo na walikuwa wakijifaharisha kwa kuonesha sehemu zao za siri. Dini ya Uislamu, ambayo imetumwa kama rehema ya kiungu, iliweka baadhi ya amri na kanuni ili kuwarekebisha watu waliokuwa katika ufisadi. Amri mojawapo kati ya hizo ni kuhusu wanawake kujisitiri kwa ma-jilbab:
“Ewe Nabii! Waambie wake zako, na binti zako, na wake za Waumini wajiteremshie nguo zao.“ (al-Ahzab: 59)
Kuna mitazamo michache kuhusu jilbab ni nini:
1- Jilbab ni kanzu ndefu au joho lenye kupwaya linalositiri mwili wote.
2- Ni nguo ya kupwaya inayovaliwa juu ya joho.
3- Ni kitambaa cha kufunika kichwa, shingo na mabega.
4- Ni vazi linalositiri sehemu ya juu ya mwili na kushuka chini mpaka tumboni.
2- Ni nguo ya kupwaya inayovaliwa juu ya joho.
3- Ni kitambaa cha kufunika kichwa, shingo na mabega.
4- Ni vazi linalositiri sehemu ya juu ya mwili na kushuka chini mpaka tumboni.
Khalil, ambaye ni mwalimu wa Sibawayhi anasema, “Maana mojawapo katika hizo inaruhusiwa.” (as-Siraj al-Munir Juz. 3. uk. 271) Mwanamke muislamu anatakiwa ajisitiri mwili wake wote isipokuwa mikono yake na uso. Ikiwa mtu anaamini hayo lakini hayatendi, anakuwa mwenye kufanya dhambi. Hata hivyo, ikiwa mtu atayakanusha hayo, anatazamwa kuwa ameritadi. Ni upotovu kukimbilia tafsiri ambazo Uislamu hauzipokei ili kuharibu imani ya watu.
Maswali juuyau islamu
Comments
Post a Comment