Hadithi ni nini? Je utafafanua tofauti kati ya aya (ayah) na hadithi?

Aya maana yake ni sentensi ambayo mwanzo wake na mwisho uko wazi katika Quran. Kila aya ya Quran ni muujiza. Kila aya ni ushahidi kwa ajili ya uaminifu wa mtume aliyefikisha aya hiyo na somo la kupigiwa mfano kwa ajili ya wenye kufikiri, kutafakari na kuzingatia; kila aya ni ‘kitu cha ajabu’ kwa sababu ni muujiza na ina thamani.
Hadithi ni maneno, amali, idhinisho na sunnah za Mtume zinazojumuisha maadili yake na ubora wa kiutu ulioelezwa kwa maneno au maandishi. Kwa namna hii, hadithi ni kisawe cha sunnah.
Neno hadithi limeanza kutumiwa kuwa ni jina la jumla kwa ajili ya habari zilizoripotiwa kutoka kwa Mtume kwa mujibu wa muda.
Mjumbe wa Allah (s.a.w.) sio tu aliwapelekea watu ufunuo alioupokea kutoka kwa Allah bali pia aliwafafanulia ufunuo huo na kuutekeleza katika maisha yake yeye mwenyewe, kuwa ni mfano madhubuti kwao. Kwa hivyo, pia alikuwa akiitwa Quran hai.
Wanazuoni wa Kiisilamu kwa ujumla wanazizingatia hadithi zinazohusiana na masuala ya kidini kuwa zimefunuliwa na Allah kwa mtume na kuonesha aya ifuatayo kuwa ni ushahidi wa hilo:
“Wala hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa; “(an-Najm, 53/3-4).
Kwa kuongezea, wanasema neno hikmah (hekima) lililotajwa katika aya ifuatayo linamaanisha sunnah:
“Hakika Mwenyezi Mungu amewafanyia wema mkubwa Waumini vile alivyo waletea Mtume aliye miongoni mwao wenyewe, anaye wasomea Aya zake, na anawatakasa, na anawafunza Kitabu na hikima, ijapo kuwa kabla ya hapo walikuwa katika upotovu ulio wazi.” (Aal-i lmran, 3/164)
Kwa hakika, baadhi ya masimulizi yaliyoripotiwa kutoka kwa Mtume na Maswahaba zake yameutanguliza ukweli huu. Yafuatayo yanaripotiwa kutoka kwa Mjumbe wa Allah:
“Nimepewa Kitabu kitukufu na mfano wake (sunnah)” (Abu Dawud, Sunan, II, 505).
Hassan Ibn Atiyya amefafanua yafuatayo kuhusiana na suala hili: “Jibril (Jibrilu) ameleta na kufundisha sunnah kwa Mjumbe wa Allah kama vile alivyoileta na kuifundisha Quran.” (Ibn Abdilbarr, Jamiu'l Bayani'l-ilm, II, 191).
Kama inavyofahamika kutoka kwenye aya na taarifa za hapo juu, Quran na hadithi (au sunnah kwa ufahamu mpana zaidi) ni sawasawa kwa upande wa kuwa ni ufunuo ulioteremshwa kwa Mjumbe wa Allah (s.a.w.) na Allah. Hata hivyo, Quran inatofautiana na hadithi kwa sababu ni jambo lisilowezekana kutoa kitu kama Quran kwa upande wa maana na maneno, inathibitishwa kwa maandishi katika ubao uliohifadhiwa (Lawh al-MafuzMahfudh), na sio Jibril wala Mtume (s.a.w.) anayeweza kubadilisha kitu ndani yake. Hadithi hazikuwa ufunuo kama maneno; na sio miujiza kama maneno ya Quran; inaruhusiwa kuiripoti kwa maana yake tu maadamu maana haibadiliki.
Kama ilivyo fiqh ni chanzo kinachotegemea ufunuo, hali ya hadithi kwa kulinganisha na Quran na kwa upande wa hukumu inayoileta ni kama ifuatavyo:
1. Baadhi ya hadithi zinathibitisha na kusisitiza hukumu ambazo Quran imezileta; kwa mfano, hadithi zinazokataza kuwaasi wazazi wawili, kubeba ushahidi wa uongo na kufanya mauaji.
2. Baadhi ya hadithi zinafafanua na kuzijalizia hukumu ambazo zimeletwa na Quran. Kusimamisha sala, kutekeleza hajj na kutoa zakah yote yameamrishwa katika Quran lakini haikuelezewa namna ya kutekelezwa. Tunajifunza namna gani ya kuyatimiza hayo kutoka katika hadithi.
3. Baadhi ya hadithi zimetoa hukumu kuhusu masuala ambayo Quran haikuyataja kabisa. Hadithi zilizokataza kula nyama ya punda na ndege wanaowinda na hadithi zinazothibitisha hukumu mbalimbali kuhusu diyah, n.k. ni mifano ya hadithi inayoonesha kuwa hadithi zinaweza kuwa ni chanzo cha sheria za kutegemewa.
Tulichokieleza hadi sasa kinaonesha nafasi ya hadithi (sunnah) katika dini ya Uisilamu. Ukweli kuwa ni lazima kuzipa umuhimu hadithi kama ni chanzo kinachokuja mara tu baada ya Quran kutoka katika nukta ya mtazamo wa dini ya Uisilamu na kutenda kwa mujibu wa sunnah za Mtume kumeamrishwa kwa hotuba za dhahiri na wote wawili Allah na mjumbe Wake Bwana Muhammad (s.a.w.). Aya zifuatazo zinazohusiana na suala hilo zimo ndani ya Quran.
“Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu.” (Aal-i Imran, 3/31);
“Sema: Mt’iini Mwenyezi Mungu na Mtume. Na wakigeuka basi Mwenyezi Mungu hawapendi makafiri.” (Aal-i Imran, 3/32);
“Na mt’iini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemewa. (Aal-i Imran, 3/132);
“Na anacho kupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho. (al-Hashr, 59/7).
Kama inavyoonekana, katika aya kama hizo hapo juu, kumtii Mjumbe wa Allah (s.a.w.) kumeamrishwa pamoja na kumtii Allah; hata pia imeelezwa wazi kuwa kumtii Mtume (s.a.w.) kunamaanisha ni kumtii Allah.
Katika hadithi fulani, Mjumbe wa Allah (s.a.w.) amesema, “Jueni ya kwamba nimepewa Quran na mfano wake (sunnah). Utafika wakati mtu ameshiba juu ya kochi lake atasema: Ihifadhini Quran; mkikuta jambo la halali ndani yake lihalalisheni, na mkikuta linalokatazwa likatazeni. Bila ya shaka yoyote, lile ambalo Mjumbe wa Allah ameliharamisha ni kama vile Allah ameliharamisha.” (Abu Daawd Sunnah, 5; Ibn Majah, Muqaddima, 2; Ahmad b. Hanbal, Musnad, IV,131), akiwaonya Waisilamu dhidi ya wale wote wanaodharau sunnah na wanaotaka kuitenganisha kutokana na dini na kutilia mkazo kuwa dini haiwezi kuzingatiwa bila ya sunnah.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU