Daktari Ashangazwa na Wanao HOJI Afya ya Rais Magufuli Mitandaoni..Wachukuliwe Hatua

DAKTARI wa binadamu katika Hospitali ya Lugalo, Dar es Salaam, Walter Nnko, amejitokeza na kueleza kushangazwa na hatua ya baadhi ya watu kuanza kutoa taarifa za kutetereka kwa afya ya Rais Dk. John Magufuli, akisema hatua hiyo inakiuka misingi ya utu, taaluma na hata sheria za nchi.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Dk. Nnko alisema kutokana na namna ambavyo taarifa hizo zimekuwa zikisambaa, ni vyema wahusika ambao wanafahamika wachukuliwe hatua na vyombo vinavyohusika.

Alisema ni wazi kuwa kwa binadamu yeyote, kuugua ni suala la kawaida na yeyote ana haki ya kufanya ugonjwa wake kuwa siri, lakini ubaya unakuja pale watu wengine wanapoamua kwa sababu zao binafsi kuzusha ugonjwa na kusambaza taarifa mbaya kwa nia ya kuvuruga hali ya usalama wa nchi.

“Katika utaratibu wa kawaida, ni suala la uamuzi wa mtu binafsi kutangaza ugonjwa wake. Wakati mwingine mtu anaweza kuumwa hata asimwambie mwenza wake, akafanya matibabu akamaliza.

“Inapotokea kundi la watu wachache wakaanza kusambaza uvumi kuhusu kutetereka afya ya mtu au hata kifo, ni suala baya lisilokuwa na nia njema. Hasa uvumi huo unapomhusu kiongozi mkubwa wa kitaifa, ambaye kila siku tunamwombea awe mzima, mwenye afya tele ili atekeleze majukumu yake,” alisema.

Alisema yeye akiwa daktari, anatambua kuwa haki ya usiri wa mgonjwa ni suala la kimaadili, kwa hiyo anaona kuna hatari zaidi, hasa pale wanapojitokeza watu na kusambaza uzushi huku wakijua kabisa kuwa kwa kufanya hivyo wanalikosea taifa.

Dk. Nnko alisema anaamini Tanzania ni nchi yenye amani na isiyo na ubaguzi wa ukabila, kwamba mtu anaweza kufanya kazi popote na yeyote, hivyo uvumi wa ugonjwa, tatizo la kiafya au kifo kwa mtu mwingine ni suala linalochochea chuki.

Alisema kutokana na dhana hiyo, ni vyema Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) na mamlaka zote zinazohusika ziwashughulikie wahusika na kuhakikisha kuwa suala kama hilo halijirudii kwa kuwa ni aibu kwa taifa, hasa ikizigatiwa watu wanaofanya hivyo ni watu wenye elimu na dhamana.

Dk. Nnko alisema anaamini watu wenye elimu ndio wenye uwezo wa kupima jambo na wakati mwingine wana utambuzi wa kujua mema na mabaya, hivyo kuwa na ufahamu unaowasukuma kufikiri kabla ya kutenda.

“Kwa akili ndogo tu, kwa mtu muungwana hutakiwi kumwombea jirani yako mabaya, na ukiona mtu anafanya hivyo basi ujue akili yake siyo nzuri, ukiona mtu anafurahia mtu mwingine apate matatizo, si jambo jema,” alisema.

Alieleza kuwa ni wazi asilimia 80 ya Watanznaia wametokea katika familia masikini, hivyo miongoni mwao hakuna anayeweza kufurahia kuona Rais ambaye amejipambanua kutetea rasilimali za taifa kusaidia wanyonge kwa nguvu zake zote anafanyiwa dhihaka.

“Inatakiwa tumwombee Rais kila siku, aendelee kuwa na afya njema, aendelee kwa nguvu ile ile kutetea haki za wanyonge. Hakuna binadamu mwenye haki ya kumtangazia mwenzake jambo baya, hata daktari haruhusiwi kutoa taarifa mbaya au kutangaza ugonjwa wa mtu,” alisema Dk. Nnko.

Alisema kwa sasa wakati wengine wakiendelea kujenga chuki kwa Rais Magufuli na Serikali yake, ndio wakati sahihi wa Rais kuendelea kujenga nchi kwa kuwa hata kama angekuwa malaika, watu hawawezi kuacha kumsema kwa mabaya.

“Tumejifunza mengi sana kupitia kwake, kwa jinsi ambavyo amekuwa na utendaji kazi wa kipekee na bado anapigwa vita. Rais endelea kuchapa kazi. Taifa linakutegemea katika kuchochea maendeleo,” alisema Dk. Nnko

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU