Aya 19 -25: Na Ardhi Tumeitandaza

Na ardhi tumeitandaza na tumeweka humo milima na tumeotesha kila kitu kwa wizani.
Umetangulia ufafanuzi wake katika Juz. 13 (13:3).
Kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Kila kitu kwa wizani’ ina maana moja na kauli yake:
وَكُلُّ شَيْءٍ عِنْدَهُ بِمِقْدَارٍ {8}
“Na kila kitu kwake, ni kwa kipimo” Juz.13 (13:8),
Pia kauli yake:
وَخَلَقَ كُلَّ شَيْءٍ فَقَدَّرَهُ تَقْدِيرًا {2}
“Na akaumba kila kitu na akakikadiria kipimo” (25:2).
Yaani anachunga kiwango, aina, sura na lengo la kupatikana kitu hicho. Kama ingelikuwa ni sadfa basi kusingelikuwa na mpangilio huu.
Na tumejaalia humo maisha.
Yaani humo ardhini. Maana ya maisha ni zile sababu za maisha; kama vile kilimo, biashara na viwanda. Lakini maisha ya unyonyaji na uporaji hivyo ni viwanda vya shetani, sivyo alivyovijaalia Mwenyezi Mungu.
Na ya ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
Kila kiumbe hai ardhini sisi hatukiruzuku wala hatukalifiwi na riziki yake, hilo liko wazi; isipokuwa lengo la ishara hii ni kuwa sisi tujue kuwa viumbe vyote hai vinaishi kwa riziki ya Mwenyezi Mungu, hakuna aliye hai anayeweza kumruzuku aliye hai; hata watoto tuwaleao na wanyama tuwafugao, riziki zao zote zinaatoka kwa Mungu, si kwa mwengine.
Na hakuna chochote ila hazina yake iko kwetu na wala hatukiteremshi isipokuwa kwa kipimo maalum.
Razi anasema: “Wameafikiana wafasiri kuwa makusudio ya chochote ni mvua, kwa vile hiyo ndiyo sababu ya riziki na maisha.” Lakini ukweli ni kuwa makusudio ya chochote ni mvua na mengineo. Kwa sababu neno chochote linaenea kwenye kila kitu; kama kusema sikumuona yeyote. Makusudo ya kuteremsha ni kutoa. Kiwango maalum ni sababu ya riziki. Maana ni kuwa heri yote iko kwa Mungu, Yeye ndiye anayewapa wenye kujitahidi, sio wavivu na wazembe. Mwenyezi Mungu ansema:
هُوَ الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ ذَلُولًا فَامْشُوا فِي مَنَاكِبِهَا وَكُلُوا مِنْ رِزْقِهِ ۖ {15}
 Yeye ndiye aliyewafanyia ardhi iwe laini basi nendeni katika pande zake na kuleni katika riziki zake” (67:15).
Kwa maelezo zaidi angalia kifungu ‘Je riziki ni bahati au majaaliwa?’ Juz.7 ( 5:100).
Na tukazipeleka pepo za kupandishia na tukateremsha kutoka mbinguni maji tukawanywesha hayo wala nyinyi sio mnaoyaweka akiba.
Pepo zimesifiwa kuwa za kupandishia mbegu kwa vile zinaabeba mawingu ya mvua na kufanya miti iwe inamea kutokana na mvua. Kwenye hali hii Mwenyezi Mungu ameishria mahali pengine kwa kusema: “Na yeye ndiye azipelekaye pepo kuwa ni bishara kabla ya kufika rehema yake. Hata zinapobeba mawingu mazito tunayasukuma kwa ajili ya mji uliokufa.” Juz. 8 (7:57).
Vilevile zimesifiwa kuwa ni za kupandishia kwa vile zinahamisha mbegu za maua ya kiume na kuzipeleka kwenye maua ya kike ili yaweze kutoa mazao na matunda.
Makusdio ya kusema: ‘wala nyinyi sio mnaoyaweka akiba’, sio kuwa maji yote yako kwenye tangi kubwa lililoko kwa Mwenyezi Mungu, hapana; isipokuwa makusudio ni kuwa Mwenyezi Mungu anayateremsha maji kwa sababu zake za kimaumbile, kuayahifadhi ardhini na kuyatoa kidogo kidogo, kupitia mito, kulingana na mahitaji.
Na hakika sisi ndio tunaohuyisha na tunaofisha. Na sisi ndio warithi.
Sisi ndio warithi ni fumbo la kuwa kila aliyeko ataondoka, hatabaki yoyote isipokuwa dhati ya Mola mwenye utukufu na kutukuka.
Na hakika tunawajua watanguliao katika nyinyi na hakika tunawajua wachelewao.
Razi na Tabrasi wametaja njia sita katika maana ya watanguliao na wachelewao. Usahihi ni kuwa makusudio ni kwamba hakifichiki kitu chochote mbele ya Mwenyezi Mungu katika hali ya waliotangulia na watakaokuja nyuma.
Na hakika Mola wako ndiye atakayewakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mjuzi.
Atawakusanya wote siku ya hisabu na malipo na ni Mwenye hekima katika kuwakusanya kwao huko, ambapo mtenda mema atapata thawabu za mema yake na mtenda maovu atapata adhabu ya movu yake. Vilievile Yeye anamjua aliyefanya mema na aliyefanya maovu.
وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنْسَانَ مِنْ صَلْصَالٍ مِنْ حَمَإٍ مَسْنُونٍ {26}
Na hakika tulimuumba mtu kutokanudongmkavu kwmatopmeusyenye kufinyangwa.
وَالْجَانَّ خَلَقْنَاهُ مِنْ قَبْلُ مِنْ نَارِ السَّمُومِ {27}
Na majini tumewaumba kwa moto wenye joto kali.
وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي خَالِقٌ بَشَرًا مِنْ صَلْصَالٍ مِنْ حَمَإٍ مَسْنُونٍ {28}
Na Mola wako alipowaambia Malaika: “Hakika mimi nitamuumba mtu kutokana na udongo mkavu kwa matope meusi yenye kufinyangwa.
فَإِذَا سَوَّيْتُهُ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِنْ رُوحِي فَقَعُوا لَهُ سَاجِدِينَ {29}
Basi nitakapomkamilisha na nikampulizia rohyangu, basi muangukieni kumsujudia.
فَسَجَدَ الْمَلَائِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ {30}
WakasujudMalaikwote pamoja.
إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ أَنْ يَكُونَ مَعَ السَّاجِدِينَ {31}
Isipokuwa Ibilisalikataa kuwa pamoja na waliosujudi.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU