Aya 120 – 124: Ibrahim Alikuwa Umma

Maana

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuashiria washirikina, katika Aya zilizotangulia, kwamba wao wamehalalisha haramu na kuharamisha halali, sasa anawatolea hoja kwa Ibrahim (a.s.) ambaye wanamtakasa na wanalazimisha kumfuata.
Mwenyezi Mungu amemsifu Ibrahim kwa sifa zifuatazo:
1. Hakika Ibrahim alikuwa ni umma. Wametofautiana katika kufasiri umma katika Aya hii. Razi amenukuu kauli nne, zenye nguvu zaidi ni kauli mbili: Kwanza kwamba Ibrahim alikuwa ni mwadilifu kwenye umma aliokuwa nao, Pili kwamba yeye alikuwa ni Imam. Vyovyote iwavyo ni kuwa makusudio ya umma hapa ni kuwa yeye alikuwa ni mkuu aliye adhimu.1
2. Mnyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu. Yaani mtiifu kwa Mungu.
3. Mnyoofu. Yaani mwenye kuachana na dini potofu, na kushikamana na haki.
4. Wala hakuwa katika washirikina. Hii ni kuwarudi washirikina ambao wanadai kuwa wao wako katika mila ya Ibrahim.
5. Mwenye kuzishukuru neema zake. Shukrani yake kwa Mwenyezi Mungu, kwa yale aliyomneemesha, alikuwa na ikhlasi.
6. Alimteua. Yaani alimchagua kuwa Mtume.
7. Na akamawongoza kwenye njia iliyonyooka, ambayo ni Uislamu sio Uyahudi wala Ukiristo:
مَا كَانَ إِبْرَاهِيمُ يَهُودِيًّا وَلَا نَصْرَانِيًّا وَلَٰكِنْ كَانَ حَنِيفًا مُسْلِمًا وَمَا كَانَ مِنَ الْمُشْرِكِينَ {67}
“Ibrahimu hakuwa myahudi wala mnaswara (mkristo), lakini alikuwa Mwislamu, mnyoofu na hakuwa katika washirikina” Juz. 3 (3:67).
8. Na tukampa wema duniani ambao ni kuadhimishwa na watu wa dini zote na kukubali kuwa yeye ni Mtume
9. Na hakika Akhera yeye atakuwa miongoni mwa watu wema. Hii ni kuitikiwa dua yake pale alisema:
رَبِّ هَبْ لِي حُكْمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ {83}
“Mola wangu nitunukie hukumu na uniunganishe na watu wema” (26: 83)
Kisha tukakupa wahyi kwamba ufuate mila ya Ibrahim mnyoofu na hakuwa katika washirikina.
Hii ni dalili kwamba Uislamu na dini ya Ibrahim ni moja katika itikadi na kuukana ushirikina. Basi mwenye kudai kuwa yuko katika dini ya Ibrahim na huku anaukana utume wa Muhammad atakuwa amejipinga yeye mweyewe, atake asitake.
Unaweza kuuliza kuwa Muhammad (s.a.w.) ni bwana wa Mitume, itakuwaje aamrishwe kumfuata Mtume mwengine?
Jibu: Lengo la kufuata hapa ni kuwarudi washirikina amabao wanaikubali dini ya Ibrahim na kuipinga dini ya Muhammad (s.a.w.) na hali ni kitu kimoja. Zaidi ya hayo ni kuwa amri ya kufuata hapa ni kwa kutangulia; yaani amfuate aliyemtangulia. Na kutangulia hakumaanishi ubora zaidi katika jamabo lolote.
Hakika Sabato iliwekwa kwa wale waliohitalifiana tu kwenye hiyo.
Makusudio ya kuwekwa ni kuwa ni wajibu; yaani Mwenyezi Mungu alilazimisha kuadhimishwa sabato (Jumamosi) na kuacha kufanyakazi kwa mayahudi peke yao wala haikuwekewa yeyote kabla yao wala baada yao.
Inasemekana kuwa jamaa miongoni mwao waliikataa Ijumaa; wakawa hawataki siku nyigine isipokuwa Jummamosi tu. Ndipo Mwenyezi Mungu akawakubalia, lakini kwa sharti la kuwa wasivue siku hiyo. Basi wakakubali sharti, lakini hawakulitekeleza; kama ilivyo desturi ya mayahudi siku zote na sehemu zote.
Mwenyezi Mungu hakubainisha sababu ya kutofautiana katika Sabato, kuwa je, walitofautiana katika ruhusa ya kufanya kazi siku hiyo, au walitofautiana kuhusu Sabato yenyewe kwamba wengine walisema ni sikukuu na wengine wakasema si sikuu?
Lililo na nguvu ni kuwa wao waliotofautiana katika uharamu wa kuvua siku hiyo; kama tulivyodokeza katika Juz.9 (7:163 – 166). Kwa sababu wote waliafikiana kuwa sabato ni sikukuu.
Na hakika Mola wako bila shaka atahukumu katika lile walilohitalifiana siku ya Kiyama.
Na hukumu yake siku hiyo itakuwa ni kuwapa thawabu watiifu na kuwaadhibu waasi.
ادْعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ ۖ وَجَادِلْهُمْ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ ۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنْ ضَلَّ عَنْ سَبِيلِهِ ۖ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ {125}
Waite kwenye njia ya Mola wakkwhekimna mawaidhmazurna ujadiliane nao kwa namna iliyboraHakikMola wakndiyanayemjua zaidi aliyepotea njia yake na Yeyndiyanayewajua zaidi walioongoka.
وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُمْ بِهِ ۖ وَلَئِنْ صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِلصَّابِرِينَ {126}
Na kama mkilipiza basi lipizeni kama mlivyofanyiwa. Nkammtasubiribasi hakika hivyo ni bora zaidi kwa wanaosubiri.
وَاصْبِرْ وَمَا صَبْرُكَ إِلَّا بِاللَّهِ ۚ وَلَا تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَلَا تَكُ فِي ضَيْقٍ مِمَّا يَمْكُرُونَ {127}
Na subiri na subira yako haikuwa ila kwa Mwenyezi Mungu, wala usihuzunike walusiwkatikdhiki kwa hila wanazozifanya.
إِنَّ اللَّهَ مَعَ الَّذِينَ اتَّقَوْا وَالَّذِينَ هُمْ مُحْسِنُونَ {128}
Na wale ambao wanatenda memHakikMwenyezi Mungyukpamojna wenye kucha.
  • 1. Mwenye tafsir Rawhil bayan alipofasiri Aya hii, alisema: “Imeelezwa katika Hadith ‘Hassein ni mjukuu katika vitukuu” yaani umma katika ummati. Kwa maana ya kuwa vitukuu ambao ni masharifu wanatokana na kizazi cha Zaynul’abidin, mtoto wa Husseni. Kwa hiyo ameeneza umma. Kisha akaendelea kusema mwenye Rawhil-bayan: “Baadhi ya jamaa wakati wake walisema kuwa Hussein ni mtume”. Na sisi hatujawahi kusikia hili. Hakuna shaka kwamba hilo ni ukafiri na ulahidi.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU