Vipi tunaweza kuimarisha Imani yetu?

Imani ni nuru, baraka kutoka kwa Allah. Hata hivyo, Imani ni elimu wakati huo huo, ambayo ni lazima isomwe. Kuna njia mbili za kuimarisha Imani yetu:
Njia ya kwanza na ya msingi ni kanuni za Sunnah na kuchunguza kwa mujibu wa Qur’an na Hadithi, kama inavyohitajika katika wakati wetu.
Njia ya pili ni kupanda daraja katika mambo ya kiroho kupitia kutekeleza matendo mema, kuutakasa moyo na roho kwa kuepuka dhambi.
Hata hivyo, hali ya karne hii inaifanya njia ya pili kuwa ngumu kuifuata. Kwa sababu hii, ni muhimu sana kusoma vitabu vinavyofunza Imani ya kuchunguza. Pia imekuwa muhimu kusoma sayansi kama sifa ya karne yetu, ukiachia mbali kusoma masomo ya dini. Hii ni kwa sababu nuru ya akili ni sayansi kama ilivyo nuru ya moyo ni masomo ya kidini. Tunaweza kusema kuwa moja kati ya vitabu  muhimu vyenye kufundisha yote mawili ni mkusanyiko wa Risale-i Nur. Kwa kuongezea, mtu anaweza kufaidika sana na vitabu vya watu maarufu kama imamu Al-Ghazali, Imamu Al-Rabbani, Imamu Mawardi na Imamu Qushairi.
Kuilinda na kuiimarisha Imani ni jambo muhimu zaidi kwa muislamu. Ni muhimu kuipa umuhimu Taqwa (Kumcha Allah) ili kuilinda Imani. Imani inaweza tu kulindwa ndani ya ngome ya Taqwa. Bila ya Taqwa, Imani hushuka. Ni muhimu kusoma na kufanya utafiti katika vitabu vinavyohusu Imani sana ili kuiimarisha Imani. Mambo ya Imani yanayotokana na elimu hayana taathira katika hisia za mtu labda yanapochujwa kupitia hoja. Kwanza, akili lazima iridhike.
Kutafakari ni muhimu sana. Ukweli wa mtume Ibrahim kumtambua Mola wake kwa kuangalia mwezi na nyota na kutafakari umeelezwa katika Qur’an. Imani huboreka kwa tafakuri. Kwa sababu hiyo, imeelezwa katika Qur’an kuwa
“Kutafakari kwa muda wa saa moja ni bora kuliko sala za sunna za mwaka mzima.”
Mazingira yana taathira kubwa kwa wanadamu. Dhambi hushauri watu ukafiri. Shauri lina taathira kubwa kwa wanaadamu. Linaingiza ukafiri ndani ya sehemu ya kutojitambua ya mtu bila ya watu kutambua. Kwa sababu hiyo, mtu anapaswa kuwa mbali na sehemu za dhambi kwa kadiri itakavyowezekana. Dhambi zinazotendwa bila ya mazingatio hushawishi watu kuwa hakuna akhera wala kuadhibiwa. Ili kulindwa na taathira hasi za mashauri kama hayo, mtu anapaswa kuwa mbali na sehemu za dhambi kadri awezavyo na kujaribu kuwashauri watu kuhusu wema na kuwakinga na shari kadri awezavyo. Mtu anapaswa kusoma mambo kuhusu Imani sana na kuwa makini na ujumbe unaotolewa ili kufidia uharibifu wa mashauri hasi aliyopewa. Ni muhimu kukutana na watu ambao wanajali kuhusu matendo mema na wanaishi kwa mujibu wa Taqwa. Katika hali kama hiyo, umuhimu wa jamii unadhihirika zaidi. Kama ilivyo dhambi kuwa inashauri hiana, matendo mema yanashauri Imani.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU