USHAURI; Jinsi Ya Kuondokana Na Tabia Ya Matumizi Mabovu Ya Fedha Na Kuweza Kujiwekea Akiba

Mambo yote kuhusu fedha yanaanzia kwenye misingi miwili muhimu kuhusu fedha. Misingi hii ni mapato na matumizi. Kila kitu kuhusu fedha, iwe ni kuishiwa, kuwa masikini, kuwa tajiri na hata kuwa na akiba na kuwekeza kutaanza na misingi hiyo miwili, mapato na matumizi. Matatizo yote ya kifedha na hata mafanikio yote ya kifedha yanaanza na misingi hiyo miwili, wale wanaoweza kuisimamia vizuri wanapata mafanikio na wanaoshindwa wanaishia kuwa na changamoto za kifedha.

Loading...
Karibu rafiki kwenye kipengele chetu cha USHAURI WA CHANGAMOTO mbalimbali ambazo zinatuzuia kufikia mafanikio tunayotaka kwenye maisha yetu. Kupitia kipengele hiki, wewe msomaji unaniandikia changamoto yako na mimi naijadili na kukushauri njia bora za kuondokana na changamoto hiyo. Kujua jinsi ya kutoa changamoto yako ili ushauriwe soma makala hii mpaka mwisho.

Leo katika kipengele hiki tutakwenda kujadiliana na kushauria kuhusu matumizi mabovu ya fedha ambayo yanawafanya watu kushindwa kuweka akiba na hivyo kubaki kuwa masikini. Karibu twende pamoja kwenye makala hii ya leo na mpaka kufika mwishoni utakuwa umepata mwanga wa hatua gani za kuchukua ili uweze kudhibiti matumizi yako na hatimaye kuweza kuweka akiba na hii kukufikisha kwenye uhuru wa kifedha.

Kabla hatujaingia kwenye kujadili mada ya leo, tupate maoni ya msomaji mwenzetu ambaye alituandikia kuomba ushauri juu ya changamoto hii ya kifedha;

Nikiwa na pesa mfukoni nikiona kizuri chochote na kununua bila kujali sina pesa nyingine ya akiba Na hatakama ninayo nyumbani nawaza kwenda kuichukua niwe nayo mfukoni. Naomba ushauri niondokaneje na hali hii.

Kama ambavyo tumesoma kwenye maoni ya msomaji mwenzetu hapo juu, tatizo lake ni kushindwa kudhibiti matumizi yake, badala ya yeye aiendeshe fedha, fedha imekuwa inamwendesha yeye.
Hili ni tatizo ambalo linawasumbua watu wengi, na limekuwa linawazuia wengi kufikia ndoto zao za kuwa na uhuru wa kifedha. Mtu anakuwa na mipango mizuri sana kabla hajapata fedha, ila akishazishika ile mipango yote inafutika na kujikuta anazitumia hovyo. Zikishaisha ndiyo anaanza kukumbuka kwamba alikuwa na mipango ya kifedha ambayo hajaitimiza.

Ni rahisi kuona hili kwa wengine kuliko kwetu binafsi, nenda popote na utakuta watu wakimzungumzia mtu ambaye amepata fedha nyingi kwa wakati mmoja, labda fedha za urithi au fedha za mafao, utasikia watu wakisema anatumia fedha vibaya. Lakini watu hao hao wape fedha na wataonekana wanatumia vibaya.

Fedha zimekuwa na changamoto nyingi sana kiasi ambapo zimewachanganya wengi, mpaka wengine wakaishia kuzipa majina mabaya. Na wengine wamekuwa wakiamini labda kuna nguvu zisizo za kawaida ambazo zinawaibia fedha zao. Hapa ndipo utakutana na watu wanakuambia kuna chuma ulete anawaibia fedha zao. Ukweli ni kwamba hakuna chuma ulete anayechukua fedha za mtu, bali mtu mwenyewe ndiye anakuwa chuma ulete wa fedha zake mwenyewe. Kama kungekuwa na mtu mwenye uwezo wa chuma ulete, asingehangaika na fedha ndogo ndogo za watu, badala yake angeenda kuchukua fedha nyingi benki kwa nguvu zake zisizo za kawaida.

Kama nilivyosema mwanzoni kwenye utangulizi wa makala yetu hii ya leo, changamoto zote za kifedha zinaanzia kwenye misingi miwili mikuu, mapato na matumizi.

Mapato ni ile fedha ambayo inakuja kwenye mfuko wako. Kitu chochote ambacho unafanya na watu wakakulipa ni njia yako ya kujipatia kipato. Na matumizi ni kile ambacho kinaondoka kwenye mfuko wako. Kitu chochote unachofanya kwa kutumia fedha yako ni matumizi.

Masikini wote kanuni yao iko hivi, matumizi yanakuwa makubwa kuliko mapato. Kwa njia hii wanaishi kwa madeni na hawawezi kuweka akiba yoyote. Wengi wanaishi kwa mkono kwenda kinywani, yaani chochote wanachopata wanakitumia.

Matajiri wote kanuni yao ni hii; mapato ni makubwa kuliko matumizi au matumizi ni madogo kuliko mapato. Kwa njia hii wanaweza kuweka akiba na kuwekeza, kitu ambacho kinawawezesha kupata zaidi na kufikia kwenye utajiri.

Kuna njia tatu za kutumia kanuni ya mapato na matumizi. Njia ya kwanza ni kuongeza mapato, njia ya pili ni kupunguza matumizi na njia ya tatu ni kufanya vyote kwa pamoja, kuongeza mapato na kuongeza matumizi.

Leo katika kumshauri msomaji mwenzetu tujikite kwenye kupunguza na kudhibiti matumizi. Hizo njia nyingine tutazijadili wakati mwingine.

Je unawezaje kudhibiti matumizi yako na kuweza kujiwekea akiba?
Hili ndilo swali ambalo tunahitaji kujiuliza ili kuweza kuondokana na matumizi mabaya, matumizi yanayotokana na msukumo wa hisia au mihemko. Hapa tutaangalia mambo muhimu ya kuzingatia ili kuweza kudhibiti na kupunguza matumizi ili kuweza kufikia uhuru wa kifedha.

Kwanza jua matumizi yako kwa sasa ni yapi. Unaweza kujua matumizi yako kwa kuorodhesha kila kitu unachofanya kwa kutumia fedha yako. andika kila shilingi ambayo umetumia kwenye siku saba zilizopita. Na kama huwezi kukumbuka vizuri fanya zoezi hili kwenye siku saba zijazo. Kila siku andika matumizi yako yote ambayo umeyafanya, hata kama umetumia shilingi mia tano au mia moja iandike. Usiache chochote. Wakati unafanya zoezi hili usijihukumu kwa lolote, wewe andika kila shilingi ambayo umeitumia.

Baada ya kujua matumizi yako ya kifedha, pitia orodha yako na kata yale matumizi ambayo siyo muhimu kwako. Na umuhimu upime kwa kigezo hiki, kama hutakufa kwa kukosa matumizi hayo basi siyo muhimu, yakate. Kwa njia hii kata kila matumizi ambayo kwa kuyakosa hutaharibu afya yako wala mahusiano yako na wengine. Kwa mfano sijawahi kusikia mtu kafa kwa kutokunywa soda, au kwa kutokununua nguo mpya, au kwa kutokununua gazeti. Vitu vingi vya anasa vitaondoka kwenye orodha yako hiyo.

Ukishaondoa yale matumizi ambayo siyo muhimu, sasa unabaki na orodha yako ya matumizi muhimu, haya ndiyo utakayoyafanya pekee.

Sasa hili zoezi haliishi kirahisi hivi, kuna changamoto nyingi hasa pale manunuzi yanapotokana na msukumo wa kihisia, na ili kuondokana na msukumo huu fanya yafuatayo;

1. Usitembee na kiasi kikubwa cha fedha kwa wakati wowote.
Hivyo pia usiwe na kiasi kikubwa cha fedha ambacho unaweza kukifikia kwa haraka kama vile benki au kwenye mpesa/tigo pesa. Badala yake fanya zoezi la kupata fedha kuwa gumu sana kwako, kwa mfano fungua akaunti maalumu ya benki ambayo hutaomba kuwa na kadi ya atm wala huduma za kifedha. Maana yake ukitaka fedha ni lazima uende mpaka benki, upange mstari ndiyo uchukue fedhga. Na fedha hizi zikishakua kidogo ziondoe na wekeza sehemu ambayo huwezi kuziondoa haraka.


2. Chelewesha manunuzi yako kwa muda.
Mara nyingi watu wamekuwa wakikutana na kitui na kushawishika kununua, huenda kwa mwonekano au maneno ya muuzaji. Lakini wanapofika nyumbani wanagundua kitu kile hakikuwa muhimu kwako. Hii huwatokea sana wakina dada na wakina mama hasa kwenye mavazi. Kuondokana na hali hii chelewesha manunuzi yako. Pale unapohitaji kununua kitu, jikubalie kwamba utanunua, lakini usinunue muda huo, badala yake jipe angalau siku saba za kufikiria kama kweli unataka kitu hiko. Ikiwezekana jipe hata siku 30. Ukifikiria kwa siku hizo utashangaa vitu vingi utasahau hata kama ulikuwa unataka kununua. Na hapa unahitaji kuwa na tahadhari kwa sababu wauzaji wengi ni wajanja na wanajua njia ya kukusukuma ununue muda huo, wanakuambia ni ya mwisho na hutapata tena, au bei itapanda, siyo kweli usiwasikilize, utakapohitaji utapata tu.

3. Jiwekee ukomo wa vitu unavyohitaji.
Hasa kwenye mavazi au starehe. Matumizi ya aina hii usipokuwa na ukomo utajikuta matumizi yanaongezeka kila siku. Kudhibitio hili kuwa na ukomo ambao huwezi kuuvuka. Kwa mfano kwenye mavazi jiwekee ukomo kwamba hutanunua nguo mpya mpaka uwe umeshavaa zile zote ambazo unazo kwa sasa.

4. Yatumie matumizi yako kama hamasa ya kuongeza kipato.
Njia nyingine ya kudhibiti matumizi yako ni kuyatumia kama hamasa ya kuongeza kipato chako. Na hapa unachofanya ni pale unapoona kitu ambacho unataka kununua, jiambie utanunua kitu hiko kama utaweza kutengeneza fedha za ziada, tofauti na ulizonazo sasa. Na hapa iweke akili yako kazini ili kukuonesha njia mbadala za wewe kupata fedha za kununua kile unachotaka. Kwa njia hii utaacha matumizi hayo kama hutapata kipato cha ziada, na kama utakipata basi utakuwa umejiongezea njia za kipato.

5. Kula nyumbani badala ya kula kwenye migahawa, nunua vitu vya jumla badala ya kununua kwa reja reja.
Haya pia ni mambo ambayo yanakuwezesha kupunguza gharama zako za maisha hasa pale unapokuwa na familia. Badala ya kula vyakula vya kununua, ni vyema mkapika na kula nyumbani. Na badala ya kununua vitu kwa reja reja, nunua kwa jumla, hii siyo tu inapunguza gharama, bali inakuondolea usumbufu wa matumizi madogo madogo ya kila siku.
Fanyia kazi haya ambayo umejifunza kuhusu kudhibiti na kupunguza matumizi ili uweze kufikia uhuru wa kifedha.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU