NYIRADI KUBWA ZAIDI:

Sheria inataka sura za kinga zisomwe kila asubuhi na jioni. Imenukuliwa katika Hadithi kwamba: «Soma (Qul Huwallahu Ahad) na (Qul Auudhu Birabbil Falaq na Qul Auudhu Birabbin-naas) wakati wa asubuhi na wakati wa jioni mara tatu, zitakutosha kwa kukukinga dhidi ya kila kitu». (Tirmidhiy 3575)
Na kila baada ya swala ya faradhi, kama Mtume alivyomfundisha Swahaba mmoja. (Abudaudi 1523)
Na kabla ya kulala. Mtume alipokuwa akipanda kitandani kwake kila usiku alikuwa akiviweka pamoja viganja vyake halafu anatabana humo na kusoma (Qul Huwallahu Ahad) na (Qul Auudhu Birabbil Falaq) na (Qul Auudhu Birabbin-naas), halafu anajipangusa kwa kutumia viganja hivyo sehemu awezazo katika mwili wake akianza kichwa chake na uso wake na sehemu ya mbele ya mwili wake. Anafanya hivyo mara tatu». (Bukhariy 4729)
Sura hizo ni kinga kubwa sana inayomkinga mwanadamu dhidi ya uchawi na uovu. «Mtume alikuwa akiomba kinga dhidi ya majini na macho ya watu mpaka ziliposhuka sura za kinga. Alizitumia sura hizo na kuacha nyinginezo». (Tirmidhiy 2058)

Nyiradi muhimu

Hii ni aya kubwa sana katika Qur’ani kama ambavyo Mtume amelieleza hilo, kwa sababu ya Allah anavyotukuzwa humo na sifa zake kamilifu na uwezo wake mkamilifu unaotajwa humo.
Sheria pia inataka aya hii isomwe asubuhi na jioni na kabla ya kulala. Imenukuliwa katika Hadithi kwamba, mwenye kuisoma aya hii kabla ya kulala ataendelea kuwa katika ulinzi wa Allah na shetani hatamsogelea mpaka asubuhi. (Bukhariy 2187)
Pia inasomwa baada ya swala. Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusoma Aya Kursiy baada ya kila swala ya faradhi hakuna kitakachomzuia kuingia peponi isipokuwa kifo tu». (Annisai 9848) 
«Allahu Laa Ilaaha Illaa Huwal-hayyul-qayyuum. Laa Ta’khudhuhuu Sinatun Walaa Nauum. Lahuu Maa Fissamaawaati Wamaa Fil-ardhi. Man-dhalladhii Yashfau Indahuu Illaa Bi-idhnih. Yaalamu Maa Baina Aydii Him Wamaa Khalfahum. Walaa Yuhiitwuuna Bishai-in Min-ilmihii Illaa Bimaa Shaa’a. Wasia Kursiyyuhussamaawaati Wal-ardhi. Walaa Yauuduhuu Hifdhuhumaa Wahuwal-aliyyul-adhwiim». (Sura Albaqara, aya 255)
«Allahu Laa Ilaaha Illaa Huwa»
Allah ni ambaye hakuna anayestahiki kuabudiwa kwa haqi ila yeye tu.
«Alhayyul-qayyuum»
Aliye hai, ambaye yeye tu ndiye mwenye maana zote za uhai mkamilifu unaolingana na utukufu wake, msimamizi wa kila jambo kwa kuliandaa na kulifanya vizuri. 
«Laa Ta’khudhuhuu Sinatun Walaa Nauum»
Hasinzii wala halali.
«Lahuu Mafis-samaawaati Wamaa Fil-ardhi»
Ni vyake yeye tu vyote vilivyomo ulimwenguni; mbinguni na ardhini, kwa sababu yeye ndiye mwenye kuvimiliki.
«Man Dhalladhii Yashfau Indahuu Illaa Bi-idhnih»
Hakuna yeyote atakayekuwa na ujasiri wa kuombea mbele yake isipokuwa kwa idhini yake tu.
«Yaalamu Maa-bayna Aydiihim Wamaa khalfahum»
Anajua mambo yao yajayo na ya zamani yaliyopita.
«Walaa Yuhiitwuuna Bisha-in Min-ilmihii Illaa Bimaa-shaa’a
Hakuna kiumbe yeyote anayejua chochote katika anayoyajua Allah isipokuwa tu yale ambayo Allah amemjuza na kumfahamisha.
«Wasia Kursiyyuhussamaawaati Wal-ardhi»
Baadhi ya wafasiri wamefasiri «Kursiy» kwamba ni mahali ilipo miguu ya Allah kwa namna inayolingana na utukufu wake. Kursiy ni miongoni mwa viumbwa vikubwa vya Allah ambavyo vinazishinda mbingu na ardhi kwa ukubwa na upana.    
«Walaa Ya-uuduhuu Hifdhuhumaa»
Hakumuelemei Allah kuzitunza mbingu na ardhi na vilivyomo humo. 
«Wahuwal Aliyyul Adhiim»
Na yeye kwa dhati yake na sifa zake yuko juu ya viumbe vyake, ni mwenye sifa zote za utukufu na ukubwa.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU