Ni sababu zipi zilizofanya Dunia ya Kiislamu iwe nyuma katika sayansi na teknolojia?

Dear Brother / Sister,
“Kwa kuwa ni kweli kuwa kila mara ukweli hushinda, kwa nini kafiri humshinda muumini na nguvu huushinda ukweli?” Mkusanyiko wa Risale-i Nur, Maneno, 725
Kuna maradhi yaliyokuwa yakitajwa mara kwa mara katika siku za nyuma na ambayo kwa sasa yanarejea: Kuchukulia kuwa dini ni kikwazo dhidi ya maendeleo na kuinasibisha dini ya Uislamu na ukosefu wetu wa maendeleo ikilinganishwa na ulimwengu wa Kikristo.
Kabla ya kujibu swali hili, kwanza ninataka kutaja baadhi ya nukta. Mstari tunaouchora kati ya nukta hizi utatufikisha katika jibu la kwanza la swali hili. 
Nukta ya Kwanza
Katika kipindi ulipoibuka Uislamu, Waislamu waliteseka kwa ukandamizaji na uchokozi wa waabudu masanamu kwa muda na baadaye ikaja dola na kudumu katika maendeleo mpaka karne iliyopita. Huo ni uthibitisho wa kwanza wa ukweli huu kuwa Enzi za Upeo wa Furaha (wakati wa Mtume) zilikuwa ni za imani, maadili, fadhila, haki na amani. Baada ya hapo, Andalusia ikawa mtangulizi wa elimu kwa ajili ya Ulaya; na Dola za Seljuk na Uthman zilifikia vilele vya juu sana katika elimu na sanaa ambazo haiwezekani kufichwa kwa madai ya namna hiyo.
Hapa, tunataka kutofautisha baina ya maneno Uislamu na Muislamu. Waislamu ndio wenyewe wanaoendelea na kurudi nyuma. Uislamu ni kama ulivyo.
Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini.” (Qur'an, Al-Ma'idah Surah, 5:3)
Basi jibu la swali hili linatakiwa litafutwe kwa kuwa:
Lini tulipokuwa wafuasi wazuri wa Uislamu: Lini tulipojenga dola kadhaa au tuliporudi nyuma kimaendeleo?
Nukta ya Pili
Wale walionasibisha kurudi nyuma kwetu na Uislamu wanapaswa wawaache pembeni Waislamu na washughulikie Uislamu; waseme “Kanuni kadhaa wa kadhaa za Qur'an na hadithi kadhaa wa kadhaa za Mtume ziko kinyume na maendeleo.” Matokeo ya madai yao, yatakuwa katika mipaka ya jitihada za kuleta ushahidi.
Mathalani, wanapaswa wathibitishe kuwa kukataza uongo, matendo mabaya na uonevu, pombe, kamari, uzinifu, hila, riba, usengenyaji, ubaguzi wa kimbari na kwa kifupi kukataza maovu yote ni dhidi ya maendeleo. 
Nukta ya Tatu 
Kuna jukumu jingine linalowapasa wenye kulinasibisha na Uislamu kuwa Wakristo wameendelea zaidi kuliko sisi. Na wajibu huo ni kutafuta kanuni za teknolojia ya leo na maendeleo yakinifu katika Agano Jipya na kuleta hoja kwa kusema “Tumerudi nyuma kwa sababu hatuna hiki na kile.” Hawataweza kufanya hivyo. Kwani, hakuna hata aya moja katika Agano Jipya kuhusu maisha ya kibiashara au kuongoza dola.
Hebu tutaje nukta ya mwisho na kuenda kwenye jibu:
Wanaoleta dai hili wanapaswa wathibitishe mfumo wa elimu uliomgeuza mtu mwenye bidii, mjasiri, mzalendo na mwaminifu wa nyakati zilizopita kuwa ni mtu fidhuli, mwenye tamaa na ubinafsi katokea katika Uislamu.
Hebu sasa tujaribu kujibu swali kwa kurejea katika kazi za mtunzi wa Mkusanyiko wa Risale-i Nur, Badiuzzaman Said Nursi.
Katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur, huko Lemeat, kuna swali:
Mara mtu mmoja alipouliza: “Kwa kuwa ni kweli kuwa ukweli kila mara hushinda, kwa nini kafiri anamshinda muumini na nguvu inaushinda ukweli?
Hiyo inamaanisha kuwa, “Kwa kuwa ukweli uko juu zaidi na kwa kuwa hauwezi kushindwa, kwa nini makafiri wanawashinda Waislamu na wenye nguvu wanawashinda wenye haki?
Jibu la swali hili linatolewa kwa kifupi na kutosheleza likiwa na vipengele vyake vinne tofauti:
Kwanza, njia zinashughulikiwa na kuainishwa kwamba katika dunia hii ya hekima njia na sababu hugongana. Iwe Muislamu au Asiye-Muislamu, yeyote anayetimiza masharti ya kinachokusudiwa kukipata, na kuendana kikamilifu na sababu na njia zake atafanikiwa. Ni wazi kuwa mtu anawezaje kupata mafanikio kutokana na kitu chini ya masharti yapi, kwa mbinu zipi na kwa mpango wa namna gani. Mwenye kushikamana na masharti hayo na kutumia njia hizo atafanikiwa.
Dhana 'uwezo' iliyoelezwa katika swali imetajwa kama ifuatavyo: “Uwezo una haki ya hilo, na kuna mastaajabu katika kuumbwa kwake.
Ukitaka ufanikiwe, na ukitaka kuwashinda maadui au washindani wako, jaribu kuwa mwenye uwezo. Kwa kuwa, uwezo pia huna haki yake wenyewe. Yeyote mwenye haki hiyo mkononi mwake mara nyingi huwa ndio mshindi. Kama unagonganisha chuma na mbao, ni wazi kuwa mti utashindwa.
Pili, jambo hilo linashughulikiwa kuhusiana na dunia ya sifa walizo nazo wanaadamu. Sifa zote nzuri zimo katika jina la neno “Allah” na zimeoneshwa vyema kabisa na mjumbe wa Allah, rehema na amani zimfikie. Hata hivyo, kivitendo, inawezekana Muislamu asifanikiwe katika kuzidhihirisha sifa zote hizo nzuri maishani mwake kwa sababu ya nafsi, shetani, upotovu wa kijamii, na sababu nyingine nyingi. Halikadhalika, asiye Muislamu anaweza kuwa na baadhi ya sifa nzuri kutokana na elimu aliyoipata na zilizo katika jamii. Hizo ni sifa za Muislamu alizo nazo. Kazi inapotakiwa kufanywa, sifa hizo sio imani zilizo nyoyoni ndizo hujitokeza.
Hebu tutoe mfano wa kibiashara: Sifa za namna hiyo kama vile elimu, uaminifu, bidii, kupangwa na kuwekewa kanuni huathiri matokeo ya biashara moja kwa moja. Kama asiye-Muislamu atakuwa na sifa hizi na Muislamu akakosa, ni jambo la kawaida kuwa huyu asiye -Muislamu atakuwa tajiri kuliko Muislamu. Hapa, kafiri hamshindi muumini; bali sifa za muislamu zinazishinda sifa za asiye Muislamu. Na mshindi yupo, katika ulimwengu wa sifa, tena ni ukweli.
Nukta hii inaweza kutajwa ili kutufungulia taswira:
“Na katika dunia, haki ya kuishi ni ya wote. Huruma hii iliyowaenea wote ina nukta muhimu na mastaajabu ya hekima; ukafiri si kikwazo.”
Haki ya kuishi ni ya kuenea wote. Hiyo inamaanisha kuwa, katika muktadha huu, hakuna tofauti baina ya muumini na kafiri, binadamu na mnyama. Yeyote aliyepewa uhai amepewa na riziki. Riziki si jaza ya imani na ibada, bali ni jaza ya uhai. Jaza ya imani na ibada ni upeo wa furaha ya milele katika makazi ya akhera.
Tunaweza kuendelea na fikra zetu kutokana na taswira hii kama ifuatavyo:
Ili kumdhihirishia kila mmoja kuhusu majina ya Allah, kuna vioo tofauti na majukwaa mbalimbali. Mengi katika hayo hayahusiani na imani ya mtu. Mathalani, mkulima anayetaka kupata mafungu zaidi kutokana na dalili za jina Ar-Razzaq (Mwingi wa Kuruzuku) atapata mazao zaidi pindi atakapotii masharti muhimu kwa ajili ya hili. Hapa, imani ya mtu si kigezo. Tena, mtu anayetaka jina Ash-Shafii (Mwenye kujaalia Afya) lidhihirishwe kwake atatumia dawa muhimu. Hapa, pia, imani yake si kigezo. Kwani, anajua namna ya kuomba kudhihirishwa jina hili na matokeo yake ananeemeshwa afya. Mtu asiyefuata njia hii, hata kama ni muumini kikamilifu, huenda asipate afya.
Hivyo, kama Muislamu atataka kunufaika kutokana na baraka za majina ya Allah katika maisha ya duniani, anapaswa ajaribu awe kioo stahiki kwa ajili ya udhihirishwaji huo. Vinginevyo, hataweza kupata matokeo anayotaka. Hata hivyo, muumini huyo huyo analenga katika kupata baraka za Allah katika makazi ya akhera kwa kutii masharti ya ibada, amali njema na unyoofu.
Mtu asiyetii masharti haya hatakuwa na fungu lolote Peponi, hata kama ana mafanikio gani katika dunia.
Kipimo cha tatu cha suala hili kimeoneshwa katika Mkusanyiko wa Risale-i Nur kama ifuatavyo:
Allah ana vipengele viwili vya kanuni. Mojawapo ni kanuni za Qur'an, ambayo huweka nidhamu ya amali za binadamu zinazotegemea utashi wake huru. kipengele kingine kina kanuni zinazohakikisha nidhamu ya ulimwengu na ya vilivyomo ndani mwake. Jambo la kwanza ni Shari'ah (Sheria ya Kislamu); na ya pili ni Shari'ah at-Takwin (Sheria ya Kuumbwa). Sheria za asili zimo katika kundi hili la pili.
Imeoneshwa na Badiuzzaman kuwa wenye kutii na wanaoasi hukumu za Qur'an watapata malipo yao na adhabu zao kwa ujumla huko akhera na kwamba wenye kutii sheria ya kuumbwa na wasiofanya hivyo watalipiziwa kwa ujumla duniani. Kwa mujibu wa hayo, muumini asiyetii sheria ya kuumbwa atapata adhabu yake katika namna ya kukosa mafanikio na taabu duniani. Na asiye Muislamu anayefuata sheria hizi atapata jaza ya kutii utashi wa Allah duniani, hata kama hajui hilo.
Nukta hizi tatu ndizo sababu za mafanikio na ukosefu wa mafanikio. Na sehemu kubwa ya jambo hili inaweza kuelezwa na nukta moja au mbili katika hizo. Pia inaweza kujitokeza kuwa hatufanikiwi ingawa tumetimiza masharti yote. Hapa, tunapaswa tutafute siri ya rehema na hekima ya Uamuzi wa Kiungu. Katika sehemu ya jibu lijalo, nukta hii imeelezwa; kwa maneno mengine, taswira ya Utashi wa Kiungu na Uamuzi wa kiungu imesisitizwa.
Katika nukta ijayo, katika Risale-i Nur, kumesisitizwa kuwa wakati mwingine inasaidia ukweli kustawi kwa uongo kuushinda ukweli hata kama kwa kipindi kifupi, na kuimarisha na kuung’arisha ukweli.
Nukta hii ina umuhimu mkubwa kwa hili:
Katika hadithi (kwa maneno ya Mtume), yafuatayo yameelezwa: “Taabu nyingi huwapata mitume, na kisha waja wengine wapenzi wa Allah kulingana na daraja zao.” Ni siri ya Mola Mlezi na hekima ya Allah kuwa mitume wengi walitukanwa na watu wao, walifukuzwa kutoka katika ardhi ya kwao na waliteswa. Matatizo yaliyoyapata ni 'ibada hasi', kwa maneno ya mtunzi wa Mkusanyiko wa Risale-i Nur. Malipo ya ibada hii, iliyoegemea juu ya subira, inayolazimisha mtu kufanya mtu anachopaswa kukifanya kwanza na matokeo yake baadaye kumtumaini Allah, na ambayo ni vigumu kuistahamilia, halikadhalika ni kubwa. Kwa majaribu hayo, waja wapenzi wa Allah, mitume wakiongoza, wote huendelea kiroho na njia yao ya kweli kwa kawaida inatulia katika nyoyo za watu hata kama itachelewa vipi, kutokana na kuteseka kwao katika hali ya subira. Wakati wale waliowaonea na kuwadhulumu wanaadhibiwa makaburini mwao, wafuasi wao wanaishi na kuwafanya wengine waishi katika ukweli duniani.
Kama ilivyo kutofautiana mchana na usiku hunufaisha ukuaji wa mmea, halikadhalika nuru ya Jalal (mtukufu) na Jamal (mzuri) inavyoathiri ustawi wa roho ya binadamu.
Hii ni hekima ya kiungu. Na shida na majaribu wanayoyapata marafiki wa ukweli katika duru za siri hii hazihusiani na nukta tatu za mwanzo.
Maswali juuyau islamu
ULIZA SWARI LOLOTE UTAJIBIWA LIHUSUYO DINI TUMA SMS 

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU