NAMNA YA KUHIJI

  1. Mwenye kuhiji atahirimia (atanuia kuingia katika ibada ya hija) siku ya nane ya mwezi wa Dulhijja akiwa Makka. Atatia nia moyoni mwake; kwa maana ya kuingia katika ibada ya hija. Atatamka kwa ulimi wake: «Labbaika llaahumma hajjan». Maana yake ni kwamba: (Ewe Mola wangu, nimeitikia kuja katika hija). Baada ya kunuia huko ataleta Talbiya akitangaza utumishi, ufuasi na kuitikia wito wa Muumba pekee kwa kusema: «Labbaika-llaahumma labbaiik. Labbaika laa shariika laka labbaiik. Innalhamda, wanniimata, laka walmulk. Laa shariika laka labbaiik». Maana yakeni kwamba: Nimekuitikia Mola wangu, nimekuitikia. Nimekuitiki ewe usiye na mshirika nimekuitikia. Hakika, sifa njema na neema na ufalme ni vyako wewe tu. Huna mshirikia. Nimekuitikia
Atavaa nguo za Ihramu, na atajizuia asifanye mambo yote yaliyokatazwa na ambayo mwenye kuingia katika ibada ya hija anakatazwa kuyafanya mpaka akomboke na kumaliza, kama inavyo oneshwa katika jedwali ya pembeni:
  1. Sheria inamtaka kwamba baada ya kuhirimia siku ya nane ya mwezi wa Dhul-hijja aende Mina wakati wa Dhuhaa, alale hapo, aswali hapo swala ya Adhuhuri, Alasiri, Magharibi, Ishaa na Alfajiri. Kila swala aiswali kwa wakati wake bila ya kujumuisha, pamoja na kupunguza swala za rakaa nne na kuziswali kwa rakaa mbili mbili.
  2. Katika siku ya tisa ya mwezi wa Dhul-hijja atakwenda Arafa baada ya kuchomoza kwa jua. Ataswali Adhuhuri na Alasiri kwa kuzijumuisha na kupunguza rakaa kwa Adhana moja na Iqama mbili. Halafu watu wataomba dua na kujinyongesha mbele ya Allah. Arafa ndio tukio kubwa sana miongoni mwa matukio ya hija mpaka Mtume,swallalahu alayhi wasalam, ameeleza kwamba Allah hujivuna mbele ya Mailaika wake kupitia watu walioko Arafa kutokana na hali waliyo nayo ya kuomba dua, unyenyekevu na kumlilia Allah. Mtume swallalahu alayhi wasalam anasema kwamba: «Hawa ni waja wangu wamenijia wakiwa nywele kitimtim, wamejaa vumbi. Ninakushuhudizeni kwamba nimewasemehe». (Ahmad, Hadithi Na. 7089).
  3. Ataondoka Arafa kwa utulivu baada ya kuzama kwa jua akielekea Muzdalifa. Ataswali Magharibi na Isha kwa kuzijumuisha. Atalala Muzdalifa na kuswali Alfajiri hapo. Ni sunna kwake kumtaja Allah na kumuomba mpaka kupambazuke na kabla ya kuchomoza kwa jua. Inafaa kwa wanawake, watu wenye udhaifu na wazee pamoja na wanaofuatana nao kuondoka Muzdalifa baada ya usiku kugawanyika nusu.
  4. Ataondoka Muzdalifa kabla ya kuchomoza kwa jua kwenda Mina. Hii ni siku ya Eid. Sheria inamtaka aliyemo katika ibada ya hija kufanya mambo kadhaa katika siku ya Eid, na amabayo ni haya: 
  • Kuurushia vijiwe saba mnara mkubwa huku akileta Takbira katika kila kijiwe anacho rusha. Minara (Jamaraat) ni sehemu ambazo shetani alimuwekea pingamizi baba wa Mitume Ibrahimu, Allah amfikishie amani, kwa kumshawishi asitekeleze amri ya Allah. Mtume Ibrahimu alimrushia vijiwe saba shetani huyo. Allah amelifanya tukio hilo kuwa sheria kwetu. Kwa hiyo, tunalifanya hilo kwa ajili ya kumtii Allah Mtukufu, kufuata vile alivyotuamrisha, kumuiga Mtume wa Allah ambaye pia amefanya hivyo, na pia tunafanya hivyo ili tuzipe nafsi zetu msukumo wa kupambana na shetani na udhaifu uliopo katika nafsi zetu na uchaguzi wetu wa mambo ya kufanya.
  • Atachinja mnyama wake hapo Mina au Makka siku ya Eid. Muda wa kuchinja unaendelea siku tatu baada yake. Atakula, atatoa zawadi na atatoa sadaka. Kama hana uwezo wa kununua mnyama wa kuchinja, atafunga siku tatu akiwa hija na siku saba atakapo rejea nyumbani kwake. Inawezekana kwa mwenye kuhiji kuipa uwakala taasisi inayoaminika kwa ajili ya kuchinja mnyama wake na kugawa nyama yake kwa wenye shida. 
  • Atanyoa nywele zake au atapunguza. Kwa hatua hii, atakuwa amekomboka (Uhuru wa kwanza). Kwa maana hiyo, ataruhusiwa kufanya yote aliyokatakazwa kufanya kwa sababu ya kuingia katika ibada ya hija isipokuwa tu kukutana kimwili na mkewe
  • Ataelekea Makka ili kutufu Tawafu Ifadha(twawaf ya hijja), mara saba kuzunguka Kaba Tukufu.  Tawafu Ifadha ni moja ya nguzo za hija. Halafu baada yake atakwenda kufanya Saayi ya hija. Kwa kufanya Tawafu, atakuwa amehalalishiwa yote aliyokatazwa kufanya kwa kuingia katika ibada ya hija. Kila kitu kilichokuwa haramu kwa sababu ya Ihramu kitakuwa halali kwake, hata kukutana na mkewe. Inawezekeana kwake kuahirisha kufanya Tawafu siku ya Eid iwapo itakuwa uzito kwake. 
  1. Kisha atarejea Mina na kulala hapo siku mbili kwa mwenye kufanya haraka kuondoka na siku tatu kwa watakao chelewa kuondoka. Sheria inamtaka kuirushia vijiwe minara mitatu kila siku baada ya jua kupinduka kutoka usawa wa kati (muda wa swala ya Adhuhuri): Mnara mdogo (ambao uko mbali na Makka), kisha Mnara wa kati, kisha Mnara mkubwa ambao aliurushia vijiwe siku ya Eid. 
  2. Atakapo taka kuondoka Makka itamlazimu, kabla ya kuondoka, atufu Tawafu ya kuaga, ili uhusiano wake wa mwisho na Kaaba Tukufu uwe kuitufu.   

Mambo ya haramu kufanya ukiwa umehirimia.

  1. Kunyoa nywele au kuzipunguza. Na ni mfano wake kukata kucha.
  2. Kutumia manukato, sawa iwe kwenye nguo yake au mwilini mwake
  3. Kukutana kimwili mke na mume. Pia kugusa na kukumbatia iwapo kutafanyika kwa matamanio.
  4. Kufunga ndoa; ni sawa aliyeingia katika ibada ya hija ni mwanaume au mwanamke.
  5. Mwenye kuingia katika ibada ya hija anakatazwa kuwinda mnyama. Haifai kwake kuwinda  ndege na wanyama pori.
  6. Makatazo yanayowahusu wanaume tu ni haya:
  • Kuvaa nguo inayo onesha mchanganuo wa maungo kwa namna kwamba kila kiungo kinabainisha nguo iliyovaa na kujitenga, kama vile shati, kanzu,  nguo ya ndani, suruali na mfano wake.
  • Kufunika kichwa kwa kitu kinacho gusana na kichwa. Ama mapaa ya majengo, vyombo vya usafiri na myamvuli inayofunika kichwa haina ubaya.
  1. Makatazo yanayomhusu mwanamke tu ni haya:
  • Kuvaa barakoa (nikabu) na kufunika uso. Jambo linalotakiwa na sheria ni mwanamke kufunua uso wake, isipokuwa tu watakapo pita mbele yake wanamume ambao sio maharimu zake. Hapo anaweza kufunika uso wake na haitamdhuru iwapo hiki anachotumia kufunikia uso wake kitaugusa uso.  
  • Kuvaa glovu(soksi za mikononi).
Mwenye kufanya lolote kati ya haya yaliyokatazwa kwa kusahau au kwa kutojua au kwa kulazimishwa, hana kosa, kwa mujibu wa kauli ya Allah  isemayo kwamba: «Na hakuna ubaya kwenu katika yale ambayo mmeyafanya kwa kukosea, na lakini ubaya upo katika yale ambayo nyoyo zenu zimekusudia kuyafanya». (Sua Al-ahzaab, aya 5). Lakini iwapo atakumbuka au akapata kujua kuwa haifai kuyafanya, basi aliache haraka hilo alilokatazwa.
Msikiti wa Khaif na mahema ya mahujaji yanaonekana huko Mina.

Umra

Ni kumuabudu Allah kwa kuhirimia (kunuia kuingia katika ibada ya Umra = Ihraam), kuzunguka Kaaba mara saba, kufanya Saayi kati ya Swafaa na Mar`wa mara saba, kisha kunyoa au kupunguza nywele. 
Hukumu yake: Ni wajibu kwa watu mwenye uwezo, mara moja tu katka umri. Ni jambo linalo pendekezwa kurudia rudia kufanya Umra.
Wakati wake: Inafaa kufanya Umra muda wotewote wa mwaka, lakini kuifanya katika mwezi wa Ramadhani kuna malipo mengi zaidi, kama Mtume,swallalahu alayhi wasalam, alivyosema kuwa: «Umra ndani ya Ramadhani inahukumika kuwa ni kuhiji pamoja na mim». (Bukhari, Hadithi Na. 1863).

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU