MWENYEZI MUNGU NI MMOJA WA KWELI KATIKA
(Agano la kale):
" Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. (Kumbukumbu la torati 6:4).
"Je! Mwenyezi Mungu mmoja hajatuumbia roho ya maisha na kuturuzuku"?. (Malaki 2:15).
" Ninyi ni mashahidi wangu, asema Bwana, na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine. Mimi, naam, mimi, ni Bwana, zaidi yangu mimi hapana mwokozi ". (Isaya 43:10-11).
" Bwana, Mfalme wa Israeli, Mkombozi wako, Bwana wa majeshi, asema hivi; Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu. "?. (Isaya 44:6).
" Hubirini, toeni habari; naam, na wafanye mashauri pamoja; ni nani aliyeonyesha haya tangu zamani za kale? Ni nani aliyeyahubiri hapo zamani? Si mimi, Bwana? Wala hapana Mungu zaidi ya mimi; Mungu mwenye haki, mwokozi; hapana mwingine zaidi ya mimi. (Isaya 45:21).
Je! Unakumbuka dalili nyingine kama hizo.
MWENYEZI MUNGU NI MMOJA WA KWELI KATIKA (Agano jipya):
" Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma (Yohana 17:3).
" Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake " (Matayo 4:10).

Comments
Post a Comment