MAKUSUDIO YA HIJA

Hija ina makusudio na malengo makubwa kwa mtu na jamii, na ndio maana Allah baada ya kutaja mambo yaliyo wajibu kwa mwenye kufanya ibada ya hija, ikiwa ni pamoja na mnyama ambaye anamchinja kwa ajili kujiweka karibu na Allah, amesema kuwa: «Hazitamfikia Allah nyama zake wala damu zake na lakini utamfikia uchamungu kutoka kwenu». (Sura Alhajj, aya 37). Mtume,swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakuna vingine isipokuwa kwamba imewekwa Tawafu katika Nyumba Takatifu, na (Saayi) kati ya Swafaa na Mar`wa na kutupia vijiwe minara kwa lengo kudumisha kumkumbuka  Allah tu». (Abuu daudi, Hadithi Na. 1888).
Miongoni mwa malengo na makusudio hayo ni haya: 
  1. Kuonesha udhalili na unyenyekevu kwa Allah
Hili linatokana na kwamba mwenye kuhiji: anaachana na sababu za starehe na mapambo,  anavaa nguo za Ihram kwa kuonesha uhitaji kwa Mola wake, anajiweka mbali na dunia na mishughuliko yake ambayo inaweza kumtoa katika kumtumikia Mola wake. Kwa kufanya hivyo, anajiweka katika nafasi ya kupata msamaha na rehema za Mola wake.
 Kisha anasimama Arafa akiwa mnyenyekevu kwa Mola wake, akimsifia, akishukuru neema na Fadhila zake na kuyaombea msamaha  madhambi na makosa yake. 
  1. Kushukuru neema
Shukurani katika kutekeleza ibada ya hija zinapatikana kwa kuzingatia pande mbili: Kushukuru neema ya mali na afya njema. Mambo haya mawili ndio neema kubwa sana za duniani ambazo mwanadamu anafaidika nazo. Katika kufanya ibada ya hija kuna kuzishukuru neema hizi kubwa, pale ambapo Muislamu anasumbuka yeye mwenyewe na kutoa mali yake kwa ajili ya kumtii Mola wake na kujiweka karibu naye. Hapana shaka kwamba kushukuru neema ni jambo la wajibu ambalo akili ya kawaida inalikubali na sheria ya dini inaliona kuwa la lazima. 
  1. Waislamu Kukutana
Waislamu kutoka pembe zote za dunia hukutana katika hija. Hufahamiana na kuzoeana. Hapo, zinayayuka tofauti kati ya watu; tofauti kati ya tajiri na masikini, tofauti za kijinsia na rangi na tofauti za lugha. Kauli ya Waislamu inakuwa moja katika mkutano mkubwa wa wanadamu ambao kauli yao imeungana katika wema, uchamungu, kuusiana kutenda haki na kuusiana kuwa na subira. Lengo kuu la mkutano huo ni kuunganisha sababu za maisha na sababu za mbinguni.
  1. Kukumbuka Siku ya kiama
Hija inamkumbusha Muislamu siku ya kukutana na Mola wake. Mwenye kufanya ibada ya hija anapoacha kuvaa nguo zake za kawaida na akaleta Talbiya akiwa katika nguo za Ihram, akasimama katika viwanja vya Arafa, akaona watu walivyokuwa wengi na mavazi yao yakiwa ya aina moja yanayofanana na sanda, picha hii itampeleka Muislamu kwenye kukumbuka matukio yatakayomtokea baada kufa kwake. Jambo hilo litamfanya ajiandae kwa ajili ya matukio hayo na kufanya maandalizi kabla ya kukutana na Allah.
  1. Kuonesha upekee wa Allah na kumuabudu yeye tu kwa kauli na vitendo
Kaulimbiu ya Mahujaji ni Talbiya (Labbaika-llaahumma labbaiik. Labbaika laa shariika laka labbaiik. Innalhamda wanniimata laka walmulk,Laa shariika lak).Kwa jili hii, Swahaba mmoja katika kuielezea Talbiya ya Mtume alisema kuwa: «Aliitangaza Tauhidi (Upekee wa Allah)». (Muslim, Hadithi Na. 1218). Upekee wa Allah unajionesha wazi katika matukio yote ya ibada ya hija; kauli na vitendo vyake.  

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU