Kuna hekima gani kwenye matendo ya sala?

Dear Brother / Sister,
Maana ya Matendo katika Sala: Kila nguzo na sehemu ya sala ina hekima zake mahususi,
Moja ya majina ya Allah ni al-Hakim (Mwingi wa Hekima). Yaani, kwa hakika anapangilia na kuumba hekima nyingi, mapendefu na malengo ya kila tendo ni Vyake. Ni kweli kwamba kuna maelfu ya hekima katika amri Yake na makatazo yake. Kuna maana nyingi katika kila tendo la sala, ambayo ndio ibada muhimu zaidi.
Tunaweza kuziorodhesha kama ifwatavyo:
Sala ndio nguzo ya dini. Kama tutafikiria kwamba Kaaba ndio nguzo ya ulimwengu, tutafahamu hekima ya kuligeukia Kaaba wakati wa kusali.
Kunyanyua mikono yetu tukiwa tunasema takbir (Allahu akbar) kunamaanisha tunavirusha vitu vya kidunia nyuma yetu na kusimama kusali kwa ajili ya Allah.
Tukisimama kwa miguu yetu, tunawakilisha namna miti inavyoabudu, milima na malaika ambao daima huabudu wakiwa wamesimama.
Tunapoinama, tunaiwakilisha ibada ya wanyama kama ngamia, mbuzi na kondoo namna wanavyoabudu, na malaika mara zote huabudu kwa kuinama.  
Tunaposujudu, tunaiwakilisha ibada ya mnyama anaetambaa, majani na malaika ambao daima huabudu wakiwa wanasujudu.   
Tunapoketi, tunaiwakilisha ibada ya viumbe vyote kwa Allah kwa niaba yetu wenyewe. Mwishowe, tunapotoa salamu upande wa kulia na kushoto, tunautolea salamu ulimwenu mzima.
Isitoshe, tunaposali, tunaufanya mwili wetu na kila kiungo chake kuabudu.
Kusimama na kusoma Quran kwenye sala pia kuna maana. Kuna hekima maalumu kwenye kuinama/kurukuu baada ya kusimama na kusujudu baada ya kurukuu, kunamaanisha kuwa karibu mno na Allah…
Mwanaadamu, akiwa katika hali ya kuiwakilisha ibada kuu inayotekelezwa ulimwenguni kote, anatekeleza kwa Mwingi-wa-Rehema-Mwenye-Kurehemu ibada ambayo inaendelea kuchukua nafasi mwilini mwake pamoja na kuabudu kwa viumbe hai na viumbe tunavyovizingatia kuwa sio hai mara tano kwa siku.
1. KUSIMAMA (QIYAM)
Kwanza, tunasimama, tunanyanyua mikono na kusema Allahu akbar (Allah ndio mkubwa kuliko wote). Hapo, mwanaadamu hurusha nyuma kila kitu isipokuwa Allah na kujielekeza kwa amri Yake na utashi. Utumwa na uja umewekwa hivyo. Hapo, ibada ya viumbe vyote ndio huwakilishwa.  
2. KUINAMA (RUKU)
Baada ya kumsifu Allah kama Anavyostahiki, mwanaadamu hijisikia unyonge kwenye uwepo wa kiburi anachokiinamia kukionesha na kukiinamisha kichwa chake kama ni alama ya heshima na kusema Subhana Rabbiyal-Azim (Utakasifu ni wake Mola Mlezi, Aliye Mkuu). Muumini anaiwakilisha ibada ya viumbe vyote wanaorukuu kwa kufanya hivyo.
3. KUOMBA KWA UNYENYEKEVU (DUA)
Kisha, ananyooka, na kumshukuru na kumsifu Allah kwa sababu Amemwongoza mja kwenye njia iliyonyooka. Kwa muda fulani, anatafakuri, akiwa amesimama, kiburi na utukufu wa Allah na uwepesi na uchache wa tendo lake, kisha anatishiwa.
4. KUSUJUDU (SAJDAH)
Anasujudu na kuweka paji lake la uso chini akijisikia staha na udhaifu kikamilifu na kusema,
‘Subhana Rabbiyal-Ala (Utakasifu ni wa Mola Mlezi, Aliye Mkuu).
5. KUKETI NA KUTOA SALAMU
Baada ya kurudia matendo hayo kwa mpangilio, anajikuta yuko mbele ya Allah pasi na viunganishi vyovyote na kumwomba Yeye msaada.
Vinapokutana viumbe viwili, husalimiana. Katika upande mmoja wa sala (kuketi), anaesali hurudia ibara hizo hizo za salamu ambazo zimetumika kati ya Mtume Muhammad (s.a.w.) na Allah wakati wa safari ya Miraji (kupaa mbinguni):
(Maamkizi mema yote, sala na wema ni wa Allah. Amani iwe juu yako, Ewe Mtume na rehema za Allah na baraka Zake. Amani iwe juu yetu na juu ya waja wema wa Allah!)
Matendo ya mwili katika sala:
Kuna matendo 4 katika sala. Tendo la kwanza ni qiyam, ambalo ni, kusimama. La pili ni ruku (kuinama). La tatu ni sijdah ya kwanza (kusujudu) na la nne ni sijida ya pili. (Fususulhikam,  2/476-477)
Kwenye kisimamo katika sala, kichwa kinamwashiria Mola Mlezi na miguu inawaashiria watu. Mwanaadamu, anayeyachanga matendo yote katika kisimamo, anasoma Quran (qira’ah), ambayo ni fard, katika hatua hii. Anatimiza fard mbili: qiyam na qira’ah.
Kama ilivyo ruku’, inamaanisha kuitenda hali ya wanyama katika sala. Katika hatua hii, miguu ya wanyama inatazama kwenye kitovu cha ardhi, na mwelekeo wa viwiliwili vyao viko kimlalo. Inamaanisha, wanyama husimama sambamba na mvuto wa dunia. Wakiwa wamesimama namna hiyo, kichwa cha mnyama hakitazami eneo wala mvutano wa dunia. Ni hali inayowahusu wao. Kwa nini tunatenda hivyo ilhali sisi ni wanaadamu? Swali kama, ‘Wanyama ni nani kwetu?” linaweza kuibuka. Jawabu ni ifwatavyo: mwili wa mwanaadamu, ambao ni kifupi cha wanyama 18 elfu, una roho ya kinyama inayoishi duniani. Roho hiyo, inayoitwa nafsi kwa upande wa matamanio, haiwezi kupandikizwa kwa binaadamu isipokuwa iwe imesafishwa. Atatakiwa ale kidogo, alale kidogo na ajamiiane kidogo ili awe mbali na upande wa mnyama, ambao ni karibu na dunia. Kisha, atakuwa katika hali ya kusafishwa. Salah (kusali), ambayo ni ibada inayoefahamika, inatakiwa itende uwepo wa mnyama ndani yake.
Hekima ya sajdah; mtu anaposujudu, kichwa kinakwenda chini sawa na kiwango cha miguu. Mtu hutenda hali hii ambayo ni kusujudu kwa mimea.
Kusujudu mara ya pili ni kukosa uhai. Lenyewe halina tendo. Yaani, hakuna tendo linakuja kutoka ndani yake. Inafanya kama ni matokeo ya nguvu kutoka nje. Inayojumuisha mbale ndani ya mawe na sakafu. Mbale inamilikiwa na kitu kinachoitunza isipokuwa ikiyeyushwa kwa kuwa ipo katika hali ya mtawanyiko katika vitu visivyo hai. Elementi ya kila mbale ina roho kwa upande wa atomi zake.
Kusujudu mara ya pili ni kama ya kwanza kwa sababu mimea na vitu visivyo hai viko pamoja; havina matendo kama wanyama. Kila sayari, nyota na vinavyofanana angani havina uhai. Kusujudu ni kukubwa kama kilivyo kiwango chao.
Kwa kuongezea, sala (salah) ni aina ya ibada inayojumuisha mwanaadamu, wanyama na viumbe vyote. Hata hivyo. Inafahamika kwa kutimizwa kimoyomoyo na kiroho na sio kimwonekano.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU