KUMUAMINI ALLAH

Kusujudu ni miongoni mwa dalili kubwa za unyenyekevu kwa Muumba.

Maana ya Kumuamini Allah:

Ni imani thabiti ya kuamini kuwepo kwa Allah alietukuka na kukubali kuwa yeye ndiye Mola, ndiye muabudiwa, pia kuamini majina na sifa zake.
Tutayazungumzia mambo haya manne kwa ufafanuzi kama ifuatavyo:
  1. Kuamini Uwepo wa Allah subhanahu wa’taala

Kukubali kuwepo kwa Allah Mtukufu ni jambo la kimaumbile kwa mwanadamu lisiliohitaji kujikalifisha katika kulitolea ushahidi. Na kwa sababu hii, watu wengi sana wanakiri kuwepo kwa Allah pamoja na kutafautiana dini zao na madhehebu yao.

Sisi tunahisi kutoka ndani ya nyoyo zetu kwamba Allah yupo; tunamkimbilia katika shida na majanga kwa maumbile yetu yanayoamini na silka ya kuamini dini ambayo Allah ameiweka katika nafsi ya kila mwanadamu, japokuwa baadhi ya watu wanajaribu kuififiliza na kuipuuza.
Nasi tunasikia na tunaona katika majibu ya wanao omba dua, wapewayo waombaji na wenye matatizo kutatuliwa shida zao tunasikia na kuona mambo ambayo yanatoa ushahidi wa yakini juu ya kuwepo kwa Allah. .
Ushahidi wa kuwepo kwa Allah uko wazi zaidi usiohitaji kutajwa na kuhesabiwa. Miongoni mwa ushahidi huo ni huu:
  • Ni jambo linalojulikana kwa kila mtu kwamba tukio lolote halina budi kuwa na aliyelitenda. Viumbe vyote hivi vingi na ambavyo tunaviona kila wakati ni lazima vina muumba aliyevifanya viwepo, naye ni Allah. Ilivyo ni kwamba haiwezekani kuwa vimeumbwa bila ya muumba aliyeviumba. Kama ambavyo pia haiwezekani kuwa vimejiumba vyenyewe, kwa sababu kitu hakijiumbi chenyewe, kama Allah alivyosema kuwa: «Au wameumbwa bila ya jambo au wao ndio waumbaji?». (Sura Attuur, aya 35). Maana ya aya ni kwamba wao hawakuumbwa bila ya muumbaji, wala wao pia hawakujiumba wenyewe. Hivyo, inalazimika kuwa muumba wao ni Allah.
  • Mfumo wa huu ulimwengu kwa mbingu zake, nyota zake na miti yake unatoa ushahidi usiokuwa na shaka kwamba huu ulimwengu una muumba mmoja, naye ni Allah. «Utengeneaji wa Allah ambaye amekitengeneza vizuri kila kitu». (Sura Annamli, aya 88).
Hizi sayari na nyota, kwa mfano, zinatembea katika mpangilio madhubuti usiotetereka. Kila sayari inatembea katika njia ambayo haiikeuki na haiipitilizi.
Allah anasema kuwa: Si jua linalotakiwa kuuwahi mwezi na si usiku unaoutangulia mchana. Na kila kimoja katika njia kinatembea». (Sura Yasin, aya 40).
  1. Kuamini kuwa Allah ni mola:
Maana ya kuamini kuwa Allah ni Mola:
Ni kukubali na kuamini kuliko thabiti kwamba Allah ni Mlezi wa kila kitu, mmiliki wake, muumba wake, anayekipa riziki na kwamba yeye ndiye mletaji uhai, mletaji kifo, mletaji manufaa, mletaji madhara, ambaye mambo yote ni yake yeye, naye anaweza kila jambo, hana mshirika katika hayo.
Kwa hiyo, imani hiyo ni kuamini kuwaa Allah ni pekee katika matendo yake, na hiyo ni kwa mtu kuwa na itikadi kwamba:
  • Allah peke yake ndiye muumba wa vyote vilivyopo ulimwenguni, na hakuna muumba mwengine, kama Allah alivyosema kuwa: «Allah ndiye muumba wa kila kitu». (Sura Azzumar, aya 62).
    Ama utengenezaji wa mwanadamu ni wa kugeuza kutoka katika sifa fulani kwenda kwenye sifa nyingine au kukusanya na kuunda, na mfano wa hayo, na sio uumbaji wa kweli na sio kuumba kutoka kisichokuwepo, na sio kuleta uhai baada ya mauti.
  • Na yeye ndiye mwenye kuvipa riziki viumbe vyote, na hakuna mtoaji riziki asiyekuwa yeye, kama Allah anavyosema kuwa: «Na hakuna kitu mbaacho katika ardhi isipokuwa kwamba ni juu ya Allah riziki yake».  (Sura Huud, aya 6).
  • Na yeye ndiye mmiliki wa kila kitu, na hakuna mmiliki wa kweli asiyekuwa yeye, ambapo Allah anasema kuwa: «Ni wa Allah tu umiliki wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yao». (Sura Almaida, aya 120).
  • Na kwamba yeye ndiye mwendeshaji wa kila jambo, na hakuna mwendeshaji ila Allah pekee, kama Allah alivyosema kuwa: «anatengeneza mambo kutoka mbinguni mpaka ardhini». (Sura Assajda, aya 5).Ama uendeshaji wa mwanadamu kwa mambo yake, maisha yake na kuyapangilia umefungika na unahusika tu na mambo yaliyopo ndani ya uwezo wake na ambayo anayamiliki na kuyaweza. Uendeshaji huo unaweza kufanikiwa na unaweza kufeli. Lakini uendeshaji wa Allah Mtukufu ni mpana, hakuna kinachoweza kujitoa, na ni wenye kufanyika; hakuna kinachoweza kuuzuia au kuukwamisha, kama Allah Mtukufu alivyosema kuwa: «Ee! Ni kwake yeye tu kuumba na kuamrisha. Ametukuka Allah Mola wa walimwengu». (Sura Al-aaraf, aya 54). 

Makafiri wa Kiarabu wakati wa Mtume swallalahu alayhi wasalam walikuwa wakikiri kwamba Allah ndie mola mlezi wa ulimwengu:

Makafiri wakati wa Mtume wa Allah swallalahu alayhi wasalam, walikiri kwamba Allah ndiye Muumba, Mmiliki na Muendeshaji mambo. Hilo pekee halikuwaingiza katika Uislamu, kama Allah alivyosema kuwa: «Na kwa yakini kabisa, ukiwauliza: Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka yoyote, watasema: Ni Allah». (Sura Luqman, aya 25).
Kwa sababu aliyekiri kwamba Allah ni Mola wa walimwengu, kwa maana ya kuwa ni Muumba wao, Mmiliki wao na Mlezi wao kwa neema zake inamlazimu kumkusudia yeye peke yake kwa ibada na kumfanyia ibada hizo yeye tu asiyekuwa na mshirika.
Ni vipi iingie akilini kwamba mtu anakiri kwamba Allah ni Muumba wa kila kitu, Muendeshaji wa ulimwengu, Mletaji uhai na Mletaji mauti halafu mtu huyo anafanya jambo katika aina za ibada kumfanyia asiyekuwa Allah? Hii ndio dhuluma mbaya sana na dhambi kubwa sana. Kwa sababu hii, Luqman alimwambia mwanae akimpa nasaha na maelekezo kwamba: «Ewe kijana wangu, usimshirikishe Allah Kwa yakini, ushirika ni dhuluma kubwa». (Sura Luqman, aya 13).
Na Mtume, swallalahu alayhi wasalam alipoulizwa kwamba: Ni dhambi gani kubwa sana mbele ya Allah? Alisema: «Ni wewe kumfanyia Allah mshirika na ilhali yeye ndiye aliyekuumba». (Bukhari hadithi Na. 4207. Muslim Hadithi Na. 86).

Kuamini kuwa Allah ni Mola kunazipa nyoyo utulivu:

Mja akijua kwa yakini kwamba haiwezekani kwa kiumbe yeyote kuyaepuka aliyoyapanga Allah kwa kuwa Allah ndiye Mmiliki wao anayefanya atakavyo kwa mujibu wa hekima na busara zake, naye ndiye Muumba wao wote na kwamba kila asiyekuwa Allah basi ameumbwa au kimeumbwa hivyo kinamhitaji Muumba wake na kwamba mambo yote yako mkononi mwa Allah; hakuna Muumba ila yeye tu, hakuna mtoaji riziki ila yeye tu, hakuna muendeshaji ulimwengu ila yeye tu, hakuna chembechembe yoyote inayotikisika ila kwa idhini yake na hakuna inayotulizana ila kwa amri yake tu, hilo linaacha katika moyo wake uhusiano na Allah pekee, kumuomba, kumhitaji, kumtegemea katika mambo yote ya maisha yake, kupambana na kuwa na bidii katika harakati za maisha kwa utulivu, ari na bidii, kwa sababu  mwanadamu ametekeleza sababu ya kutafuta anayoyataka katika mambo ya maisha yake na amemuomba Allah ili amtekelezee matakwa yake, basi amekwisha tekeleza wajibu wake. Hapo, nafsi yake inatulia na kuacha kuyakodolea macho mambo yaliyoko kwa watu wengine. Mambo yote kwa ukweli yako kwa Allah,anaumba atakayo na anachagua.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU