Jihad inamaanisha nini? Ni zipi Aina za Jihad?

Jihad ni jina linaloitiwa kila shughuli na harakati katika njia ya Allah (SWT). Linamaanisha kutoa bidii ili kuinyanyua haki na kuifanya itawale. Kwa maneno mengine, jihad ni kufanya kwa vitendo katika Uisilamu; ni nguvu ya Uisilamu ili kutenda.
Neno jihad mara nyingi linafasiriwa kuwa ni “vita vitakatifu” kwa lugha za Magharibi. (1) Ufasiri huo unatokana na juhudi ili kuonesha kuwa Uisilamu ni dini inayoenea kwa mabavu ya silaha.
Hata hivyo, maana ya neno “jihad” sio “vita.” Kupigana kwa ajili ya Allah (SWT) pia ni namna ya jihad lakini, kwa maana jumla, neno hili linahusisha mchakato wowote na kitendo ili kuifanya dini ya Allah ienee kila pahala.
1- Abu’l Ala Mawdudi, Jihad katika Uisilamu, Machapisho ya Kiisilamu LTD, Lahor, uk.1; Rudolph Peters, İslam ve Sömürgecilik (Uisilamu na Ukoloni), Kilichofasiriwa na Süleyman Gündüz, Nehir Pub. ist.1989, uk.29; M.J. Kister, "Mali ya Ardhi na Jihad" , Jarida la Kiuchumi na Historia ya Kijamii ya Mashariki, Leiden, 1991, XXXIV, 276; W. Montgomery Watt, Nadharia ya Siasa ya Kiisilamu, Edinburgh, p. 14; Ahmet Özel, İslam Hukukunda Milletlerarası Münasebetler ve Ülke Kavramı (Mahusiano ya Kimataifa Katika Sheria ya Kiisilamu na Dhana ya Nchi), Marifet Pub. Ist. Uk. 64
Aina za Jihad
1. Jihad dhidi ya Ujinga: Jihad hii inamaanisha kuwafundisha watu ukweli na mambo mazuri. Allah Mtukufu anamhutubia Mtume wake katika Quran kama ifuatavyo:
“Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hikima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora.” (an-Nahl, 125)
Yafuatayo yanaelezwa katika aya nyengine:
“Na uwe kutokana na nyinyi umma unao lingania kheri na unao amrisha mema na unakataza maovu. Na hao ndio walio fanikiwa.”  (Aal-i Imran, 104)
Quran ni dawa ya roho inayotosha kutibu kiyakinifu na kiroho, na majeraha ya mtu mmoja mmoja na ya kijamii sio tu kwa taifa fulani mahususi bali watu wote hadi Siku ya Kiama. Wajibu wa kuwasilisha dawa hii kwa watu wamepewa Waisilamu.
2. Jihad dhidi ya Nafsi ya Mtu: Waumini wanaonywa dhidi ya njama za nafsi katika aya kama ifuatavyo: “… wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Mwenyezi Mungu.” (Sad, 26)
Mtume (s.a.w.) ameeleza yafuatayo “jihadi kubwa zaidi ni ile dhidi ya nafsi yako.” Pia amesema, “Adui mkubwa ni nafsi yako, ambayo imo ndani mwako.” (Ajluni, Kashfu’l-Khafa, Beirut, I, 143, Hadith Nambari: 413)
Mtume amevutia umakini juu ya umuhimu wa jihad hii. Kwa hakika, wakati wa kuridi mapiganoni, Mtume (s.a.w.) alisema, “Tumerudi kutoka jihad ndogo kuja kwenye jihad kubwa kabisa.” (Kanzu’l-Ummal, IV, 430, Hadith Nambari: 11260 ) Hivyo, alielezea kwa kifupi kuwa mtu kuishinda nafsi yake lilikuwa ni suala zito zaidi na muhimu zaidi kuliko kupigana na adui.
3. Jihad dhidi ya Shetani: Aya ifuatayo katika Quran inaonesha kuwa Shetani ni adui mkubwa kabisa kwa mwanadamu. “Hakika Shet’ani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui.” .”(Fatir, 6 ) Hivyo, umakini unavutwa kwenye ukweli kuwa jihad kubwa zaidi ni ile inayofanywa dhidi ya adui mkubwa zaidi.
4. Jihad ya Silaha: Jihad hii sio yenye kuendelea. Sio faradhi kwa kila mtu. Kama dola lina nguvu ya kutosha, jihad ni fard al-kifayah (fardhi ya kujitosheleza); yaani, kundi la watu fulani linaposimamisha jihad, watu wengine hawabebeshwi jukumu.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU