Je unaweza kuelezea kuhusu umuhimu unaowekwa na Uislamu kwenye sayansi na teknolojia? Je, dini ya Uislamu ndio sababu ya ujinga na kutokuendelea kwa dunia ya Kiislamu hivi leo?

Dear Brother / Sister,
Chanzo cha maendeleo ni elimu na sayansi. Adui mkubwa zaidi wa watu ambaye lazima wamwepuke ni ujinga kwa sababu kikwazo cha maendeleo yote na mageuzi na chanzo cha mwinamo ni ujinga. Katika mamia ya aya, Quran tukufu inawahimiza wanadamu wajifunze sayansi zinazohusiana na dini na dunia. Tutazinukuu mbili kati ya hizo:
"Ati watakuwa sawa wale wanao jua na wale wasio jua?" (Az-Zumar, 9)
"Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui." (An-Nahl, 43)
Mtume wetu Mohammad (S.A.W) ana Hadithi nyingi zenye kuwahimiza watu wajifundishe sayansi. Baadhi yake ni kama ifuatavyo:
"Tafuteni elimu tangu utotoni mpaka mfikwe na mauti.
Kila kitu kina njia. Njia ya kwenda Peponi ni elimu na sayansi.
Tafuteni elimu hata mpaka China."
 (Bayhaqi, Shuabul-Eeman, Beirut, II. 254)
"Hekima ni mali iliyopotea ya muumini. Huichukua popote anapoikuta." (Tirmidhi, Ilm 19)
"Kutafuta elimu ni faradhi kwa kila Muislamu mwanamume na mwanamke." (Ibn Majah, Muqaddima, 17)
Kama inavyojulikana, Mtume wetu Mohammad (S.A.W) alipofika Madinah, kwanza alijenga madrasah pamoja na msikiti wake. Wanafunzi waliosoma katika madrasah hiyo kwa wakati huo waliitwa watu wa Sofa (Suffa). Watu hao wote walijitolea maisha yao katika elimu na ufahamu. Madrasah ya Sofa ndio msingi wa madrasah zote za Kiislamu na shule zilizofikia leo.
Kama dini ingekuwa ndio kikwazo cha maendeleo, je maendeleo katika enzi za upeo wa furaha, ukamilifu katika Andalusia iliyokuwa mkuu wa Ulaya, ustaarabu wa dola za Seljuk na Uthman zilizoitatanisha dunia ungekuwepo? Je, maelfu ya wanazuoni na wanafalsafa wa kidini kama vile Imamu Ghazali, Ibn-i Sina, Farabi, Imamu Rabbani, Mawlana Jalal-ud-Din Rumi wangeibuka katika dunia ya Uislamu! Badiuzzaman anaeleza kuwa Uislamu hauwezi kuchukulika kuwa unapinga sayansi kama ifuatavyo:
"Mtumwa, mtumishi, mtoto anawezaje kuwa adui na mpinzani wa mkuu wake, kiongozi na baba mtawalia? Kwa hakika, Uislamu ni mkuu na kiongozi wa sayansi na mkuu na baba wa elimu ya kweli." (Muhakemat,10)
Ni kweli kuwa Waislamu leo hawako katika kiwango kinachotakiwa katika nyanja za sayansi na teknolojia lakini si sahihi kudai kuwa Uislamu unahusika na kuwa nyuma huko kimaendeleo.
Baadhi ya duru zainadai kila uvumbuzi wa sayansi kuwa ni ushindi uliopatikana dhidi ya Uislamu. Inaweza kuwa ni kweli kwa dini batili zinazokana sayansi. Hata hivyo, Muislamu huchukulia maendeleo ya namna hiyo kuwa ni "uvumbuzi wa kimwujiza kutoka katika ulimwengu ambao ni kitabu cha uwezo wa Allah". Uvutiwaji na mastaajabu yake kwenye elimu na hekima ya Allah huzidi anaposikia kuhusu vumbuzi mpya.
Kipengele kimoja muhimu cha jambo hilo ni hiki: hakuna kanuni inayowazuia watu dhidi ya sayansis katika Quran, kitabu cha mwisho na kikamilifu miongoni mwa vitavu vya kweli. Hivyo, madai ya baadhi ya watu kuwa Uislamu ni dhidi ya sayansi na teknolojia hayana msingi kabisa na ya makusudi.
Kwa kuangalia karne iliyopita tu ambapo Waislamu waliacha misingi yao - kwa hakika, waliacha misingi yao katika namna iliyopangwa - kutoka katika ari ya Uislamu, na kupuuzia mafanikio na maendeleo yote ya karne kumi na nne si haki.
Maswali juuyau islamu

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU