Je Jihad ni suala la vita tu? Unaweza kutueleza kuhusu Jihad katika mwangaza wa aya za Quran na Hadith?

Dear Brother / Sister,
Baadhi ya waandishi wa Kimagharibi kwa makusudi wanaijadili dhana ya Jihad kuwa ni kama vile suala la vita, na kuzipuuza maana nyengine.  Wakati ambapo, jihad ina maana ya ufahamu zaidi, inakubali kila aina ya mapambano kwa ajili ya Allah. Ambapo, aya za Quran, Hadith, na matendo ya Mtume Muhammad katika maudhui hii yanapewa mazingatio, ni wazi kabisa kuwa Jihad haimaanishi vita tu.
Mifano kutoka katika Hadith:

Bibi Aisha aliuliza, Ewe Mjumbe wa Allah, tunaiona Jihad kuwa ni amali bora zaidi, je tusijiunge nayo? Akajibu, Lakini, Jihad bora zaidi ni hajj timilifu (kuhiji mjini Makkah). (Sahih Al-Bukhari Jihad, 2784)
Katika hadith nyengine, inaelezwa kuwa, Kweli, maneno ya kweli na haki ni Jihad kubwa kabisa hususani inaposemwa mbele ya mtawala dhalimu. (Tirmidhi's Kitabu'l-Fitan) Hadithi nyengine ya aina yake ilisimuliwa na Abdullah bin Amr, Mtu mmoja alikuja kwa Mtume kumuomba ruhusa aende Jihad. Mtume aliuliza, “Je wazazi wako wako hai?” Akajibu ndio kwa kutilia mkazo. Mtume akasema, “Pambana na nafs yako (uovu wako) ili uwatimizie haki zao” (Sahih Al-Bukhari Jihad, Juzuu ya 4, Kitabu 52, Nambari 248)
Inasimuliwa kwenye mamlaka ya Tariq b. Shihab: Alikuwa ni Marwan aliyeanzisha (tendo la) kutoa hotuba kabla ya sala ya sikukuu ya ‘Id. Mtu mmoja akasimama na kusema: Sala inapasa iitangulie hotuba. Marwan akasema, Hili (tendo) limeshatendeka. Huku haya yakitokea Abu Sa’id akasema: Mtu huyu ameshatimiza (wajibu wake) alionao. Nimemsikia Mjumbe wa Allah akisema: Yeyote atakayeona uovu basi anapaswa ausawazishe kwa mkono wake; na kama hawezi hivyo, basi anapaswa ausawazishe kwa ulimi wake, na kama hakuweza hivyo, basi (hata) kwa kuchukia kwa moyo wake, na hii ni imani finyu kabisa. Sahih Muslim Imani, Kitabu 001, Nambari 0079-80)
Hadithi hizi zinapotegemewa, itaonekanwa kwamba Jihad ina maana pana, inayojumuisha aina zote za bidii kwa ajili ya Allah.
Jihada maana yake ni kujibiidisha au kupambana kwa Kiarabu, linatokana na mzizi Jahd.
Jihad, kwa maana pana zaidi, ni kujibidiisha kupitia njia ya Allah, kutimiza wajibu wa uja kwa Allah, kupambana na vyote viwili uovu wa nafsi na Shetani, kuishi na kuakisi roho ya mfumo wa maisha ya Kiisilamu kwa kufuata kigezo cha Mtume Muhammad, kuwalingania watu kuja katika Dini, kuutangaza Ujumbe wa Kiungu kwa watu, kuulinda Uisilamu na Waisilamu dhidi ya uadui wowote unaoweza kutokea na kupigana kwa ajili ya hayo ikilazimika. Katika muktadha huu, Jihad ina sura mbili: Kiroho na Kiyakinifu.
Namna ya Kiroho inahitaji imani kamili na kujisalimisha, unyoofu na usafi, kujitolea nafsi na juhudi kubwa katika dini. (Al-Baqarah Surah, 2:285, 286) Kwa namna hii, inawaandaaa waumini kuwa na imani thabiti na elimu ya kisayansi, ili kuwa makini na wenye kuona mbali, na kuidumisha dini kwa unyoofu wa hali ya juu kuwa ndio kigezo. (Az-Zumar Surah, 2-3) Namna ya Uyakinifu kwa upande mwengine, inachambua umuhimu wa kujiendeleza kiuchumi, kiteknolojia, kitamaduni dhidi ya uchochezi wa maadui unaoweza kutokea.
Dhana ya Jihad katika Uisilamu inarejea katika kipengele kikubwa cha wajibu na majukumu, ambayo yamebainishwa na aya za Quran na Hadithi.
1- Kujaribu kuidumisha Dini kwa ajili ya Allah kwa unyoofu

2- Kusambaza ukweli juu ya kila kitu.

3- Kujitahidi kuwalingania wengine kuja katika Uisilamu, kuwafundisha wasiouju.

4- Kuamrisha mema na kukataza maovu.

5- Kujitahidi kuvumilia matatizo yanayohusu kuwalingania watu kuja kwa Allah na matusi ya watu.

6- Kutangaza elimu ya Ujumbe wa Kiungu wa kuamrisha mema na kukataza mabaya kirafiki zaidi.

7- Kujibidiisha vilivyo ili kuwa juu katika sayansi na teknolojia.

8- Kujiendeleza kiyakinifu ili kushinda katika vita vya kiuchumi na utamaduni.

9- Kuongoza dola kwa busara ya kutoruhusu walanguzi

10- Kujitahidi dhidi ya maadui kwa kutokuwa adui yao kisiasa, kiuchumi, na kijeshi.

11- Kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya uhaini wowote unaoweza kujitokeza na mavamizi ya maadui.

12- Pindi vita vikiwa haviepukiki, haifai kuwakimbia maadui, bali kupigana nao, na kumwamini Allah.
Uongo na tathmini za haraka-haraka juu ya Jihad kama vile ni suala la vita tu ni ukosefu, upungufu na sio sahihi kwa mujibu wa mafundisho ya Quran na Sunnah.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU