2- Ulaghai na kutojua

2- Ulaghai na kutojua

Makusudio yake ni kila mkataba ambao ndani yake kuna sehemu haijulikani au kuna mwanya ambao unaweza ukawa sababu ya kuleta mzozo na ugonvi kati ya pande mbili au mmoja kumdhulumu  mwengine.
Mkataba huu Uislamu umeuharamisha ili kuziba mwanya wa sababu za ugomvi, dhuluma na kupunjana. Mkataba huu ni haramu hata kama watu watauridhia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amekataza biashara za ulaghai. (Muslim, Hadithi Na. 1513).
Uislamu unaharamisha kila mkataba (makubaliano) wenye sehemu isiyofahamika ambayo baadae inaweza kusababisha mzozo na ugomvi.

Mfano wa biashara za ulaghai na kutojua

  1. Kuuza matunda kabla ya kukomaa na kuwa tayari kuchumwa. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amekataza kufanya hivyo, kwa sababu ya uwezekano wa matunda hayo kuoza kabla ya kupevuka. 
  2. Kulipa kiasi fulani cha pesa kwa ajili ya kununua sanduku ambalo haijulikani ndani yake kuna nini; inawezekana kukawa na kitu chenye thamani au kitu kisichokuwa na thamani.

Wakati gani kutojua kunakuwa na athari?

Ulaghai na kutojua hakuwi na athari katika kuifanya mikataba kuwa haramu isipokuwa tu utakapokuwa mwingi na ukawa katika mkataba wenyewe na sio katika viambatanishi vyake. Kwa maana hiyo, inafaa kwa Muislamu kununua nyumba, kwa mfano, hata kama hajui, kama vile rangi n.k. Huku ni kutojua kidogo, na pia kutojua huku kupo katika viambatanishi vya mkataba na sio katika mkataba wenyewe.

3- Dhulma na kuchukua mali za watu kinyume na utartibu

Dhuluma ni katika mambo mabaya sana ambayo Uislamu umeyakataza. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Dhuluma ni giza Siku ya Kiama». (Bukhari, Hadithi Na. 2315. Muslim, Hadithi Na. 2579). Kuchukua mali za watu bila ya haki, hata kama ni kidogo, ni katika madhambi makubwa ambayo mwenye kuyafanya ameahidiwa adhabu kali Akhera. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kudhulumu kipande cha shubiri ya ardhi, atabebeshwa shingoni kipande cha ardhi hiyo Siku ya Kiama kuanzia ardhi ya saba». (Bukhari, Hadithi Na. 2321. Muslim, Hadithi Na. 1610).

Mifano ya duluma katika miamala:

  1. Kughushi na kulaghai watu kwa ajili ya kula mali zao kwa njia batili. Hayo ni miongoni mwa madhambi makubwa. Mtume, swallalahu alayhi wasalams, amesema kuwa: «Mwenye kutufanyia ghushi si mwenzetu» (Muslim, Hadithi Na. 101). Sababu ya Hadithi hii ni kwamba Mtume, swallalahu alayhi wasalam, alikwenda sokoni na kukuta fungu la nafaka. Aliingiza mkono wake katika fungu hilo la nafaka na kukuta umajimaji humo. Alimuuliza mfanyabiashara kwamba: Ni nini hiki ewe mwenye nafaka hizi? Mfanyabiashara akajibu kuwa: Zimenyeshewa na mvua ewe Mtume wa Allah. Mtume akasema: Kwa nini hukuziweka juu watu wakaziona? Halafu Mtume akasema: Mwenye kughushi si mwenzetu». (Tirmidhiy, Hadithi Na. 1315)
  2. Kuchezea sheria kwa kuchukua mali kwa dhuluma na bila ya haki. Hali hii ni kwamba mtu anaweza kuwa na ujanja na umahiri wa hali ya juu unaomuwezesha kuchukua kitu kisichokuwa chake kwa njia ya sheria na mahakama. Lakini, hukumu ya hakimu hauibadilishi batili kuwa haki, kama alivyosema Mtume, swallalahu alayhi wasalam, kuwa: «Hakuna vingine isipokuwa kwamba mimi ni mwanadamu tu kama nyinyi. Na nyinyi mnaleta mashitaka yenu kwangu. Na huenda mmoja wenu akawa hodari zaidi wa kutetea hoja yake kuliko mwenzake, na kwa sababu hiyo, nikampa hukumu ya ushindi kutokana na nilivyo sikia. Yule ambaye nimempa hukumu ya ushindi kwa haki ya ndugu yake, asiichukue, kwa sababu nitakuwa nammegea kipande cha moto». (Bukhari, Hadithi Na. 6748. Muslim, Hadithi Na. 1713)
  3. Kutenza nguvu (Kushurutisha): Haifai kutenza nguvu katika muamala kwa namna yeyote ile ya ushurutishaji na ukandamizaji. Mikataba haiwi sahihi isipokuwa tu kwa kuridhiana. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakuna vingine isipokuwa kwamba  biashara ni kwa kuridhiana». (Ibnumaaja, Hadithi Na. 2185).
  4. Rushwa: Ni mtu kutoa mali au huduma ili apate haki isiyokuwa yake. Rushwa ni miongoni mwa aina mbaya sana za dhuluma na ni miongoni mwa madhambi makubwa sana. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amemlaani mtoa rushwa na mpokea rushwa. (Tirmidhiy, Hadithi Na. 1337)
Rushwa inapoenea katika jamii fulani, jamii hiyo hukumbwa na ufisadi, mvurugiko na kudumaa. 

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUSWALI HATUA KWA HATUA

Maana ya kufunga Maana ya kufunga katika Uislamu: Ni kufanya ibada kwa ajili ya Allah kwa kujizuia na kuacha kula, kunywa, kujamiiana, pamoja na vitu vyote vyenye kufunguza, kuanzia kuchomoza kwa alfajiri –ambao ni muda wa adhana ya Alfajiri- mpaka kuzama kwa jua – ambao ni muda wa adhana ya Magharibi-. «...Basi atakayekuwa katika mji (hayuko safarini) miongoni mwenu katika mwezi (wa Ramadhani) aufunge». Sura Albaqara, aya 185. Ubora wa mwezi wa Ramadhani Mwezi wa Ramadhan ni mwezi wa tisa katika miezi ya mwezi muandamo katika kalenda ya Kiislamu. Ni mwezi bora zaidi katika mwaka. Allah ameuhusisha peke yake kuliko miezi mingine kwa sifa nyingi bora na za kipekee, na miongoni sifa hizo bora ni hizi: Kwamba Ramadhan ni mwezi ambao Allah ameuhusisha na kushuka kwa Qur’ani kitabu kitukufu na bora kuliko vitabu vyote. Allah Mtukufu amesema kuwa: «Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur’ani ikiwa ni muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za muongozo na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini miongoni mwenu katika mwezi huu, basi afunge». (Sura Albaqara, aya 185) Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Utakapoingia mwezi wa Ramadhani milango ya pepo hufunguliwa, na milango ya Jahanamu hufungwa, na mashetani hufungwa minyororo». (Bukhari, Hadithi Na. 3103, Muslim, Hadithi Na. 1079). Hakika Allah ameuandaa mwezi huu kwa waja wake ili waelekee kwake kwa kufanya ibada na kuacha maovu. Kwamba mwenye kufunga mchana wa Ramadhani na akasimama usiku wake (kwa kuswali), Allah humsamehe madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia Mtume amesema kuwa: «Mwenye kusimama (kwa kuswali) katika Ramadhani kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, hadithi na. 1905, Muslim, Hadithi Na. 759). Kwamba ndani ya mwezi wa Ramadhani kuna usiku wenye hadhi kubwa (Lailatul Qadri), usiku ambao ni bora sana kuliko nyakati nyingine za usiku za mwaka mzima. Allah ameeleza katika kitabu chake kwamba kufanya jambo jema ndani ya usiku huo ni bora zaidi kiliko kulifanya jema hilo siku nyingi nyingine. Allah amesema kuwa: «Lailatulqadri ni bora zaidi kuliko miezi elfu moja». (Sura Alqadri, aya 3). Mwenye kusimama katika usiku huo kwa kuamini na kutaraji kupata malipo ya Allah husamehewa madhambi yake. Huo ni usiku uliopo katika siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhani, na hakuna yeyote anayejua tarehe yake kwa uhakika. Ubora wa kufunga «Ambaye hakuacha kusema uzushi na kuutumia hakuna haja kwa Allah katika kuacha chakula chake na kinywaji chake». Kufunga kuna fadhila nyingi ambazo zimeelezwa katika sheria. Miongoni mwazo ni hizi zifuatazo: Kwamba mwenye kufunga mwezi wa Ramadhani kwa kumuamini Allah, kutii amri zake, kuamini fadhila zake zilizotajwa na sheria na kuwa na matarajio ya kupata thawabu kwa Allah, atasamehewa madhambi yake yaliyopita. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga Ramadhan kwa kuamini kutaraji kupata malipo ya Allah, husamehewa madhambi yake yaliyopita». (Bukhari, Hadithi Na. 1910, Muslim, Hadithi Na. 760). Pia mwenye kufunga atafurahia malipo atakayoyapata wakati wa kukutana na Mola wake kwa sababu ya funga yake. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mwenye kufunga ana furaha mbili: furaha wakati wa kufungua kwake na furaha wakati wa kukutana na Mola wake». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Peponi kuna mlango unaoitwa Arrayaan. Haingii yeyote kupitia mlango huo isipokuwa tu wenye kufunga. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Hakika, peponi kuna mlango unaoitwa Arrayyaan. Wenye kufunga wataingia kupitia mlango huo Siku ya Kiama. Haingii yeyote kupitia mlango huo ila wao tu. Patatolewa tangazo kwamba: Wako wapi wenye kufunga? Watasimama. Hataingia yeyote kupitia mlango huo isipokuwa wao tu. Wakishaingia, utafungwa na hataingia yeyote kupitia hapo». (Bukhari, hadithi Na. 1797, Muslim, Hadithi na. 1152) Pia Allah ameyahusisha kwake yeye tu malipo na thawabu za mfungaji. Ikiwa malipo ya mtu yanatoka kwa Mkarimu, Mtukufu, Mtoaji sana na Rahimu sana, anatakiwa ayafurahie yale ambayo Allah amemuandalia. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, katika Hadithi Qudsiy amesema kuwa: «Matendo yote ya mwanadamu ni yake yeye isipokuwa funga. Funga ni yangu, na mimi ndiye nitakaye itolea malipo». (Bukhari, Hadithi Na. 1805, Muslim, Hadithi Na.1151) Hekima ya funga Allah amefaradhisha kufunga Ramadhani kwa hekima nyingi na faida mbali mbali katika dini na dunia, na miongonimwazo ni hizi: Kuthibitisha kumtii Allah na kumuogopa. Hiyo kutokana na kuwa funga ni ibada ambayo mja anajiweka karibu ya Allah kupitia ibada hiyo kwa kuacha anavyo vipenda, na kuyazuia mataminio yake. Anaidhibti nafsi yake kwa kumcha Allah na kumuogopa kila sehemu na kila wakati, katika siri na katika dhahiri. Kwa sababu hii, Allah Mtukufu anasema kuwa: «Enyi mlio amini, mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kuwa wenye kumuogopa Allah». (Sura Albaqara, aya 183) Mazoezi ya kuacha maasi na madhambi Mwenye kufunga ajizuiapo kufanya mambo yaliyo halali kwa kufuata amri ya Allah atakuwa na uwezo zaidi wa kuyadhibiti mataminio yake ya kutaka kufanya maasi na madhambi, atachunga mipaka ya Allah na hatajiachia katika kufanya maovu. Mtume, swallalahu alayhi wasalam, amesema kuwa: «Mtu ambaye haachi kusema uzushi na kuufanyia kazi, basi Allah hana haja ya kuacha chakula chake na kinywaji chake». (Bukhari, Hadithi Na. 1804). Maana ni kwamba: Mtu ambaye haachi uongo na kufanya uchafu katika kauli na vitendo, huyo hajayafikia makusudio ya funga. Kuwakumbuka wenye shida na kuwasaidia Hiyo inatokana na kwamba katika funga kuna mazoezi ya kupambana na ukata, njaa, na kuwakumbuka maskini ambao wanapambana na hali ya kutokuwa na pato la kutosha siku zote. Kwa kufunga, mja huwakumbuka ndugu zake masikini na namna wanavyoteseka na mambo mawili machungu; njaa na kiu, na kwa sababu hiyo, atafanya juhudi ya kuwasaidia na kuwafariji.

UTUKUFU WA MJI WA MAKKA NA MSIKITI MTUKUFU